Burundi: Nkurunziza ahairisha uchaguzi

RUCCI

JF-Expert Member
Oct 6, 2011
1,701
1,714
Rais wa Burundia Pierre Nkurunziza amehairisha uchaguzi wa ubunge kwa siku kumi .

Msemaji wa rais Willy Nyamitwe ameiambia shirika la habari la AFP kuwa kufuatia jaribio la mapinduzi juma lililopita na vurugu zilizofuatia ni bora kuahirisha uchaguzi huo kwa muda.

''Uchaguzi huo wa ubunge ulikuwa umeratibiwa kufanyika tarehe 26 mwezi Mei lakini sasa inatubidi kuihairisha ili kuwasikiza washirika wetu wa kimataifa pamoja na tume ya uchaguzi ambayo pia inatumia muda huo kutatua maswali yaliyoulizwa na vyama vya upinzani.'' alisema Nyamitwe.

Hadi kufikia sasa tarehe rasmi ya uchaguzi wa urais uliopangwa kufanywa Juni tarehe 26 haijabadilika.

''Subiri tu'' Nyamitwe aliwaambia waandishi wa habari.

Mwandishi wa BBC aliyeko huko Ruth Nesoba amesema kuwa tayari rais Nkurunziza ametia sahihi amri hiyo ya kuhairishwa kwa uchaguzi.

Umoja wa mataifa ya bara Ulaya EU, na Umoja wa mataifa ya Afrika AU, yametoa wito kwa uchaguzi huo uliokumbwa na utata mkubwa uhairishwe ilikutoa fursa kwa mazungumzo ya upatanishi kuendelea .

Hapo jana Rais wa Afrika Kusini alitilia pondo hoja hiyo ya kuahirisha uchaguzi akisema ni bora uchaguzi huo uliopangwa ''uhairishwe''.

Takriban watu 20 wameuawa kufuatia makabiliano baina ya polisi na waandamani katika mji mkuu wa Bujumbura kilele ikiwa ni juma lililopita makamanda waasi walipotangaza jaribio la mapinduzi rais

Nkurunziza akiwa mjini Dar es Salaam kuhudhuria mkutano wa viongozi wa kanda uliolenga kutatua mzozo wa kisiasa nchini mwake.

Wapinzani wa rais Nkurunziza wanasema kuwa kutangazwa kwake nia ya kuwania muhula wa tatu unakiuka sheria na makubaliano ya amani ya mwaka wa 2006 yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka 13.

Nkurunzizakwa upande wake anashikilia kukutu kuwa ana haki ya kuwania muhula mwengine kwani muhula wa kwanza hakuchaguliwa na wanainchi bali wabunge.

Takriban watu laki moja wamekimbilia mataifa jirani wakihofia kutibuka upya kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.



Chanzo: BBC
 
Burundi's President Pierre Nkurunziza poses at the President's office in Bujumbura on May 17, 2015. AFP PHOTO| CARL DE SOUZAADVERTISEMENTBUJUMBURABurundian President Pierre Nkurunziza has postponed parliamentary elections by one week to June 2, presidential official Willy Nyamitwe told AFP Wednesday, following weeks of violent protests and a failed coup.Legislative elections had been due on May 26, but were pushed back a week following "a proposal from the electoral commission, to respond to a request from opposition parties, and finally to answer calls of the region and the international community," Nyamitwe said.No decision has been made as to whether a presidential poll set for June 26 would also be delayed. "Wait and see," Nyamitwe said.The European Union joined the African Union on Tuesday calling for a delay to the elections, while South Africa's President Jacob Zuma said they should be "postponed indefinitely" after a meeting of Africa's Great Lakes bloc of nations.
 
Yaani kasogeza mbele wiki moja? Tena wa ubunge wakati wa urais ambao ndo chanzo cha gogoro lote wamebaki kimya? Hawana nia ya kupata amani nchini kwao hawa jamaa
 
Hilo ni jambo jema lakini linalosubiriwa kwa hamu na wanademokrasia na wapenda amani duniani kote ni kuahirisha kwa uchaguzi wa Rais uliopangwa kufanyika juni 26 na yeye Nkuruzinza kutogombea tena kwa muhula wa tatu
 
Hilo ni jambo jema lakini linalosubiriwa kwa hamu na wanademokrasia na wapenda amani duniani kote ni kuahirisha kwa uchaguzi wa Rais uliopangwa kufanyika juni 26 na yeye Nkuruzinza kutogombea tena kwa muhula wa tatu

Afu mgombee nyie mbona MNA wivu na mwenzenu. Agombee yeye tu
 
Rais wa Burundia Pierre Nkurunziza amehairisha uchaguzi wa ubunge kwa siku kumi .

Msemaji wa rais Willy Nyamitwe ameiambia shirika la habari la AFP kuwa kufuatia jaribio la mapinduzi juma lililopita na vurugu zilizofuatia ni bora kuahirisha uchaguzi huo kwa muda.

''Uchaguzi huo wa ubunge ulikuwa umeratibiwa kufanyika tarehe 26 mwezi Mei lakini sasa inatubidi kuihairisha ili kuwasikiza washirika wetu wa kimataifa pamoja na tume ya uchaguzi ambayo pia inatumia muda huo kutatua maswali yaliyoulizwa na vyama vya upinzani.'' alisema Nyamitwe.

Hadi kufikia sasa tarehe rasmi ya uchaguzi wa urais uliopangwa kufanywa Juni tarehe 26 haijabadilika.

''Subiri tu'' Nyamitwe aliwaambia waandishi wa habari.

Mwandishi wa BBC aliyeko huko Ruth Nesoba amesema kuwa tayari rais Nkurunziza ametia sahihi amri hiyo ya kuhairishwa kwa uchaguzi.

Umoja wa mataifa ya bara Ulaya EU, na Umoja wa mataifa ya Afrika AU, yametoa wito kwa uchaguzi huo uliokumbwa na utata mkubwa uhairishwe ilikutoa fursa kwa mazungumzo ya upatanishi kuendelea .

Hapo jana Rais wa Afrika Kusini alitilia pondo hoja hiyo ya kuahirisha uchaguzi akisema ni bora uchaguzi huo uliopangwa ''uhairishwe''.

Takriban watu 20 wameuawa kufuatia makabiliano baina ya polisi na waandamani katika mji mkuu wa Bujumbura kilele ikiwa ni juma lililopita makamanda waasi walipotangaza jaribio la mapinduzi rais

Nkurunziza akiwa mjini Dar es Salaam kuhudhuria mkutano wa viongozi wa kanda uliolenga kutatua mzozo wa kisiasa nchini mwake.

Wapinzani wa rais Nkurunziza wanasema kuwa kutangazwa kwake nia ya kuwania muhula wa tatu unakiuka sheria na makubaliano ya amani ya mwaka wa 2006 yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka 13.

Nkurunzizakwa upande wake anashikilia kukutu kuwa ana haki ya kuwania muhula mwengine kwani muhula wa kwanza hakuchaguliwa na wanainchi bali wabunge.

Takriban watu laki moja wamekimbilia mataifa jirani wakihofia kutibuka upya kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.



Chanzo: BBC

kizimba cha ICC the Hague kinamsubiri.
 
Back
Top Bottom