Nilikuwa nacheka hapa kuhusu madiwani wa Arusha kukwamisha kikao cha bajeti. Tatizo ni kwamba lazima wahudhurie wajumbe angalao theluthi mbili. Swali linakuja, kama bila madiwani wa chadema kikao hakiwezi kufanyika maana hakutakuwa na theluthi mbili, je, kikao cha uchaguzi kilifanyika vipi? Mbona CCM wanatuambia kilikuwa halali? Mimi nadhani ni afadhali Chadema waendelee kususia vikao, bajeti ishindwe kupita warudi kwenye uchaguzi kama CCM hawataki ku compromise.