Patrick Nyemela
JF-Expert Member
- Nov 25, 2008
- 332
- 26
MTOTO wa aliyekuwa Waziri wa Kilimo Bw. Charles Keenja, Bi. Aghata Keenja ameburutwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala akikabiliwa na makosa ya kukutwa na dawa za kulenvya kinyume cha sheria.
Mshitakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu wa Wilaya Bi. Janeth Kinyage.
Bi. Keenja anatuhumiwa kwa makosa ya kupatikana na dawa za kulevya kinyume cha kifungu 12(d) cha sheria ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya.
Alidaiwa kuwa Oktoba mosi, mwaka huu katika mtaa wa Makunganya, Dar es Salaam alikamatwa na gramu 6.6 za dawa ya kulevya aina ya Heroini yenye thamani ya sh. 60,000. Hata hivyo mshitakiwa huyo alikana kutenda makosa hayo na upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Mshitakiwa huyo aliiomba mahakama kumpatia dhamana ambapo ilimtaka kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika ambao watasaini dhamana ya sh. 500,000. Alitimiza masharti ya dhamana na kesi yake itatajwa tena Novemba 2 mwaka huu.
Mshitakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu wa Wilaya Bi. Janeth Kinyage.
Bi. Keenja anatuhumiwa kwa makosa ya kupatikana na dawa za kulevya kinyume cha kifungu 12(d) cha sheria ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya.
Alidaiwa kuwa Oktoba mosi, mwaka huu katika mtaa wa Makunganya, Dar es Salaam alikamatwa na gramu 6.6 za dawa ya kulevya aina ya Heroini yenye thamani ya sh. 60,000. Hata hivyo mshitakiwa huyo alikana kutenda makosa hayo na upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Mshitakiwa huyo aliiomba mahakama kumpatia dhamana ambapo ilimtaka kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika ambao watasaini dhamana ya sh. 500,000. Alitimiza masharti ya dhamana na kesi yake itatajwa tena Novemba 2 mwaka huu.