Samatime Magari
Senior Member
- Feb 10, 2017
- 103
- 388
Hili jibu alipewa Bonilove wakati anataka kununua Mazda Atenza na Boni Bila hiyana akavuta mzigo na picha ndo likaanzia hapa,..
.
Boni ni mkazi wa makao makuu ya nchi wenyewe wanapaita Dodoma na ni mmoja wa wasirikali waliotoka Dar wakaenda Dom Kikazi, Ni kijana flani mtu wa maji, misosi na watoto so baada ya kuvuta machine, sector ya wabebez + maji ika speed up reaction hasa upande wa wabebez...
.
Weekend moja rafiki ake Boni mida ya saa 9 alasiri alimuita Boni aje Waswanu Pub maeneo ya Uzunguni kupiga maji Rafiki ake ni wale jamaa maji yakishaanza kukolea simu zinakua nyingi kwa wadau na Boni by the time anapigiwa simu alikua na mpenzi wake home wamechil tu..
.
.
So Boni akaona ni time nzuri ya kutoka na bibie out angalau bibie nae ale good time na wapige mdudu aka chair fire basi Boni na manzi wake wakajianda wakawasha machine then chap wakafika Waswanu..
.
Kufika pale wakakuta mshikaji pia yuko na mpenzi wake wanapiga kilaji so wakawa wanne., Boni na bibie nao wakaanza kupiga maji wakati wanasubiri mdudu..
.
Basi maji yakapigwa na mdudu akapigwa kufikia jioni flani maji yakaanza kuzidi unga Kama ilivyo ada maji yakizidi unga ugali unaanza kuwa uji taratibu, so maji yalivyokolea Boni akatoa wazo wahamie Bambalaga..
.
.
Bambalaga iko maeneo ya Kisasa na akadai ndo kuna vibe zaidi, Halafu ukiwa maji chuma imepark nje huwa kuna ka kihere here flani ka kuhama kiwanja. Utasikia hapa pamepoa sana twende sehemu flani ndo kuna shangwe la kutosha, Basi Jamaa wakaamua kuhamia Bambalaga..
.
Mshikaji wake Boni alikua na Subaru Impreza akaingia kwa gari akatia reverse akatoka parking akachomoka kama mshale, Manzi wa Boni kuona vile akasema huyu rafiki ako nae anapenda kukuoshea, Boni kusikia hivi + akili za maji nae akatoka kama mshale lengo ampite Jamaa ake..
.
.
Na alifanikiwa kumpita sema baada ya kumpita Jamaa ake nae akakanyaga ile anataka kuovertake Boni akampa Bodi Jamaa akala upande wa nyuma mlangoni kote kioo kikapasuka na mlango ukobondeka, Impreza bumper chali, condenser na radiator pia zimeguswa na taa upande wa kushoto..
.
Wakaweka gari pembeni kuangalia Mazda mlango na buti kulia na taa havifai, Kama ilivyo ada Boni maji yakaanza kupungua wakati unga unaongezeka akili zikaanza kurudi. Basi Trafiki police wakaja pale + kuita Brake down lao ila wakagundua jamaa wako maji ndio ila wameamua kumalizana wenyewe..
.
Hafu ni wasirikali wakaona hamna issue hapa Trafiki wakajikataa, Sasa impreza sababu ya radiator kuguswa ikavutwa na Mazda mpaka nyumbani. Safari ya Bambalaga ikaishia hapo, kesho yake Boni akapeleka gari kwa fundi ifanyiwe marekebisho.. . Hapa ndo picha halisi likaanza sasa..
.
.
Mind you gari haikua insured so taa zikatafutwa Dodoma hola. Zikapatikana Dar pale tena Tandale kwa tumbo kwa wakata magari Bei mkasi Kuhusu body fundi akasema anaweza rekebisha body ila mlango hawezi lazima uje mwingine apachike. Tafuta mlango Dodoma hola, wakahamia Dar..
.
Dar nae pia hola hamna kitu Boni akaona isiwe Kesi tuufate Japan, Japan ile kugusa tu ni kama Parachichi moshi mlango upo ni wewe tu na Pesa yako. Mlango Japan wakakuta bei ni $61, Shipping $100 so $161 = Tsh 376,740 mapaka unafika bandarini, Boni akalipa mlango ukaja..
.
.
Ulivyofika bandarini Tiarehei wakasema kodi ni Tsh 239,993. Hawajakaa sawa wakaona haitoshi wakaongeza additional ya Tsh 14,843 na Wharfage 8,756 Jumla 263,592, Wazee wa TBS nao hawakua nyuma wakasema lazima tuukague wakaleta invoice ya Tsh 30,000,
Bandari Kavu nao mzigo Ulipofikia na kutuzwa nao wakadai Tsh 129,385, Jumla ya gharama zote ikawa 799,717.. . Agent nae aliyefanya clearance akaja hapa akabil 150,000 Jumla ikawa 949,717, Mzigo ukatoka ukapelekwa Pale Shekilango ili utumwe Dodoma na pale wakadai 20,000 Jumla kuu ikawa 969,717..
.
.
Sasa huu ni mlango mmoja tu ingekua zaidi unaweza geuza gari banda la kuku, Ingekua kama IST na ndugu zake hapa mlango ungepatika ilala kwa 350,000 - 500,000, Au ukienda kwa wakata magari pale Tandale kwa tumbo unaweza pata hadi kwa Tsh 200,000-300,000 au chini zaidi..
.
.
Sasa lengo la kukupa hii story ni kukupa ufahamu ili wakati unataka gari uwe makini na chaguzi zako. Usije ingia mkenge ukaja ukapasuka mbele ya safari ndugu, Najua dunia ni kijiji ila always nasema kuagiza baadhi ya spear au body parts sio sawa na kununua hapa nchini..
.
Kuna vitu lazima uwe vizuri mfukoni tofauti na hapo utaumia, Kuna brands za gari kama uchumi wako bado ni wa kutumia ARV sio za kununua zitakutesa tu. Kama unahitaji ushauri karibu tutakupa ushauri mzuri tu ili ukusaidie kufanya maamuzi sahihi kutokana na kipato chako..
.
Kama unahitaji kuagiza gari Japan , kununua showroom au mkononi karibu, Tuko na network ya trusted dealers kwa Japan, UK, Singapore etc dealers wanaotupa gari zenye ubora wa juu kwa bei safi, Tutafanya mchakato wako wa kupata gari kuwa rahisi salama na unaojali muda wako..
.
.
Simply tupigie simu njoo WhatsApp au ofisini Posta Mpya Phoenix House mkabala na Mkapa tower tutaku assist Kama uko mkoani na unahitaji kuagiza gari karibu, utatupa hitaji lako tutakupa Ushauri then tutakutumia options za gari ukishachagua utapewa invoice..
.
.
Utafanya malipo at cost [no extra cost] huko huko ulipo mpaka gari itafika na utakuja kuichukua au kuletewa ulipo, Natumaini umejifunza kitu kama jibu ni ndio basi usisahau kushare kwa ajili ya wengine na Kama hujatu follow katika kurasa zetu za jamii tu follow chap ili next time usipitwe na madini..
.
Asante
Samatime
0714547598