ELIMU PESA
Member
- Jul 22, 2017
- 62
- 36
Habari ndugu zangu.
Ninaomba msaada, binti huyu ninaambatanisha picha zake amepotea tangu tarehe 27/08/2023.
Binti huyu anaitwa Antia Focas, nyumbani walizoea kumuita Nyakato. Ana umri wa miaka 19. Mkazi wa Mkundi Morogoro, japo ana miezi mitatu tu tangu ahamie mkundi, mwanzoni tulikuwa tukiishi Kihonda-Maghorofani. Mimi ni baba yake mdogo, nimekuwa nikiishi naye kwa muda wa miaka mitatu sasa tangu nimtoe kwa wazazi wake.
Niligundua kuwa amepotea tarehe 27/08/2023 muda wa saa 7:30 (saba na nusu) mchana, hii ni kwa sababu alikuwa akimpeleka mtoto shule alafu anapitia kujifunza cherehani, ikifika saa sita na nusu anakwenda shule kumfata mtoto, wanarudi nyumba muda wa saa 7:30. Siku hiyo ilifika muda huo hajarudi, ilipofika saa nane na nusu tukapiga simu shuleni na kugundua kuwa hata mtoto alikuwa hajachukuliwa pale shuleni, shule inaitwa WESLEY.
Tulipopiga simu kwa mtu aliyekuwa akimfundisha cherehani, alisema kuwa alifika tu asubuhi, akaaga kuwa anakwenda saloon, kuosha nywele na kusuka. Tulipofatilia saloon, tukaambiwa kuwa hakufika. Tulitoa taarifa katika kitua cha polisi cha Kihonda, tukaambiwa turudi baada ya masaa 48 kama hajapatikana, tuliporudi tukapewa RB namba na kuambiwa tuendelee kumtafuta.
Bahati mbaya hadi leo hatujampta, alikuwa na simu lakini tangu apotee haipatikani. Pengine ni rahisi kufikiri kuwa labda katoroshwa na mwanaume, lakini mazingira aliyoondoka yatia shaka, kwani hakubeba kitu chochote. Hakubeba hata nguo moja wala mkoba. Naomba msaada wenu kwa atakayemuona.
Simu 0766729127/0688746145.
Asanteni.
Ninaomba msaada, binti huyu ninaambatanisha picha zake amepotea tangu tarehe 27/08/2023.
Binti huyu anaitwa Antia Focas, nyumbani walizoea kumuita Nyakato. Ana umri wa miaka 19. Mkazi wa Mkundi Morogoro, japo ana miezi mitatu tu tangu ahamie mkundi, mwanzoni tulikuwa tukiishi Kihonda-Maghorofani. Mimi ni baba yake mdogo, nimekuwa nikiishi naye kwa muda wa miaka mitatu sasa tangu nimtoe kwa wazazi wake.
Niligundua kuwa amepotea tarehe 27/08/2023 muda wa saa 7:30 (saba na nusu) mchana, hii ni kwa sababu alikuwa akimpeleka mtoto shule alafu anapitia kujifunza cherehani, ikifika saa sita na nusu anakwenda shule kumfata mtoto, wanarudi nyumba muda wa saa 7:30. Siku hiyo ilifika muda huo hajarudi, ilipofika saa nane na nusu tukapiga simu shuleni na kugundua kuwa hata mtoto alikuwa hajachukuliwa pale shuleni, shule inaitwa WESLEY.
Tulipopiga simu kwa mtu aliyekuwa akimfundisha cherehani, alisema kuwa alifika tu asubuhi, akaaga kuwa anakwenda saloon, kuosha nywele na kusuka. Tulipofatilia saloon, tukaambiwa kuwa hakufika. Tulitoa taarifa katika kitua cha polisi cha Kihonda, tukaambiwa turudi baada ya masaa 48 kama hajapatikana, tuliporudi tukapewa RB namba na kuambiwa tuendelee kumtafuta.
Bahati mbaya hadi leo hatujampta, alikuwa na simu lakini tangu apotee haipatikani. Pengine ni rahisi kufikiri kuwa labda katoroshwa na mwanaume, lakini mazingira aliyoondoka yatia shaka, kwani hakubeba kitu chochote. Hakubeba hata nguo moja wala mkoba. Naomba msaada wenu kwa atakayemuona.
Simu 0766729127/0688746145.
Asanteni.