Inafika mwisho kwenye ku download then inaleta ujumbe '' error installing application"
Nadhani hiyo inaweza kuwa sababu, hizi simu zinakubali simcard za airtel tu, sasa mtandao wa airtel naona hauko stable sana kwa hii simu, unakatakata sana, asanteni sana naendelea kujaribu.
@vodashops mlimani city (tshs 2.2m) zipo wanauza, they must be supprting them hawawezi uza kitu ya bei mbya hivyo bila support yake
Mkuu unaposema kila link inanikatalia akili yangu inaniambia kua unadownload version zisizosuport watsap. Version nyingi ambazo zimetapakaa ni za android na symbian
Pili hiyo bb yako ni original? Maana hazijasambaa sana hizo simu
Je ukieka app tofauti na watsap zinakubali?
Kama kweli una hio simu click link hii itadownload
BlackBerry World - WhatsApp Messenger
Then tumia site hii kama una bb inasaidia sana inaitwa crackberry maelezo zaidi ya watsap na screenshot kwa simu yako ingia hapa
WhatsApp for BlackBerry 10 now available! | CrackBerry.com
Ok, mwezi wa nne nilienda hapo na tigo pia, hawakuwa nazo na walikiri haziko supported na simcard zao, kama sasa wameleta ntapita, asante sana Mkuu.
Hiyi ni simu ya kawaida tu, inafanya kazi mitandao yote. Hakuna haja ya kuwa supported.
Mimi ni mteja sana wa hizi BB kwa uzoefu wangu toleo la mwanzo(yaani new model) la bb huwa zinakuaga zinazingua kiaina on performance etc hua nasubiri toleo la pili ndo linakuaga la ukweli
Ok, nimeingia kwenye BB world na kwenye hiyo link pia, bado inaleta the same error! Na bado nadhani ni original, sababu nililetewa na mtu ambaye aliinunua siku mbili baada ya kutolewa, tatizo ninalolipata bado nadhani ni network! Inakata sana na pia sometimes inaandika insert simcard! Nadhani hili toleo halijakaa vizuri kwetu, ntajaribu line ya voda kama sasa hivi ziko supported na wao, thanks.
Kiongozi watsapps kwa z10 mpaka uapdate latest os, sasa issue ni kwamba Z10 zipo model 4 hardware tofauti. Nenda kwenye settings then about angalia stl model kisha download os
mkuu kumbe tupo wengi nilinunua hii simu sio siri kuna baadhi ya apps kama hiyo whatsup nimeshindwa kudownload nimeichukia sana hii simu sijui kwanini imenibidi nirudi apple hii naiuza hata laki tisa nampa nimeitumia mwezi tu, ni kosa langu kila simu ikitoka nakurupuka kununua ni makosa makubwa sana tatizo nina impulse spending huu ugonjwa unanisumbua sana