CAG akague hesabu za zoezi zima la Sensa…

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
670
Agosti 23, 2022 tunatarajia kuwa na zoezi la sensa ya watu na makazi. Zoezi muhimu katika mipango ya sera na maendeleo ya Taifa.

Hata hivyo mwaka huu tumeona matangazo yamekuwa mengi sana hadi inaleta maswali kama fedha za umma zimetukima ipasavyo. Uhamasishaji umekuwa mkubwa kama kuna mgomo ulitangazwa, tofauti na mwaka 2012.

Mbali na nguvu kubwa ya matangazo bado pia kumekuwa na Tamasha la Sensabika ambalo limeanza leo ambapo wasanii na wanamichezo wamejazana leaders club kufanya yao.

Wakati huo tozo zimeongezeka kwa kiasi kikubwa na kumuumiza mwananchi, hali inayonipelekea kutoa wito kwa CAG kutupa ripoti ya bajeti nzima ya sensa ili tuone kama tumezingatia.

Natoa wito kwa wote walioko karibu na CAG kumwambia tafadhali atufanyie hili. Isije ikawa watu wanalambishana asali huku wananchi wakiumia.

OLS
 
Haina maana yoyote kwasababu mwisho wa siku ripoti itawekwa kabatini na maisha mengine yataendelea.
 
Wanasalimu ndugu wanajamvi,

Kwanza inasikitisha sana kuona pesa za walipa kodi masikini zinateketea katika zoezi la sensa kama hili. Mwanzo tumefanya hamasa vizuri sana lakini kinachofanyika huku mtaani sasahivi ni sawa na bure.

Kwa maoni yangu nini kimepelekea zoezi la sensa kufeli namna hii,

1. Mchakato wa kuwapata makarani uligubikwa na kujuanajuana bila kuangalia weledi na utashi wa makarani.

2. Usimamizi kuanzia ngazi ya kitaifa mpaka chini ni mbovu sana. Watu wanampa taarifa za uongo Rais kwamba zoezi lipo vizuri. Wakuu wa Wilaya msimdanganye Rais mitandaoni. Hebu imagine kule Bunda karani amejifungua kbl ya zoezi kuanza, sasa huyu alichukuliwaje na wakati alikuwa mjsmzito???

3. Makarani hawana elimu ya kutosha juu ya hii njia mpya ya ukusanyaji wa takwimu za sensa.

4. Uhaba wa makarani nchini na baadhi ya makarani kutokuwa serious na kazi.

Mwisho kabisa, Mhe. Rais, agiza vyombo vya usalama vifanye uchunguzi wa kina juu ya matumizi ya fedha zote za sensa...Hakika kuna upigaji mkubwa sana Mama, Mimi roho inaniuma kuona Waziri wa fedha yupo kimya na wewe unadanganywa zoezi lipo shwari kumbe hakuna kitu huku mitaani hata makarani hakuna mama.

TAFADHALI TUMSAIDIE MAMA. NCHI INALIWA. ZOEZI HILI LA SENSA KAMA RAIS HATAINGILIA KATI BASI NCHI INAENDA PABAYA SANA.
 
....kibaya zaidi yaani makarani wanne wanaenda kwa mtu mmoja, Mkuu wa Wilaya Jokate Mwengelo, hivi kweli tupo serious???, na DC anacheka tu na kupiga nao picha na wakati mamilioni ya wananchi hawajahesabiwa???.
 
....makarani wanashinda kwa watu mashuhuri huku siku zinaenda, na mwisho wa siku hatutafikia hata takwimu za 2012 na mhe. rais utaletewa data za kupikwa. Toa Waziri wa fedha, toa mtakwimu mkuu, muonye kamisaa wa sensa na wasimamizi wote baada ya zoezi hili chunguza. Hii ni aibu kubwa sana. Serikali imetumia billions of money halafu makarani wanashinda wa viongozi na watu mashughuli???. Imeniuma sana
 
Mkuu mbna huku songea kata nyingi watu tumemaliza kaz asubuh tu, mimi ni karani ambaye kazi nimemaliza jana saa 4 asubuh tu, na hamna matukio kama hayo huku, kaz yoyote haikosi dosar mkuu, hayo ndio mambo ya error katika kazi, usicomplicate sana maisha, hamna mtu aliyekuwa perfect kwa 100% tuvumiliane kazi itaisha. HAPA KAZI TU na KAZI IENDELEE
 
Mbona mna hasira hivo ndugu wananchi 🥺🤣🤣🤣🤣
Kusubiri nyumbani karani siku Tatu bila mafanikio si mchezo, huku ukitahadharishwa usiposhiriki zoezi la sensa unapewa adhabu!!(Nawaza hasira zaweza kuanzia hapa).
===
Naunga Mkono zoezi la sensa.
 
Back
Top Bottom