Losomich
JF-Expert Member
- Nov 9, 2011
- 371
- 71
Wana-Arumeru kama Watanzania wengine wote ufisadi pia ni tatizo lao. Hii dhana yako ya mgombea kuwaambia watu atakachowafanyia ndiyo imetufikisha hapa tulipo. Hivi kweli mpaka leo hii wewe unaamini kabisa kwamba mbunge atawafanyia wananchi kitu fulani? Maswala ya maendeleo ni jukumu na mchango wa kila mwananchi mwenye nguvu, akili timamu na afya njema, si jukumu la mtu mmoja aitwaye mbunge.
Watanzania tunatakiwa kuelewa dhana ya kuwajibika kwa pamoja kuleta mabadiliko na hatimaye maendeleo.
Pia kaka mtu yeyote mwaminifu hawezi kuahidi mambo makubwa ili kuwahadaa watu ile hali uwezo wa nchi anaufahamu vizuri. Kuwa rasilimali zote za nchi zimebakwa na mafisadi.