Bila shaka huu siyo msimamo wa TBC

ThnkingAloud

JF-Expert Member
Sep 13, 2017
232
180
Hbr wanajamvi,

Jana timu yetu ta Taifa pamoja na kufungwa na Morroco lakini walijitahidi kwa kadri ya uwezo waliokuwanoa.

Kitu kilichonisikitisha ni mtangazaji mmoja wa TBC kutoa maneno ya kashfa kuhusu eneo moja la nchi yetu linaloitwa Mbagala. Eneo hili nadhani liko katika mkoa wa Dar es Salaam wilaya ya Temeke.

Maneno haya ya kashfa kuhusu Mbagala aliyoyotaa huyu mtangazaji nadhani hakutumwa na Menegejimenti au Bodi ya Wakurugenzi ya TBC na kwa hiyo siyo msimamo wa TBC hata kidogo. Kama hivyo ndivyo ilivyo ninasubiri kuona Uongozi wa TBC utamchukulia hatua gani huyo mtangazaji ili iwe fundisho kwa watangazaji wengine.

Niko hapa A Town nasubiri.
 
Yule mtangazaji Huwa analazimisha kuchekesha watazamaji wa Tv tbc1 lakini hawezi, matokeo yake Huwa anajikuta anatoa vimaneno vya kukejeli na kukera wasikilizaji!
 
Back
Top Bottom