Babu Lao
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 2,043
- 179
WAKATI Serikali ikikuna kichwa kukabiliana na wimbi la mimba kwa wanafunzi, binti mwenye umri wa miaka 11 mkazi wa Ngarananyuki mkoani Kilimanjaro, Nangakwa Lowasa, amejifungua mtoto mwenzie salama nyumbani kwake kwa usaidizi wa wakunga wa jadi.
Binti huyo kutoka jamii ya Kimasai iliyoko wilayani Siha mkoani hapa, amewashangaza wengi baada ya kujifungua bila kupata tatizo lolote, na kwa sasa anaishi na mume wake aliyejulikana kwa jina moja la Narida, anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30 hadi 35.
Gazeti hili wiki hii lilizungumza na binti huyo katika wodi ya wazazi ya Hospitali ya Wilaya ya Hai iliyoko Machame alikolazwa baada ya kuugua malaria mara baada ya kujifungua ambapo licha ya kutokwenda shule kabisa katika maisha yake, pia hajui hata lugha ya Kiswahili.
Kutokana na mazingira aliyokulia, Nangakwa aliyekuwa akizungumza kwa msaada wa mfasiri, haoni tatizo lolote kwa yeye kujifungua mtoto na hata kuwa na mume.
Binti huyo alisema aliolewa mwaka jana na kwa sasa anaishi na mume wake Narida, na kwamba wakati wa kujifungua, ingawa ilikuwa nyumbani na kwa njia za kienyeji, hakupata tatizo lolote.
:A S 13: Hii bado ipo bongo?
Binti huyo kutoka jamii ya Kimasai iliyoko wilayani Siha mkoani hapa, amewashangaza wengi baada ya kujifungua bila kupata tatizo lolote, na kwa sasa anaishi na mume wake aliyejulikana kwa jina moja la Narida, anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30 hadi 35.
Gazeti hili wiki hii lilizungumza na binti huyo katika wodi ya wazazi ya Hospitali ya Wilaya ya Hai iliyoko Machame alikolazwa baada ya kuugua malaria mara baada ya kujifungua ambapo licha ya kutokwenda shule kabisa katika maisha yake, pia hajui hata lugha ya Kiswahili.
Kutokana na mazingira aliyokulia, Nangakwa aliyekuwa akizungumza kwa msaada wa mfasiri, haoni tatizo lolote kwa yeye kujifungua mtoto na hata kuwa na mume.
Binti huyo alisema aliolewa mwaka jana na kwa sasa anaishi na mume wake Narida, na kwamba wakati wa kujifungua, ingawa ilikuwa nyumbani na kwa njia za kienyeji, hakupata tatizo lolote.
:A S 13: Hii bado ipo bongo?