Malafyale
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 13,813
- 11,126
RAIS Jakaya Kikwete amesema ahadi zote zilizotolewa na Chama cha Mapinduzi (CCM) zitatimizwa kama ilivyodhamiriwa.
Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Manyoni wakati wa sherehe za kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji katika kijiji cha Mitoo, Rais Kikwete alisema Serikali yake inayodhamira ya kutimiza ahadi kama ilivyoahidi.
Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, ilisema mradi ya maji wa Manyoni umetekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Damu Aziz ya Yesu kwa gharama ya sh. mil. 693 inayohusisha visima nane.
"Tunayo dhamira ya kutimiza ahadi tulizotoa na tutazitimiza kama tulivyoahidi, suala kubwa kwa wananchi wa Manyoni ilikuwa maji na barabara vyote viwili vimekamilika" alisema Rais Kikwete.
Alisema kati ya sh. mil. 610 zinazohitajika kukamilisha kazi ya kuweka bomba kubwa na tanki kabla ya maji hayajasambazwa kwa wananchi, ameahidi kutafuta sh. mil. 300 na Halshauri itafute fedha zilizobaki.
Alisema kufikia mwisho wa mwaka barabara iliyobaki ya kilometa sita itafika Manyoni mjini hivyo kuondoa tatizo la usafiri.
Habari Toka gazeti la Majira
Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Manyoni wakati wa sherehe za kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji katika kijiji cha Mitoo, Rais Kikwete alisema Serikali yake inayodhamira ya kutimiza ahadi kama ilivyoahidi.
Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, ilisema mradi ya maji wa Manyoni umetekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Damu Aziz ya Yesu kwa gharama ya sh. mil. 693 inayohusisha visima nane.
"Tunayo dhamira ya kutimiza ahadi tulizotoa na tutazitimiza kama tulivyoahidi, suala kubwa kwa wananchi wa Manyoni ilikuwa maji na barabara vyote viwili vimekamilika" alisema Rais Kikwete.
Alisema kati ya sh. mil. 610 zinazohitajika kukamilisha kazi ya kuweka bomba kubwa na tanki kabla ya maji hayajasambazwa kwa wananchi, ameahidi kutafuta sh. mil. 300 na Halshauri itafute fedha zilizobaki.
Alisema kufikia mwisho wa mwaka barabara iliyobaki ya kilometa sita itafika Manyoni mjini hivyo kuondoa tatizo la usafiri.
Habari Toka gazeti la Majira