Bonde la Mto Msimbazi Lafurika-Polisi wahaha Kuokoa Maisha ya Wavuja Jasho

This time isiwepo misaada yoyote zaidi ya kuwatafutia makazi mapya na baada ya hapo makazi yao ya bondeni yabomlewe na asiwepo awaye yeyote wa kurudi hapo. Tutakuwa tunawalea tukiendelea kuwasaidia wakiwa hapo hapo!
 
wameona matatizo ya watu waishio bondeni msimbazi na hatari ya kuzolewa na maji kama ilivyo kwa philiphins . Hivi sasa philipines wameisha kufa watu zaidi ya 762 lakini serikali yetu inanyondea kuwahamisha watu waishio mabondeni. Hii ni hatari sana ya kuwa na makada wengi serikalini. wao hapo wanaona ni heri kuweka matawi ya chama kwa sababu kuna wakazi wengi, kuliko kuwahamisha ili kuwaokoa maisha yao.
 
Nchi iuzwe kila mtu apewe chake mu-vacate. Inawezekana mkikubaliana kimsingi.
 
GreatThinkers,

Hali ni tete ktk Bonde la Msimbazi daraja la Segerea maji yanapitia Pomoni tokea Pugu na Kinyerezi,Njoo hadi vingunguti hali ni Mbaya sana. Kigogo Polisi wapo kule wanajaribu kuokoa wananchi?

2006/7 kulikuwa na Elnino hayo majumba yaliyopo bonde la msimbazi hayakuwepo mengi kama sasa muulize Mzee Makamba ex-Mkuu wa Mkoa wa Dar.
Tulipata fundisho gani uongozi wa mkoa/taifa ulijifunza, hii mvua iliyokesha inanyesha usiku wa kuamkia leo ni kama tano ktk mia ya Elnino tuliyoshuhudia mwaka ule
Ndg. wana Dar Es Salaam mnaoaminika kunywa maji ya Bendera mnadhani CCeM inathamini tena mtu mlalahoi?
Kama wana nia njema nanyi na hawataki kesho baadhi ya miili ikaokotwe baharini kwa nini wanawaruhusu kujenga?
Je mmewahi kwenda TANESCO kuomba kuunganishiwa huduma mkaambiwa kule ni bondeni hawaweki? Maji Je?
Je serikali inamchoro wowote uliosambazwa kwa wanamitaa jirani na bonde kuwaarifu waishie wapi kujenga makazi hayo yanayoitwa holela?
Mfano. Pale Matumbi ukitokea Buguruni kuna matajiri wameziba bonde kwa Kujaza vifusi na kujenga kuta kubwa na kuweka viwanda serikali iko wapi? au ndiyo Umbwe(vacuum) la Uongozi linalosemwa kwa lipo kwa sasa?
Yangu ni hayo ila maafa yapo.
Mwigamba mchochezi. na hii mvua nayo , mchochezi ni nani , Mungu?.hapa bado tuna mengi yatatupata hapa dar.
 
GreatThinkers,

Huu mji haufai naadhani nahitaji kurudi Kanda ya ziwa-Rocky city haraka iwezekanavyo.

Watu wengi usiku wa kuamkia leo wamelala ktk madaladala kwa kulipia Buku mbili.

Mvua inaendela asubuhi hii. Niko Bindeni Hotel hapa Magomeni mvua ikizidi naamini maji yatafika hata hapa.

Aiseee Dar hapafai
 
Back
Top Bottom