Bunge ni shaghalabagala kwasasa...

Siku kama tatu/nne hivi zilizopita, katibu wa bunge alinukuliwa na vyombo vya habari (TBC1-8PM news bulletin) akisema kuwa maandalizi ya kikao cha bunge yamekamilika na kila kitu kiko sawa! Na alienda mbele zaidi kwa kutaja mambo makubwa yatakayojadiliwa kwenye hiki kikao. Sasa iweje leo wasema ratiba haijakamilika? Kwa vyovyote vile spika atakuwa na mapungufu makubwa katika 'management'. Haiwezekani awe na team inayolipwa mishahara kila mwezi lakini washindwe kufanya maandalizi ya kikao cha bunge kwa wakati! Ni tatizo gani hilio lililoshindikana kutatuliwa wakati wa maandalizi?

Bunge lenyewe linakutana mara chache kwa mwaka sio kama mabunge ya nchi zingine ambao huwa na vikao almost all year round expect miezi mitatu!
 
Huko ndiko wana ccm walikupigania kwakuweka vipengele tata kumzuia sitta kurudi kama spika tena. Na hata hivyo ni somo kabla ya wakati kuwa kuna madai ya uwt kuwa rais ajaye lazima awe mwanamke na ile njama iliyofichika yakumleta migiro kuendeleza dini iliyo bora sana hivi sasa tanzania ambayo imekuwa kama ya serikali. Kwa hili mlionyuma ya hoja ya wanawake wanaweza wakiwezeshwa mjifunze mapema na muache hayo mawazo ya wanaweza labda kuweza ndo huku pia.

Lakini huyo secretary mstaafu na asiechukua hatua juu ya wanyama wetu walioporwa na mwenzie yaweza ripoti kuwa imewakalia pabaya na huenda iko inaandikwa upya sasa
 
hapa kuna mkubwa alisema licha ya fedha kuiisha bado wanaogopa repoti ya Jairo , maana anataka kumrithi luhaj=njo ndiye alipangwav saasa hari ni TETE na jamaa yangu akinambia hadi sasa hivi hwajaingiziwa fedha za kikao cha jana na leo licha ya kwqmaba kinaairisshwa na jana wajkati repot inakabidhiwa mjadala uliotawala hawa wabunge walipwe nini maan hakuna pesa sasa wanasubiri mkopo kutoka Benki ya DUNIA ndio maana mtu akinyanyuka tu ndani ya Bunge mwaziri wote wanakuwa ful attension
 
kwani bunge na mahakama kwa sasa vina kazi gani ha Tanzania? Mi naona kila kitu kinaamriwa na serikali na CCM tu.
 
Hii nchi ina mbaya wakuu..tatizo wasomi wamekaa kimya na matai yao shingoni..tulipaswa kwasasa tuwe tunmeingia mtaani muda mrefu sana chini ya wasomi wa vyuo vyetu...vinginevyo tutajuta muda si mrefu...
 
Lazima kuna pressing issue na itakuwa ni issue ya pesa. Nahisi ofisi ya bunge haina fungu la kuendesha kikao kwa wiki mbili hivyo bado wanavutana na serikali waingize nini kwenye ratiba na nini waache.

Maadam membe wetu humu jf mkuu Said Yakub aliyekuwa BBC London sasa ni ofisa habari wa Bunge letu, hopeful atatujuza kinachoendelea bila kuathiri ahadi za usiri kwa watumishi wa umma, hivyo tutajua nini kimejiri.

Naomba niwaandae kabisa kisaikolojia, msije kushangaa mkisikia kikao ni mpaka Ijumaa tuu!.

Sasa pesa zimeishaje wkt hata nusu mwaka hawajafika na bajeti wamepitisha juzi juzi kwa 100% kwa 100%?
 
Hili swala la kuwapeleka watu dodoma na kutofanya kazi waliyoitiwa, kikao kinaahirishwa saa tano asubuhi.....huu ni uzembe wa viongozi wa bunge.
Upuuzi kila mahali.
 
hiyo ndiyo 'alternative think tank' ya Watanzania, kweli tuna hali mbaya!
huyu Makinda kweli anaweza kuongoza mhimili huu?
kama kweli aliwekwa na mafisadi (maana hajajibu 'shambulio' la Samwel Sitta) angakuwa tu fair kama yule mbunge wa Zambia na kuachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine. Huu mwaka wake mmoja nchi inaonekana wazi haimhitaji na wala haonyeshi chochote cha maana!
 
Wataalamu walisema nchi iko kwenye auto pilot, hizi ni baadhi ya dalili ambazo chanzo chake ni urafiki, ujamaa, kulindana, mwenzetu, maslahi binafsi etc

Pia, watu makini wote walishaonya kuwa uendeshaji wa nchi kimazoea kama wa kwetu hapa ipo siku mambo yatakwama tu!
Naona somo linaingia kwenye sura halisi
 
Au wanahofia ripoti ya Kamati iliyoundwa kuhusu sakata la Jairo maana lazima kuna mtu atatakiwa kuwajibishwa.
 
Hili swala la kuwapeleka watu dodoma na kutofanya kazi waliyoitiwa, kikao kinaahirishwa saa tano asubuhi.....huu ni uzembe wa viongozi wa bunge.
Upuuzi kila mahali.

Mkuu wakihairisha kikao muda huo wanakaa wanazurula tu hapa mjini.....
 
Back
Top Bottom