Binti asimulia watanzania wanavyotumikishwa kwenye madanguro China

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,896
macau.jpg

Picha: Askari wa Jimbo la Macau wakiwadhibiti machangudoa waliokamatwa katika oparesheni maalumu.


Wakati wanawake kwa wanaume wengi huenda barani Asia, hasa China kununua bidhaa kwa ajili ya kuja kuzichuuza, hali sasa ni tofauti kwa kuwa kuna wasichana ambao huenda huko kwa ahadi za ajira, lakini huishia kufanya ukahaba kwenye madanguro, gazeti hili linaweza kukuthibitishia.

Wasichana hao hutafutwa na mawakala wa hapa nchini ambao kazi yao huwa ni kutafuta wasichana wazuri na baadaye kuwashawishi kwa kuwaeleza fursa za ajira za hotelini zilizo barani Asia. Msichana akikubali, wakala huchukua jukumu la kumtafutia viza ya kuingia China na baadaye kuwasiliana na mwenyeji wake, maarufu kama Lady Boss, ambaye hutuma tiketi ya ndege kwa ajili ya kumsafirisha ‘mwajiriwa' mpya.

Hata hivyo, hali hubadilika mara wafikapo huko kwa kuwa ‘mwajiri' huyo humpokonya hati ya kusafiria na baadaye kumpa maelekezo kuwa atatakiwa kulipa Dola 200 kila siku ambazo atakuwa akizipata kwa kufanya umalaya kwenye klabu na maeneo ya biashara.


Tayari wasichana kadhaa wa Kitanzania wamenaswa katika mtego huo na kujikuta wakilazimika kuuza miili yao ili wamudu ada ya Dola 200 pamoja na fedha za kujikimu, akiwemo Munira Mathias mwenye umri wa miaka 23 ambaye alimudu kuvaa ujasiri wa kuweka bayana uovu huo katika mazungumzo yake na gazeti hili.

Binti huyo Mtanzania aliyesafiri kwa saa 18 kwenda Guangzou, China alitakiwa kupumzika kwa saa mbili tu kabla ya kupelekwa kuanza ‘kazi' ambayo hakuitarajia. "Baada ya kupumzika kwa saa mbili tu, nilipelekwa kwenye klabu," anasema Munira wakati akisimulia mkasa wake. "Sikuwa na kazi nyingine zaidi ya kucheza muziki na wanaume ambao licha ya kwamba sikuwahi kuwaona, walinichangamkia kama vile wananifahamu."


Munira aliondoka Januari mwaka huu kwenda China ambako aliahidiwa kuwa angeajiriwa hotelini, lakini alikutana na ‘ajira' ya ukahaba, huku akilazimika kuwalipa ‘waajiri' wake Dola za Marekani 200 kila siku. Binti huyo, ambaye alifanikiwa kuchomoka mikononi mwa waajiri hao baada ya viza yake kuisha, alisema kwa siku 91 alizokaa China, alipata mateso ambayo hatayasahau ikiwamo kupigwa, kubakwa na kundi la wanaume raia wa Nigeria, pia kulazimika kutoa mimba aliyoipata kwa kubakwa.

"Nilifika Guangzhou kama saa 9.00 alasiri za China na kulikuwa na baridi sana," anasema Munira akisimulia jinsi alivyokanyaga kwa mara ya kwanza ardhi ya nchi hiyo akiwa na matumaini ya kuanza maisha mapya. "Wakati huo nilikuwa nikijaribu kupata mawasiliano na mwenyeji wangu ambaye niliagizwa kutoka Magomeni, Dar es Salaam.

Alisema alipotoka Dar es Salaam aliambiwa angepokewa na mtu anayeitwa Jacky ambaye hakumkuta kwa kuwa alikuwa safarini Malaysia, lakini alikuwa ameacha maagizo apokewe na mwanamke mwingine. "Nilielekezwa nikodi taksi hadi kwenye hoteli inayoitwa Nairobian. Kutoka hapo uwanja wa ndege hadi kwenye hiyo hoteli ni sawa na umbali wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam hadi Bagamoyo," anasema Munira.

Anasema alitakiwa kulipa Yuan 200 (Sh60,000) na alipofika katika hoteli hiyo alipokewa, akaoga na kupewa chakula. "Nilipomaliza kula nilipumzika kwa saa mbili hivi. Jacky alikuwa amesharudi na alinifuata chumbani na kuniambia natakiwa kwenda saluni. Hivyo tuliondoka pamoja hadi kwenye jengo kubwa lenye maduka makubwa linaloitwa Tin- shu," anasimulia Munira.

Watanzania lukuki
Katika jengo hilo alishangaa kuwaona Watanzania wengi, wakiwamo wanawake kadhaa ambao aliwahi kukutana nao Magomeni wakati akifuatilia safari yake. Munira anasema miongoni mwa watu aliowaona ni binti mmoja ambaye wanafahamiana ambaye alistaajabu kumwona sehemu hiyo. "Aliniuliza kwa mshangao, ‘mbona umekuja huku? Umekuja kufanya nini?' Wakaanza kunishangaa. Yule msichana akaniambia ‘huku msala ndugu yangu, umekuja kufanya nini?" alimnukuu na kuongeza kuwa kabla hawajamaliza mazungumzo yao, mwenyeji wake alitokea hivyo waliyakatisha.


Anasema waliingia saluni ambako aliwakuta Watanzania na Wakenya wakifanya kazi humo na wakati yeye akiendelea kusukwa nywele kwa umaridadi, Jacky alikwenda kumnunulia nguo na viatu dukani. "Baada ya hapo niliambiwa nivae nguo niende klabu kwa sababu huo ni msimu wa sikukuu za mwaka mpya wa Kichina," alisema Munira.

Anasema alishangaa kuambiwa aende klabu usiku huo wakati alikuwa amechoka kwa safari ndefu. "Kilichokuwa kinanipa moyo usiku ule ni kuwa niliwaona wasichana wa Magomeni, lakini nilihisi wameambiwa wasiwe karibu na mimi." Anasema alipoingia klabu, pia alishangaa zaidi kukutana na Watanzania wengi wa rika tofauti ambao baadhi yao aliwatambua kwa sura na pia kulikuwa na raia wengi wa Nigeria.

"Kiasi fulani nilifarijika kuwaona Watanzania na nilijisikia kukua kiakili baada ya kuwaona Wanigeria ambao nilizoea kuwaona kwenye filamu peke yake," anasema. Hata hivyo, alishangaa kuona pale klabu alichangamkiwa na watu wengi, lakini hakutaka kudadisi zaidi bali alidhani ndiyo hali halisi au alikuwa na bahati ya kupendwa. "Baada ya kumaliza kucheza muziki kwenye klabu hiyo, walipelekwa kwenye klabu nyingine ya asubuhi.

"Tuliporudi hotelini, nilijitupa kitandani na kulala kwa sababu ya uchovu mwingi. Miguu ilikuwa imevimba kwa sababu nilikuwa nimevalishwa viatu virefu na kucheza muziki mfululizo. Nikalala bila ya hata kuoga," anasema.

Mwanzo wa mateso
Baada ya saa moja kupita na akiwa amelala fofofo mchana ule, mara aliamshwa na Jacky, ambaye alimwamuru amkabidhi pasipoti yake. "Nikampa, pasipoti yangu nilikuwa nimeiambatanisha na tiketi na kila kitu. Akanishangaza kuniambia kuwa kuanzia siku hiyo niwe nampelekea Dola 200 mezani kila siku. Nilishangaa na nikaanza kulia," anasema.


Kwa hasira na mshtuko alioupata, Munira anasema alitoka nje na kuanza kulia na wenzake walipomuuliza kinachomliza, aliwaeleza. Waliamua kumwambia ukweli kwamba hata wao walipelekwa kwa miadi ya kupata ajira za hoteli, lakini hawafanyi hivyo. "Waliniambia kuwa nao walirubuniwa na wakanyang'anywa hati za kusafiria kama mimi na wakaishia kuambiwa wafanye biashara ya kuuza miili ili watafute fedha," anasema Munira.

Munira anasema alichanganyikiwa, hasa pale alipoambiwa na wenzake kwamba kazi kubwa ni kwenda klabu kujiuza au kuzurura eneo la Chambu Chambu. Chambu Chambu ni soko la bidhaa ambako wasichana hujifanya wananunua vitu, lakini kimsingi huwa wanakwenda kutafuta wateja wa ngono. "Kule wanaume wameshajijengea picha kuwa wanawake wa Kitanzania wapo kwa ajili ya kujiuza, basi wakikuona tu wanakufuata na mnaongea biashara, mnakwenda kumalizana," anasimulia.

Wasichana wenzake wa Kitanzania walimwambia kuwa hayo ndiyo maisha yenyewe, hivyo aliporejea ndani, mwenyeji wake (Jacky) alimwambia ajiandae kuanza kazi mara moja na Munira akawa hana budi kufuata maelekezo.

Baada ya hapo aliingia bafuni akaoga, kisha akaenda eneo la Chambu Chambu kutafuta wateja. "Nikakubaliana na hali halisi nikawa nafanya kazi kama nilivyoambiwa. Niliona nikubali lakini akili kichwani mwangu ilikuwa nifanye mbinu ili nirudi nyumbani," anasema

:peep: :peep: :peep:
Minira abakwa na Wanaijeria
Munira baada ya kuamrishwa na ‘bosi' wake kufanya kazi hiyo, alielekezwa na wenzake kwenda eneo la soko liitwalo Chambu Chambu ambako wanawake Watanzania wanafahamika kuwa maarufu kwa biashara ya ukahaba. Binti huyo mwenye umri wa miaka 23 anasema usiku wa kwanza alipokwenda sokoni Chambu Chambu, wenzake walimkimbia, hivyo alichanganyikiwa na kuanza kuwapigia simu wenyeji wake kwani hakujua la kufanya. "Nilimpigia simu Jacky na yeye alinijibu, ‘acha ujinga, tafuta hela uniletee mimi." Anasema katika mazingira hayo alianza kulia na wakati akilia, alikutana na mwanaume wa Kinigeria, ambaye alimhoji maswali kadhaa.

Mnigeria yule alisema anaifahamu hoteli anayoishi Munira, lakini alimtaka wazungumze kwanza biashara kisha ampeleke na Munira alikubali. "Nilizungumza naye biashara na tukakubaliana twende kwenye hoteli niliyofikia, baada ya kufanya mapenzi akanilipa Dola 100, baadaye nilidakwa na mwenyeji wangu akinitaka nimpe fedha zote nilizopata," anasema. Alipomkabidhi fedha hizo, aliamrishwa kurudi tena sokoni kutafuta kiasi kingine cha fedha hadi atimize dola 200. Wakati huo bado ulikuwa ni mchana. "Baada ya kumalizana na Mnigeria yule, nilienda kulala, lakini sikulala sana kabla mwenyeji wangu hajaniamsha na kuniambia lazima nitimize Dola 100 iliyobaki, hivyo nikanyanyuka na kwenda tena sokoni," anasema.

Munira akawa hali wala halali vizuri akifanya kazi ya kujiuza mwili wake, kazi ambayo hata kiasi kidogo alichopata alitakiwa kugawana na mwenyeji wake kwa kumpatia Dola 200 kwa siku. "Nilikuwa nachoka, hasa kwa kudaiwa, wakati mwingine nikiwa kwenye siku zangu najiuliza nitafanyaje ili nipate fedha za kulipa deni? Niliondoka hapa nikiwa na afya, lakini nilipofika huko baada ya muda mfupi niliisha, yaani niliisha," anasema.

Ukatili wa aina yake
Anasimulia kwamba, siku moja saa 10.00 usiku akiwa klabu, alijisikia vibaya akatoka nje, akiwa huko alikutana na mwanamume ambaye walikubaliana wakastarehe kwa ujira fulani. Munira alikubali, lakini alijua kabisa kuwa anakwenda sehemu ambayo haifahamu kabisa. Baadaye aligundua kuwa eneo hilo linaitwa Nan-hai na linaongoza kwa matukio mengi ya uhalifu. Anasema walikubaliana na mwanamume huyo wa Kinigeria na alikaribishwa na kuingia ndani katika nyumba yenye vyumba vinne, alipomuuliza iwapo anaishi peke yake, mwanamume huyo alimhakikishia kuwa anaishi peke yake. "Nikamwambia nataka kiasi fulani, tukakubaliana niende Nan-hai, sehemu yenye matukio ya ajabu. Ni nyumba nzuri kwa kweli, nikaingia ndani, nikaoga," anasema.

Baadaye Munira aligundua kuwa yule mwanamume anaishi na wenzake, wakati wanafanya tendo la ngono, alishangaa mwanamume mwingine anaingia chumbani na wote mmoja baada ya mwingine walimwingilia. "Kwa kuwa nilikuwa nakataa kufanya walichotaka, walinipiga sana na ikabidi nikubali, hawakuniachia waliendelea kunibaka hadi kesho yake Saa 1.00 jioni, niliumia sana," anasema. Walimnyang'anya fedha alizokuwa nazo na walipomuachia, mmoja kati ya wanaume wale alimpa Munira Yuan 100 na kumwambia hiyo ni nauli yake. "Sikuelewa alikuwa na huruma au dharau?" anasema Munira.

Munira anasema kuwa alichukua gari na kumpigia simu rafiki yake, ambaye alimpokea na walipoingia ndani alimsimulia kisanga kilichomkuta na kwa pamoja wakaanza kulia. "Rafiki yangu alinipeleka hospitali ambako nilipigwa ultra- sound na x-ray, ikaonyesha jinsi nilivyoharibiwa kwa kiasi kikubwa." "Nikachomwa sindano za mishipa na kutundikiwa dripu, nilichomwa pia sindano za kuzuia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi," anasema.

Akiwa hospitalini hapo, Munira alikutana na mwanamume mmoja Mnigeria ambaye walizoeana kwa muda aliokuwa hapo Guangzhou. Mwanamume huyo alipenda kumwambia Munira kuwa anafanana na mke wake. Hata hivyo, Munira hawakumwambia Mnigeria huyo nini anachoumwa na badala yake walimdanganya kuwa anaumwa malaria. "Alikubali akanisaidia kulipa bili ya hospitali, akaninunulia chakula na kunipa fedha nyingine ya ziada," anasema.

Kutokana na mateso hayo, aliamua kumpigia simu Josephine wa Magomeni (aliyemfanyia mipango ya kwenda huko) kumwuliza kuhusu kazi yake, lakini Josephine alimtia moyo kuwa eti hoteli nyingi zimefungwa hadi msimu ujao. "Kumbe kile nilichoambiwa na wenzangu kwamba kazi ni ukahaba, kikawa ndiyo hicho, niliamua kumwachia Mungu," anasema.

Atuma picha
Akiwa hospitali, Munira alijipiga picha akiwa na majeraha aliyokuwa nayo na kuitumaWhatsApp kwa baadhi ya watu ambao katika kutumiana ujumbe huo, hatimaye taarifa zilimfikia mwenyeji wake, Jacky. "Aliponipigia simu hakuchukua hatua nyingine zaidi ya kuniuliza nipo wapi. Nikamwambia nipo hospitali, basi akakata simu na wala hakutaka kujua zaidi kilichonisibu," anasema.

Aliporudi hotelini, Jacky alimwambia hataki kusikia suala lolote na wala hajali kama alikuwa anaumwa zaidi ya kutaka Dola 200 kila siku iendayo kwa Mungu. Mwanadada huyo anasema kutokana na mateso hayo, alikonda kiasi kwamba, ulipofika wakati wa kuongeza muda wake wa viza, (alikuwa ana viza ya mwezi mmoja), sura yake ilibadilika na ilitofautiana na picha iliyokwekwa kwenye viza. Kwa bahati nzuri aliongezewa muda wa kuishi China kwa siku 14 zaidi ili ajitayarishe kutafuta kibali cha kuishi.

"Nilishangaa kusikia kwamba natakiwa niweke hela ya viza, kiasi cha Dola 300 na kiasi kingine Dola 200 za kumlipa mwenyeji wangu, wakati aliahidiwa kuwa atalipiwa kila kitu ikiwamo visa na malazi," anasema. Wakati huohuo, alitakiwa kulipia hoteli, ajinunulie chakula, atafute fedha ya viza, zile Dola 200 za kumpa mwenyeji wake nazo zikabaki pale pale.

Viza inakwisha
Wakati hayo yanaendelea muda ulikuwa unapita na wiki mbili za nyongeza ya viza yake zilikuwa zinayoyoma. Anasema ilikuwa ni bahati nzuri kwake kwani mteja wake mwingine pia mwenye asili ya Nigeria alimsaidia na kumpa fedha za kuongeza muda wa kuishi hapo Guangzhou. Hata hivyo, alipokwenda kuongeza muda wa viza yake, alikutana na changamoto mpya pale maofisa uhamiaji, walipomwambia kwamba hawezi kupata kwani sura yake halisi ilikuwa inatofautiana kwa kiasi kikubwa na picha iliyopo kwenye viza, hivyo walimnyima kibali. Wakati huo, muda wa viza yake ilikwisha kabisa na sasa alikuwa akiishi katika nchi hiyo kinyume cha sheria.



Mabinti+China+Pt3+Clip.jpg
Watanzania Madanguroni China (Pt. 3): Munira alivyojikuta na ujauzito usiokuwa na baba

Jana katika tovuti hii, binti huyo ambaye tulimpa jina bandia la Munira Mathias kutokana na sababu za kitaaluma, alieleza kwamba baada ya mateso mengi, viza yake ya kuishi China iliisha muda wake na alikuwa akiendela kuwapo katika mji wa Guangzhou kinyume cha sheria.

Wakati anasumbuka na masuala ya viza, alihisi kuwa na hali isiyokuwa ya kawaida, aliamua kununua kipimo cha ujauzito cha bei nafuu. Kwa bahati mbaya aligundua kuwa alikuwa mjamzito ambao anahisi kuupata siku alipobakwa na Wanigeria wanne.

Munira anasema suala la yeye kushika ujauzito lilileta shida zaidi, kwani mwenyeji wake, Jacky alimweka kikao na kumsuta kwa hilo bila kujali kuwa alibakwa. Mmoja wa wanawake hao ambao walikuwa wakifahamika kama ‘Boss Lady' alimshauri kuwa atamtafutia mwanaume ambaye atamsaidia kutafuta daktari ili watoe mimba hiyo.

Alipofika kwa daktari, alipewa vidonge tisa ambavyo alitakiwa kulipia Yuan za China 600 (zaidi ya Sh100,000). Hakuwa na fedha hivyo alitakiwa kuendelea kujiuza licha ya kuwa hakuwa amepona ili apate fedha hizo. "Baada ya muda nilipata fedha hizo na nilipewa vidonge, ambavyo hata hivyo haviharibu mimba kwa wakati huohuo bali taratibu sana," anasema Munira.

Muda wa kuishi Guangzhou ulikuwa umekwisha na Munira hakuwa amepata viza, ilimbidi aondoke. Lakini mwenyeji wake alimwambia ni lazima atafute fedha ya kulipia viza usiku uleule. Akimaanisha akajiuze usiku huo na kupata fedha kwa ajili hiyo. Munira alilazimika kuingia mitaani usiku ule kusaka wateja kwa ajili ya kupata fedha za kwenda kuchukua viza hiyo Macau, jimbo jingine maarufu nchini China.

Mwenyeji wake alimwambia wakati anaondoka asubuhi siku inayofuata, asiondoke bila kumuaga. Aliporejea usiku wa manane alijiandaa kwa ajili ya safari ya asubuhi yake, licha ya kwamba hakuwa amepata fedha za kutosha. Kulipopambazuka alikwenda kumuaga mwenyeji wake kama alivyoambiwa, lakini alishangazwa na kitendo cha mwenyeji huyo kumnyang'anya baadhi ya vitu kama nguo na viatu alivyomnunulia wakati alipofika nchini humo.

Wakati akiondoka alisindikizwa na Mtanzania, msamaria mwema, ambaye alimpa Dola 400 za Marekani kama akiba na nauli ya Yuan 50, hivyo kuongezea katika fedha alizokuwa amepata usiku ule.

Macau ni ‘Boda la JK'
Munira alichukua treni ya kuelekea Macau, mpakani lakini aliambiwa akiwa huko anatakiwa atoke kwa saa 12 kila baada ya miezi mitatu ili atakaporudi, aanze kuhesabiwa tena siku za kuishi.


Macau ni jimbo ambalo Watanzania wanapata msamaha wa kukaa kwa siku 90 bila viza, hivyo mara nyingi siku zinapokaribia kuisha, Watanzania katika jimbo hilo huondoka kwa saa 12, kisha kurejea kama wageni ambao huanza kuhesabiwa siku zao upya. Kutokana na urahisi huo wa kimaisha, Macau umebatizwa jina na Watanzania ambao wanauita ‘Boda la Kikwete', wakimaanisha kwamba maisha yao katika jimbo hilo ni kwa hisani ya makubaliano baina ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete na Serikali ya China.

Wakiwa Macau, Watanzania huenda kuchukua viza nchi jirani ya Malaysia, kinyume na hapo hubaki Macau, wakisubiri majaliwa ya kupata viza au kurudi nyumbani. "Nilipofika Macau nilipata shida, Wachina hawajui Kiingereza, nazunguka na begi langu, kumbuka bado sijapona baada ya kufanyiwa ule unyama," anasema.

Anasema alifanikiwa kuvuka mpaka wa Macau kutoka Guangzhou, ingawa alipata shida kupita katika viunzi vya uhamiaji kutokana na sheria za China. Akiwa hoi kwa kuchoka, alikutana na raia wa Somalia ambaye alimsaidia kujaza fomu, lakini hata hivyo hakuweza kumsubiri, hivyo Munira alibaki peke yake.

"Nilipofika katika kiunzi cha mwisho cha uhamiaji, nilihojiwa sana, maofisa uhamiaji walidai kuwa sura yangu ya sasa haifanani na iliyopo kwenye hati ya kusafiria, hivyo wakawa na wasiwasi na mimi," anasema. Munira anasema maofisa hao walimuuliza maswali mengi kama namba ya pasipoti, umri, majina matatu, mambo ambayo aliyajibu kwa ufasaha, lakini bado hawakuridhika na wakampeleka kwenye chumba maalumu cha polisi kwa mahojiano.

Huko, walimwambia afumue nywele alizokuwa amesukia na kumhoji kwa zaidi ya saa moja kabla ya kumruhusu.
Anasema ni kweli sura yake halisi ilikuwa imebadilika baada ya kukonda sana, kutokana na mateso aliyokuwa anayapata. "Mwisho wa siku waliniachia, nikachukue teksi, lakini ilinipoteza. Bahati nzuri mbele kabisa nikakutana na msichana raia wa Urusi, alichukua namba yangu na akanielekeza sehemu niliyotakiwa kwenda, huo ukawa mwanzo wa urafiki wetu," anasema.

Mjini Macau
Anasema alipofika eneo aliloelekezwa, katika hoteli kubwa iitwayo St Marol, aliwakuta wasichana wengi zaidi ya 200 wa Kitanzania ambao viza zao zilikuwa zimeisha muda.

Walikuwa ni wengi na wote walikuwa wanajiuza.
"Mji huo ni kama Zanzibar hivi. Ni pazuri na ni mji wa gharama sana kila kitu ni gharama, hata hivyo wateja hawakuwa wengi kama Guangzhou," anasema. Katika hoteli hiyo ya St Marol, wasichana 15 hadi 20 katika eneo hilo, huchangia gharama za chumba. Alishuhudia wasichana wadogo kuliko yeye, ambao walimlalamikia wakidai kuwa nao wanaishi maisha ya kujiuza ili wapate fedha kinachowakwamisha ni kukosa fedha za nauli ya kuwarudisha nchini.

Munira aliamua kuwasaidia, hivyo alishauriana na mmoja wao aitwaye Candy kwamba warekodi sauti kwenye simu wakieleza adha wanazopata, kisha wazitume Tanzania kupitia WhatsApp ili wapate msaada wa kurudi nyumbani.

Anasema ujumbe ule wa sauti ulisambaa karibu kwa Watanzania wote wanaoishi Macau, China, Guangzhou na Hong Kong na kwamba wezao wa Macau waligundua kwamba sauti hiyo ni ya mmoja wa wasichana wanaoishi kwenye hoteli hiyo ndipo walipoamua kwenda kuwasuta Munira na Candy chumbani kwako.

"Kundi la wasichana wa Kitanzania zaidi ya 100 walifika kwenye chumba chetu, wakaanza kutusuta kwa nini tuliamua kutuma ujumbe wa sauti kama ule." "Walitaka kunipiga wakidai kuwa nawaharibia maisha yao kwani wanapata pesa za kujenga nyumba na kununua magari kwa kazi hiyo," anasema.

Anasema yeye na Candy walipoona hali imekuwa mbaya, waliamua kukimbia. Munira kwa hofu, alibahatika kubeba hati ya kusafiria, tiketi na kadi ya manjano, akiacha nguo na baadhi ya mali zake. Hata hivyo, walipofika njiani, Candy alibadili uamuzi na kuamua kurudi hotelini. "Nilimshukuru Mungu kwa kunipa akili ya kuchukua vitu vitatu muhimu, nikampigia simu rafiki yangu Mrusi, ambaye alikuja kunisaidia na kunipeleka kuishi kwake.


 
Utumwa mamboleo unashika kasi

Munira Mathias, binti wa Kitanzania aliyekuwa akiishi China akitumikishwa kufanya ukahaba, alikimbilia Jimbo la Macau akitokea Guangzhou, baada ya muda wa viza yake kumalizika.

Kama tulivyoona katika gazeti hili jana, Macau nako hakukaa kwani alikimbilia kwa rafiki yake wa Kirusi, baada ya yeye na mwenzake, Candy kutishiwa na mabinti wenzao Watanzania kwa ‘kosa' la kurekodi ujumbe wa kuomba msaada kisha kuurusha kupitia mtandao wa WhatsApp.

Munira (ambaye si jina lake halisi) aliondoka katika chumba alichokuwa amepanga na kuacha kila alichokuwa nacho, isipokuwa hati ya kusafiria, tiketi ya ndege na kadi ya chanjo ya kuzuia ugonjwa wa manjano.

Itakumbukwa kwamba wakati akikimbia kutoka Guangzhou, tayari Munira alikuwa amemeza vidonge kwa ajili ya kutoa mimba ambayo hata hivyo hakuwa anafahamu baba wa mtoto anayemtarajia, kwani siku alipobakwa na vijana wanne hawakutumia kinga yoyote.

Alitakiwa kumeza vidonge tisa alivyopewa kwa ajili ya kutoa mimba, huku moja ya masharti yake yakiwa ni kutokukutana na mwanaume katika kipindi hicho. Hata hivyo hakuweza kutimiza masharti hayo kwa sababu alikuwa na shida ya pesa, hivyo alikuwa akimeza dawa huku akijiuza. Alikaa kwa rafiki yake wa Kirusi kwa siku nne na wakati huo vidonge alivyokunywa vilikuwa vimeanza kumzidi nguvu, hivyo alikuwa akilegea.

"Nadhani nilikosea masharti, ile mimba haikutoka bali niliona uchafu wenye harufu ukinitoka na nikawaambia ukweli wale marafiki zangu kuwa nina mimba, nikapelekwa tena kwa daktari ambaye alinipa vidonge vingine ambavyo pia havikufanya kazi," anasema.

Anasema alilazimika kutoa mimba hiyo kwa daktari baada ya kufika Dar es Salaam ambako awali hakuwahi kuwaza kama angerejea, baada ya kuishi China kwa siku 91.

Wale marafiki zake wa Kirusi, waliamua kumvusha aelekee Hong Kong, kisha Tanzania, lakini, alikutana na vikwazo zaidi kwa sababu bado picha yake haikufanana na ile iliyopo kwenye hati ya kusafiria.

"Waliniingiza kwenye chumba maalumu na kuanza kunikagua upya, wakaniambia nifumue nywele nilizosukia, ili wanihakiki," anasema.

Anasimulia kuwa alifanikiwa kupanda ndege kurudi nchini, akiwa ametimiza siku 91, kuanzia Januari 19 hadi Aprili 10 mwaka huu.

"Ilikuwa ni tukio jingine ambalo sikuwahi kulitegemea maishani. Sikudhani kama ningerudi tena nchini kwangu kwenye amani, sikuamini kwa kweli," anasema.

Asakwa na mwenyeji

Munira anasema akiwa njiani kurejea Tanzania, alikuwa akiwasiliana na rafiki yake ambaye yupo China bado. Rafiki huyo alimwambia kuwa mwenyeji wake, Jacky alikuwa akimsaka kwa udi na uvumba hivyo awe makini.

"Aliniambia kuwa mwenyeji wangu amesambaza picha zangu Bongo (Tanzania) ili atakayeniona anipige hadi kuniua, kisa sijamaliza deni, ambalo ni Dola 8,500 za Kimarekani (Sh12 milioni)," anasema.

Deni hilo ni malimbikizo ya Dola 200 kwa siku muda wa siku 40, ambazo alipaswa kumlipa mwanamama huyo kutokana na shughuli za ukahaba aliokuwa akiufanya.

Munira anasema alihisi kuwa yule mwenyeji wake atakuwa ametuma watu Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, hivyo aliamua kuwa wa mwisho kabisa kushuka ili kama kuna watu wabaya, wasijue kama amefika nchini siku hiyo.

"Niliposhuka kutoka kwenye ndege, ndugu zangu akiwamo mama na dada zangu walinipokea na mimi nilijizuia nisilie ili wasigundue chochote. Sikutaka wajue kuwa nilipitia shida kubwa... lakini moyoni mwangu najua mwenyewe nilivyokuwa najisikia," anasema.

Anasema hata hivyo alipohojiwa na mama yake sababu ya kurudi mapema nchini, alimdanganya kuwa hoteli aliyokuwa akifanyia kazi imeungua moto.

Kuhusu maisha ya baadhi ya Watanzania nchini China, Munira anasema wapo wasichana wadogo wa Kitanzania wanapokamatwa au kutaka kusaidiwa kurudi nchini, hukataa wakiwahofia mawakala wanaowapeleka huko.

Mawakala hao huwatisha kuwa wakiwataja au kujaribu kutoroka watawaua. Wengi wanaamini kuwa mawakala hao hutegemea nguvu za ushirikina.

Pamoja na hayo, Munira anasema wasichana wanaofanya biashara ya kujiuza China, hukumbana na ukatili wa kutisha, huku akitoa mfano wa binti aitwaye Habiba ambaye aliingiliwa na Wanigeria kadhaa kwa nguvu na baadaye aliuawa.

Anasema kutokana na hali hiyo, hata yeye anaishi kwa hofu mpaka sasa kwa sababu mawakala wanaosafirisha wasichana wa Kitanzania, wanamtafuta.

"Bado niko kwenye hatari zaidi. Nazidi kusali, kwa sababu bado niliyotendewa hayawezi kufutika katika historia ya maisha yangu na hao wabaya wangu bado wananiwinda," anasema.


Alikwendaje China?

Munira alizaliwa Oktoba 1991 jijini Dar es Salaam na baada ya kumaliza kidato cha nne alibahatika kusoma kozi ya uhudumu wa hoteli na baada ya kuhitimu aliajiriwa katika hoteli kadhaa kwa nyakati tofauti nchini.

"Nimefanya kazi kwenye hoteli nyingi hapa mjini, lakini nikaamua kujiajiri na nikaanza kununua pochi ambazo nilizisambaza kwenye ofisi mbalimbali, hapa Dar es Salaam," anasimulia.

Anasema siku moja alifuatwa na mwanamke mkazi wa Sinza, Dar es Salaam ambaye alijitambulisha kuwa anataka kumsaidia kupata kazi nzuri nje ya nchi. Anasema mwanamke huyo aliyeonekana msamaria mwema, kwanza alimuuliza ni fani gani aliyosomea na kumuahidi kuwa angemtafutia kazi.

"Nilipomwambia kuwa nimesomea masuala ya hoteli, alisema kuna kazi nyingi za hoteli nchini China na mishahara ni mikubwa kwa hiyo ningekuwa tajiri baada ya muda mfupi," anasema.

"Siku moja akaniuliza kama nina hati ya kusafiria, nikamwambia ipo kwenye mchakato wa kutafuta nikipata ningemwambia. Wakati huo kweli nilikuwa natafuta hati hiyo kwa matumizi ya safari zangu nyingine," anasema.

Anasema alipopata hati ya kusafiria alimweleza mama huyo, ambaye alimwambia kwamba asubiri huku akimpa ahadi kuwa safari huenda ikawa leo au kesho, lakini ahadi hizi hazikutekelezwa.

Siku moja mwanamke huyo, alimwambia kuwa safari yake inakaribia jambo lililomfanya auze vitu vyake vya ndani kwa ajili ya kupata fedha kidogo na kwa sababu nyumbani kwao hakukuwa na nafasi ya kuvihifadhi.

"Nikaamua kupanga hotelini kwa sababu sikutaka kuishi nyumbani kipindi kile, lakini bado nikawa napewa ahadi na yule mwanamke kuwa kesho, kesho, hivyo hivyo," anasema.

Ushauri wa mama

Anaeleza kuwa kutokana na ahadi kuwa nyingi, mama yake (Mama Munira) alimshauri aachane na safari hiyo akapatwa na hisia kuwa pengine haina mwisho mzuri.

"Mama alinikataza nisisafiri. Aliniambia hiyo safari siyo nzuri, nikamuuliza kwa nini, lakini hakuniambia. Nikaamua kumweleza yule dada kuwa sitakwenda tena kwa sababu mama amekataa. Basi kwa kufanya hivyo nilikuwa nimezua balaa jingine," anasimulia.


Baada ya kumweleza yule mwanamke, Munira anasema alishangaa anafuatwa na wanawake wanne wakazi wa Magomeni, baadhi yao aliwafahamu na wengine hakuwa akiwafahamu ambao walifika katika hoteli aliyopanga na kuanza kumtukana na kufanya fujo.


Alisema kinamama hao walikuwa wakihoji sababu za kukataa kwake kwenda China, tena dakika za mwisho wakati wao wapo kwenye mchakato wa kumwandalia safari.

"Walifanya fujo kweli hadi uongozi wa hoteli ile ukataka kunifukuza. Yaani walikuwa ni washari, halafu mibonge ya mijimama iliyoshiba kikweli kweli," anasema Munira.

"Waliniambia niwape Dola za Marekani 350 kwa ajili ya viza na pia niwape hati ya kusaifiria. Wakaja tena siku ya pili wakaniambia safari yangu ni keshokutwa," anasema.

Aliamua kuwapa kiasi chote cha fedha kilichobaki kwa sababu tu alitaka kusafiri, lakini wakati huo yeye aliamua kuishi kwa rafiki yake kwa kuwa hakuwa na fedha zaidi za kupanga hoteli.

"Niliishiwa pesa kabisa nikabaki na kama laki moja tu, ndiyo maana nikaamua kuishi Gongo la Mboto, kwa rafiki yangu," anasema.

Safari ya Guangzhou

Munira anasema siku hiyo aliyofika kwa rafiki yake, alipigiwa simu na wale wanawake wakamwambia wanahitaji kuonana naye.

"Nikachukua bajaji kwa Sh15,000 mpaka Magomeni nilipoelekezwa. Nikamkuta huyo dada ambaye alikuwa mgeni kwangu. Alikuwa na mume wake na mimi nilikuwa na rafiki yangu. Nilikuja kujua baadaye jina lake ni Josephine," anasema.

Anasema Josephine alimdai Sh15,000 ambayo alisema ni kwa ajili ya kukodi gari, kuelekea Uwanja wa Ndege na wakati huo Josephine alikuwa akimjazia kadi ya chanjo ya homa ya manjano.

Anasema alikabidhiwa kadi hiyo na walipofika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, alikuwa tayari ameshapewa masharti kuwa asibebe nguo nyingi, asisuke wala kujipamba sana.

"Tulipofika uwanja wa ndege yule dada akaanza kuniuliza kwamba mimi nitamsaidiaje kwa sababu naye amenisaidia, akawa ananiambia, si umeniona nilivyokusaidia hata fulani na fulani (anawataja majina) nimewasaidia na wewe unanisaidiaje?" anasimulia.

Muda wa kuingia ndani ya ndege ulipofika yule dada alimpa tiketi, lakini akakumbusha tena kuhusu kusaidiwa, ndipo Munira alipoamua kumpa Sh20,000 na baadhi ya nguo zake.


"Lakini, kabla sijaondoka akaniambia nikiulizwa naenda wapi, niseme dada yangu amejifungua na mimi naenda kumwangalia huko China kwa kuwa hana msaidizi," anasema Munira.

"Jambo la kushangaza ni kuwa alikuwapo msichana mwingine hapo uwanja wa ndege na nilishangaa kuambiwa na mwanamke mmoja kuwa kama naenda China basi nimsaidie mdogo wake ambaye naye anakwenda China," Munira anasema na kuongeza kuwa alimkubalia.

"Ilitokea tukakaa kiti kimoja, na tukaanza kuzungumza katika mazungumzo yetu nikagundua kuwa naye ameambiwa anaenda China kufanya kazi ya hoteli. Nilishangaa lakini sikushtuka. Mwenzangu alikuwa anaitwa Chantelle," anasema.

Baridi kali Ethiopia

Baada ya safari ya saa kadhaa, walifika Addis Ababa, Ethiopia ambako ni kituo cha kwanza kabla ya safari ya mojua kwa moja kwenda China, lakini hali ya pale ilikuwa ni ya baridi sana na Munira hakuwa amebeba koti au jaketi.

Munira na Chantelle walisubiri kwa saa tano hivi kabla ya kuondoka Addis Ababa na hata muda wa kuondoka ulipofika, Munira aligundua kuwa pasi yake ya kusafiria ilikuwa haionekani.

"Lakini kwa bahati nzuri baada ya kumwaga vitu vyangu vyote chini, niligundua kuwa pasi yangu ilikuwa imejibana ndani ya begi ndipo niliporuhusiwa kuingia kwenye ndege," anasema.

Munira na mwenzake, walifanikiwa kufika Guangzhou muda wa saa 9:00 alasiri na huko walikutana na baridi kali kuliko ile ya Ethiopia.

Wakati huo, kila mmoja alikuwa akijaribu kupata mawasiliano ya mwenyeji wake na kwa bahati mbaya, Chantelle hakufanikiwa kumpata mwenyeji wake.

"Nikamwambia Chantelle kwa kuwa tumekuja pamoja halafu wote tumekuja kwa ajili ya kazi za hoteli, wacha nimpigie mwenyeji wangu tuondoke wote hadi utakapompata wa kwako, alikubali," anasema.

Baada ya kuzungumza na mwenyeji wake aliyefahamika kwa jina moja la Jacky, walielekezwa wakodi teksi hadi katika hoteli moja ifahamikayo kama Nairobian.

Kutoka uwanja wa ndege hadi katika hoteli waliyoelekezwa, ilikuwa ni sawa na umbali wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere na Bagamoyo. Walitakiwa kulipa Yuan 200 ambayo ni sawa na Sh60,000.


Munira anasema, hakumkuta mwenyeji hasa aliyepewa maelekezo yake akiwa Tanzania, bali alipokewa na Mtanzania mwingine aliyeachiwa maagizo na Jacky, ambaye alikuwa amekwenda Malaysia kutafuta viza.

Huo ukawa mwanzo wa maisha yake China, ambayo yalijaa dhiki, mateso na tabu za aina yake. Chantelle kwa upande wake alimpata mwenyeji wake na kuendelea na maisha nchini humo.

MWISHO.





 
kwa nini asingekataa?huko magomeni alikuwa anaishi kwa nani? au ndio alikuwa kwa macheni?kwa nini asingepiga simu kwao kuwa kuna matatizo atumiwe nauli arudi ?nauli ya china ni mil 1 sasa kwa nini asingetafuta balozi za tanzania huko china aombe msaada kwa kwa vyombo vya habari? mapato yake kwa siku ni kiasi gani kwa huo umalaya? kwa nini alitoa hiyo mimba? amepima hiv?
 
Ajira shida na elimu vilevile shida! Mtu anapochonga bahati yake huwa hwaambie wenzake ili akiukata aje kuwaringia baadae kumbe. Angezungumza angeambiwa unakotaka kwenda si kwema na kama atafikiri ni wivu mwache aende akavune alichopanda. Si tunaona Wahindi wanaletwa kwetu Watanzania wanapelekwa India, China na kwingineko! Mungu tusamehe makosa yetu na tunakuomba sana utuepushe na haya majanga.
 
Did she say $200 day...???

Tuwasubiri wenyeji wa chambu-chambu.
 
Last edited by a moderator:
Inaelekea huko wamejaa wasichana wa magomeni manake kila aliemuona anasema ni wa magomeni, na hivyo ndivyo wanavyoingizwa kwenye biashara za madawa ya kulevya, ila pia kama hawataki na hawapendezwi na huko kuuzwa kwanini huwa hawakimbilii ubalozi kuomba msaada? au kukosa elimu kunawafanya wawe wafinyu wa kufikiri? Me nazani wengi wao hufurahia na hata wanapopata nafasi za kurudi huku wanakuja kujitapa kwa wenzio kwamba mambo safi
 
Heheheheh mm namjua mmoja yupo macau ila hata huku alikuwa anauza naona kapanda daraja nw
 
Hivi kuna watu wanawaza kweli??

Nchi yenye idadi ya watu bilioni kadhaa halafu unategemea kupata ajira huko??

Bora ubaki bongo ukalime vitunguu na kupata visenti kadhaa.


hivi wanapo muona mchina mwenye nchi yake anuza vyuma gerezani kariakoo wanahisi kwanini kaja huku Mimi mtz yoyote alieko India, China, Malaysia, afu anakwambia anatafuta huwa na mshangaa Sana unashindwa kushiba kwenye sinia ushibe kwenye kijiko
 
Nilimsikiliza huyo dada clouds radio,kwenye kipindi cha njia panda,kwa kweli waTz wako wengi sana huko,chakushangaza!!?kama wanaona tabu,kwa nn wasiende kwenye ubaloz wa TZ wakatafuta msaada.mi nadhan nikukosa elimu au wanapenda.
 
Nilimsikiliza huyo dada clouds radio,kwenye kipindi cha njia panda,kwa kweli waTz wako wengi sana huko,chakushangaza!!?kama wanaona tabu,kwa nn wasiende kwenye ubaloz wa TZ wakatafuta msaada.mi nadhan nikukosa elimu au wanapenda.

Hao watu ni mafia haswa. Huo muda wa kwenda ubalozi ataupata wapi? Akiingia kule keshakuwa mtumwa na passport wanachukua.
Watu wanapenda ubwete sana Bongo. Kule China maskini kibao mtu anadanganywa kama mtoto mdogo. Mbona wachina wenyewe wanakuja kujiuza hapa Bongo. Si wangebaki kwao wafanye hizo kazi za hotelini? Sijui ni upeo mdogo mtu hupati jibu.
Serikali yet japo haiwezi kufuatilia nyendo binafsi za mtu mmoja mmoja, wanayo sehemu ya lawama. Ingetafuta njia za kuwaeleimisha hasa vijana na utapeli huo. Bado kuna vichwa maji wataenda lakini wengine watastuka. Mtu from nowhere anakuwa mfanyabiashara za kwenda China!
 
Wabongo kwa kudanganyika, waliwe tuu

Hawa wanawake wasilalamike kwani walijua fika kwamba wanakwenda kufanya umal..... China. mtu huna elimu. huna cheti chochote. hujui kiingereza wala kichina. unatafutiwa paspot mpaka yai viza ya china. unategemea kweli aanakuhudumia paspot na yai viza akakupe kazi china waqt wachina wenyewe wamjaa bongo. mtu akugharamie vyote hivyo na sio ndugu yako kweli unategemea akutafutie kazi china na malazi juu bila kusahau maradhi. Tumia akili mama
 
Mnazunguka tuu mbuyu hapa, huyo wakala wa hapa bongo ni nani?

Anapatikana Migomigo kwenye bar maarufu karibu na kibenki kimoja. Fika pale nunua soda uinywe masaa mawili uonekane kama huna dili au pesa atakuaprochi. umri usizidi 25
 
Back
Top Bottom