Buriani Elimu yetu, Buriani Tanzania na historia yake

TAWA

JF-Expert Member
Jun 23, 2013
3,667
1,566
Unakaribia mwaka sasa toka tuzindue sera mpya ya elimu ambayo inatafsiriwa kwamba ni mpya, utekelezaji wake tunaambiwa utakuwa ni kuanzia mwakani, siyo mbaya yote ni heri. Yaloliolyomo ndani ya sera yenyewe machache ni ya kuchekesha na yanaonesha kabisa kwamba yanakwenda kuua elimu yetu. Kwa mfano:
1. Kuunganisha elimu ya msingi na ile ya srkondari (form one to four) kuwa moja na kuitwa elimu msingi. Hii maana yake hakutakuwa na mkwamo kutoka darasa la saba kwenda sekondari, kwamba yeyote aliyefika la saba huyo anayo sifa ya kujiunga na sekondari. Sasa najiuliza,
. tuna shule za kutosha za sekondari kupokea idadi hiyo ya wanafunzi?
. walimu nao wanatosheleza kama ile ya msingi?
. mfumo wa ufundishaji umeboreshwa vya kutosha na hao wakufunzi wamepewa elimu?
2. Elimu msingi Bure.
Sina tatizo katika hili na hasa kwa huyu raisi wetu. Maana hata yeye amesisitiza "ninaposema bure ni bure kweli". Ila na penyewe pana maswali mengi sana ya kujiuliza lakini kubwa kuliko yote ni "kama tunahitaji elimu bora au bora elimu". Naona kabisa serikali sijui kama itamudu kupeleka Capitation grants za kutosheleza katika haya mashule ya sekondari nchi nzima. Hapo ndiyo mwisho wa elimu yetu, elimu yetu inakufa tukiwa tunaitazama tena kwa sisi tusiojua kilichopo kapuni tunashangilia na kuwasifu wana siasa kwamba wamepunguza ukali wa maisha kwa kuondoa michango ya shule.
Poleni sana watanzania, BURIANI ELIMU YETU, LALA SALAMA.
 
Kwa hilo la hiyo sera mpya ya elimu, ni muhimu watawala waliopo waliangalie upya. Naamini watangulizi wao hawakujipa muda wa kutosha kuliangalia kabla ya kuridhia
 
Tulia we are going back to basics,tunaanza upya na hizi ni hatua za muhimu.
Tutafumua kila mahali, jifunzeni kuvumilia...
 
Inasikitisha kuona baadhi ya watu hawana imani na mipango ya nchi/ serikali.
Hatuwezi kutoka hapa tulipo kama tuandelea kuona kila kitu katika uhasi badala ya uchanya.
 
Ngongo hawa watu unawaelewa wanachokiongea hata mwaka bado? Maana alianza assadsyria3 na leo na bwana Mkubwa TAWA kaibuka na hili. Tuseme wanasimamia misingi au ndiyo maslahi yao yameguswa? Maana lugha ya jingalao na Kina eddy imebaki ile ile lakini hawa wenzao naona kama vili wamepiga"U-turn" sielewi unajua!!
 
Last edited by a moderator:
Elimu bure mpaka chuo kikuu inawezekana, nitaidai ni swala la muda tu. Ngoja Rais wangu Dr Magufuli utumbue majibu kwanza naona usaa tu damu bado haijatoka. Pia tusihujumu elimu yetu ya msingi ibaki ya msingi na sekondari ibaki na hadhi yake.
 
Tulia we are going back to basics,tunaanza upya na hizi ni hatua za muhimu.
Tutafumua kila mahali, jifunzeni kuvumilia...

Batili;
Namkumbuka mwalimu wangu wa Biolojia, wakati wa Practical tulikuwa tunawapaka Chlorofom vyura, tukawapasua tukaangalia sehemu zao za ndani, tukafurahi tukiona moyo unavyo dunda.
Hao walikuwa vyura. Leo Serekali hii tukufu imeamua kuwatoa watoto wetu kafara? Mleta hoja hajakataa sera hii nzuri ya Elimu Bora, Bure kwa kila mtoto wa Kitanzania.
Lakini, elewa, kuna wanafunzi wanao ingia form II na Form IV mwakani. Hao wasihusishwe na mfumo huu mpya. Tatizo kubwa tulilo nalo ni kuwa, hata huyo magufuli sidhani kama alisoma elimu ya bure.
Tulikuwa na hesabu za Cambridge Mathematics au O level mathematics (Pure Maths). Tulipokuwa tuna badilika tukaleta hesabu za SMP Maths. School Mathematics Project. Hesabu tofauti na zile za Mwingereza.
Hatukuingiza hizo SMP haraka au ghafla shuleni. No, tulienda na wale waliokuwa na hesabu zao taratibu mpaka 1968-70 tukamaliza kabisa last banch ya Cambridge Mathematics.
Sasa leo, serekali hii inatangaza badiliko kwa mfumo mzima ati kwa muda chini ya mwezi mmoja.
Naunga mkono kusema BURIANI ELIMU TANZANIA tena nasema R.I.P elimu Tanzania. Naamini, CCM mnataka kutumalizia kabisa tuwe Malofa na Wapumbavu kweli kweli.
HAKUNA JINSI MTAITEKELEZA SERA HII YA ELIMU BURE KWA MTINDO HUU.
 
Unakaribia mwaka sasa toka tuzindue sera mpya ya elimu ambayo inatafsiriwa kwamba ni mpya, utekelezaji wake tunaambiwa utakuwa ni kuanzia mwakani, siyo mbaya yote ni heri. Yaloliolyomo ndani ya sera yenyewe machache ni ya kuchekesha na yanaonesha kabisa kwamba yanakwenda kuua elimu yetu. Kwa mfano:
1. Kuunganisha elimu ya msingi na ile ya srkondari (form one to four) kuwa moja na kuitwa elimu msingi. Hii maana yake hakutakuwa na mkwamo kutoka darasa la saba kwenda sekondari, kwamba yeyote aliyefika la saba huyo anayo sifa ya kujiunga na sekondari. Sasa najiuliza,
. tuna shule za kutosha za sekondari kupokea idadi hiyo ya wanafunzi?
. walimu nao wanatosheleza kama ile ya msingi?
. mfumo wa ufundishaji umeboreshwa vya kutosha na hao wakufunzi wamepewa elimu?
2. Elimu msingi Bure.
Sina tatizo katika hili na hasa kwa huyu raisi wetu. Maana hata yeye amesisitiza "ninaposema bure ni bure kweli". Ila na penyewe pana maswali mengi sana ya kujiuliza lakini kubwa kuliko yote ni "kama tunahitaji elimu bora au bora elimu". Naona kabisa serikali sijui kama itamudu kupeleka Capitation grants za kutosheleza katika haya mashule ya sekondari nchi nzima. Hapo ndiyo mwisho wa elimu yetu, elimu yetu inakufa tukiwa tunaitazama tena kwa sisi tusiojua kilichopo kapuni tunashangilia na kuwasifu wana siasa kwamba wamepunguza ukali wa maisha kwa kuondoa michango ya shule.
Poleni sana watanzania, BURIANI ELIMU YETU, LALA SALAMA.

Mkuuu nakuunga mkono 100% unajua nini kinakuja ila mazwazwa wao wanakenua meno tu kama mazuzu
 
Wamiliki mna Bahati Mbaga kweli first family in walimu wote.hivyo make believe zenu hazina nafasi Tena.muda wa kuishi Kwa ujanja ujanja umeisha,sasakazitu.
 
Nchi hii ina vituko sana sasa unapomuweka shukuru kawabwa waziri wa elimu unategemea nini kama sio ujinga kama huu na mengine mengi kama ya kiu na st Joseph
 
Ngongo hawa watu unawaelewa wanachokiongea hata mwaka bado? Maana alianza assadsyria3 na leo na bwana Mkubwa TAWA kaibuka na hili. Tuseme wanasimamia misingi au ndiyo maslahi yao yameguswa? Maana lugha ya jingalao na Kina eddy imebaki ile ile lakini hawa wenzao naona kama vili wamepiga"U-turn" sielewi unajua!!
Mkuu nina kila sababu kusema kuwa ndugu assadsyria na TAWA ni moja ya majipu yaliyotumbuliwa
 
Sasa kijana atakuwa form three lakini bado atakuwa analia jiwe.
 
Ngongo hawa watu unawaelewa wanachokiongea hata mwaka bado? Maana alianza assadsyria3 na leo na bwana Mkubwa TAWA kaibuka na hili. Tuseme wanasimamia misingi au ndiyo maslahi yao yameguswa? Maana lugha ya jingalao na Kina eddy imebaki ile ile lakini hawa wenzao naona kama vili wamepiga"U-turn" sielewi unajua!!

Mkuu Allen Kilewella nafikiri labda ndiyo mara yako ya kwanza kuona andiko langu humu ndani. Mimi siyo wa mfani wa Jingalao.
 
Last edited by a moderator:
Elimu bure mpaka chuo kikuu inawezekana, nitaidai ni swala la muda tu. Ngoja Rais wangu Dr Magufuli utumbue majibu kwanza naona usaa tu damu bado haijatoka. Pia tusihujumu elimu yetu ya msingi ibaki ya msingi na sekondari ibaki na hadhi yake.

Tafuta sera hiyo mnayoiita mpya, kwanza inajichanganya hasa katika lugha ya kufundishia..........any way..... tafuta uisome, utachoka wewe.
 
Back
Top Bottom