Something is behind these attacks. Not CDM not CCM
Nchi ipo katika hali tete ya kiusalama,
Nashauri kila mkusanyiko mikubwa hasa ya CDM screening ifanyike kwa kila anayeingia,
mmetengeneza matukio mengi sana ya uongo na kizandiki ikiwa ni pamoja na filamu za kigaidi ili tu CDM waonekane wabaya kwa wananchi, mli-achieve nini?!!. Hakika Magamba mwisho wenu umekaribia na kadri mnavyozidi kufanya huu ujinga wenu ndivyo chuki dhidi yenu inavyozidi kuongezeka!ccm hawawezi kutega hayo mabomu ,ili waachive nini?tena siku ya mwisho wa kampeni...mbona unakua na haraka kulaumu kabla,au unahusika mkuu?
Kwa hiyo ulitaka nani afanye uchunguzi?
Ukase ukijua hao wanaopanga haya mauaji iko siku mmoja wao ataimba tu. Subiri wanyimwe malipo au wazungushwe utasikia tu.
Mwisho wa mpangaji wa haya mauaji utafika tu siku moja
Kwa nini bomu lilipuke baada ya mkutano na siyo kabla au wakati wa mkutano?.
Kwa nini bomu lisubiri mpaka viongozi wa CHADEMA wamalize kuwapa wananchi ujumbe wa uchaguzi na jinsi ya kupiga kura ndiyo bomu lilipuke?. WHY?.
Nini kilichoko nyuma ya hii SIRI ya kisiasa?.
Kuna maswali ambayo ukiangalia kifikra unapata jibu pamoja na kwamba uchunguzi ni muhimu sana.
Unauliza polisi walikuwa wapi wakati wao ndio waliopanga.Sasa tunakokwenda ndiko siko! Polisi walikuwa wapi?
Hivi una uhakika gani kama bomu lilirushwa kwa mkono wakati wengine wanadai lilikuwa limepandikizwa, lakini pia kwa kutumia akili tu ya kawaida, kama watu walijaa na akasogea mpaka karibu na jukwaa kuu, ataweza kufanikiwa kukimbia tena baada ya kurusha wakati kuna watu wengi na baina yao watakuwa wanamuona wakati akirusha.Kama ni mhudhuriaji wa mikutano ya chadema utajua kwanini huyo mtu alirusha bomu wakati wa kuchangisha/kutoa sadaka kwani kipindi ndo kunakuwa na watu kutembeatembea hivyo inakuwa rahisi kwake kusogea karibu na pia kuwa rahisi kwake kukimbia baada ya kufanya uharifu.
Wakuu hivi ni vitu vilivyoaandaliwa kunamtu mwingine kaposti huu eti kwenye mkutano wa chadema mbeya nao umerushiwa bomu wakuu haya mambo wanapanga na kutekeleza wao wenyewe chadema sijui wanataka jamii tuelewe nini.
na ndo ilivyo mkuu,nye hamuaminiki kwa loloteNayajua haya
Siku zote ukiongea habari wanayotaka makamanda kuisikia utaonekana genius na mkweli
Ndugu yangu najua unalipwa, ila huu upuuzi unaouongelea hapa mungu atakuadhibu huko kaburini. Jifariji kwa njaa zako ila siku yakimpata ndugu yako hizo huku saba hazitakisaidia.
Uchunguzi upi mkuu wakati bomu la Olasiti Polisi walishampa Cardinal majibu kabla ya uchunguzi,wakakamatwa watu ambao sio,kwa jeshi hili hili la matukio ya Dr.Ulimboka,Kibanda,Mwangosi na matukio ya kidini tusitegemee jipya kabisa,najiuliza sisi watanzania viongozi wetu wanatuonaje mpaka kila kinachotekea ni mwendo wa kauli tu,kulaani sijui tuko pamoja,ikipita siku kila kitu kinafutwa tunaanza moja,toka arudi Kibanda hakuna tamko toka serekalini,hivi mpaka lini hawa watu watacheza na maisha yetu ili hali na wao ni binadamu kama sisi?Mimi naona uchunguzi unatakiwa, na kukurupuka kwamba CCM ndio waliotega bomu, au CHADEMA ndio waliotega bomu, kabla ya uchunguzi hakufai.