Bilioni 286 Kujenga Uwanja Mpya wa "Samia Suluhu Hassan Arusha Stadium" Kwa Ajili ya AFCON 2027

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,054
49,739
Serikali imeingia mkataba wa kuanza Ujenzi wa uwanja Mpya Jijini Arusha Maarufu kama Samia Suluhu Hassan Stadium ambao ni Mahsusi Kwa Ajili ya Maandalizi ya AFCON 2027.

Uwanja huo utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 286.

Kazi iendelee 👇👇

View: https://youtu.be/q05ytnyfpa0?si=jLrsYa4X_7tKcjKO

============

Serikali kupitia wizara ya Sanaa ,Utamaduni na Michezo leo Machi 19, 2024 imesaini mkabata wa ujenzi wa Uwanja wa Dokta Samia Suluhu Hassani wenyewe thamani ya shilingi bilioni mia mbili na themanini na Sita ambao utatumika katika michuano ya mataifa Afrika AFCON 2027 inayoandaliwa na nchi za Tanzania, Kenya na Uganda

Akizungumza na waandishi wa habari Waziri wa Michezo Dokta Damasi Ndumbaro amesema Lengo la uwanja huo kujengwa mkoani Arusha ni kuchochea maendeleo ya sekta utalii kupitia michezo.
---

BILIONI 286 KUTUMIKA UJENZI WA UWANJA MPYA JIJINI ARUSHA

Serikali imesaini Mkataba wenye thamani ya shilingi Bilioni 286 na kampuni ya China Construction Engineering Group (CRCEG) kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mpya wa mpira wa miguu Mkoani Arusha.

Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini Mkataba huo leo Machi 19, 2024 Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro amesema uwanja huo utakuwa na uwezo wa kuingiza watazamaji 30,000 huku akibainisha kuwa uwanja huo utakuwa wa kisasa zaidi Afrika Mashariki.

Amesema Serikali itahakikisha ujenzi huo unafanywa kwa haraka kwa kuwa Tanzania itakuwa mwenyeji wa michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027 ikiwa ni juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema uwanja huo utachagiza kwa kiasi kikubwa utalii nchini kwa kuwa uwepo wa uwanja huo utakuwa chachu shughuli mbalimbali tofauti na mpira wa miguu kama vile mchezo wa riadha, biashara zitakazokuwa zinafanyika.

"Uwanja huu utakuwa na ubora wa hali ya juu kwani utakuwa na vyumba vya watu mashuhuri, tumefanya zoezi hili leo ambapo, Rais Samia wetu anatimiza miaka mitatu ya uongozi wake, amesema Dkt. Ndumbaro.

Aidha, ameipongeza Kamati ya kudumu ya Bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo kwa juhudi ilizofanya za kuhakikisha zoezi hilo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo Mhe. Husna Sekiboko amemtaka Mkandarasi wa uwanja huo ahakikishe kuwa ujenzi huo unakamilika kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

"Wakandarasi hakikisheni kabla ya uchaguzi wa mwaka 2025 uwanja uwe umefikia kiwango kinachoridhisha na utekelezaji huo uanze haraka iwezekanavyo ikiwa ni maandalizi kuelekea katika michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON),"amesema.

Amesema Kamati itatoa ushirikiano kuhakikisha ujenzi huo unafanyika kama ilivyokusudiwa akibainisha kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anaitendea haki sekta ya michezo kama anavyofanya kwenye sekta nyingine akitoa wito kwa wakazi wa Arusha watunze miundombinu ya uwanja huo.

View: https://twitter.com/MsigwaGerson/status/1776649963608342614?t=Y2yLEpnC-hxC0Wn2ukTW_g&s=19

-679785384.jpg
1268245040.jpg
2059848824.jpg
-837842686.jpg
623001783.jpg
 
Serikali imeingia mkataba wa kuanza Ujenzi wa uwanja Mpya Jijini Arusha Maarufu kama Samia Suluhu Hassan Stadium ambao ni Mahsusi Kwa Ajili ya Maandalizi ya AFCON 2027.

Uwanja huo utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 286.

Kazi iendelee 👇👇

============

Serikali kupitia wizara ya Sanaa ,Utamaduni na Michezo leo Machi 19, 2024 imesaini mkabata wa ujenzi wa Uwanja wa Dokta Samia Suluhu Hassani wenyewe thamani ya shilingi bilioni mia mbili na themanini na Sita ambao utatumika katika michuano ya mataifa Afrika AFCON 2027 inayoandaliwa na nchi za Tanzania, Kenya na Uganda

Akizungumza na waandishi wa habari Waziri wa Michezo Dokta Damasi Ndumbaro amesema Lengo la uwanja huo kujengwa mkoani Arusha ni kuchochea maendeleo ya sekta utalii kupitia michezo.

View attachment 2938864View attachment 2938865View attachment 2938866
Mama anang'arisha sekta ya michezo kwa nguvu zote 🐒
 
Back
Top Bottom