Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Hatimaye kile kitendawili cha kuwepo au kutokuwepo uchaguzi mdogo Jimbo la Biharamulo Magharibi, kimeteguliwa baada ya Mkurugenzi wa Uchaguzi Rajabu Kiravu, kukitegua.
Uchaguzi huo unafanyika kesho Jumapili Julai 5.
Uchaguzi huo unafuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo Hilo, Pheres Kabuye, kilichosababishwa na ajali ya gari mkoani Morogoro. Huu ni uchaguzi mwingine wa moto kati ya TLP kuthibitisha sio chama mfu kwa kutetea kwa nguvu zote, kiti pekee cha ubunge kilichoshikwa na chama hicho, Chadema lazima ifanye tena kipimo cha operesheni Sangara huku CUF iking'ang'ana na Ngangari yake wakati CCM watataka kumaliza usongo wa kulikosa jimbo hilo kwa kipindi kirefu.
Je Matokeo yatakuwa yale yale kama tutakayoyashuhudia Busanda hivi karibuni, watagawana kura nyingi hivyo kumpa mwanya mgombea wa CCM kushinda kwa kura chache na mwisho wa yote, "The winner takes it all".
Kwa wapinzani kutoungana na kumsimamisha mgombea mmoja, ni CCM Busanda, CCM Biharamulo na 2010 ni CCM kwa kwenda Mbele.
Uchaguzi huo unafanyika kesho Jumapili Julai 5.
Uchaguzi huo unafuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo Hilo, Pheres Kabuye, kilichosababishwa na ajali ya gari mkoani Morogoro. Huu ni uchaguzi mwingine wa moto kati ya TLP kuthibitisha sio chama mfu kwa kutetea kwa nguvu zote, kiti pekee cha ubunge kilichoshikwa na chama hicho, Chadema lazima ifanye tena kipimo cha operesheni Sangara huku CUF iking'ang'ana na Ngangari yake wakati CCM watataka kumaliza usongo wa kulikosa jimbo hilo kwa kipindi kirefu.
Je Matokeo yatakuwa yale yale kama tutakayoyashuhudia Busanda hivi karibuni, watagawana kura nyingi hivyo kumpa mwanya mgombea wa CCM kushinda kwa kura chache na mwisho wa yote, "The winner takes it all".
Kwa wapinzani kutoungana na kumsimamisha mgombea mmoja, ni CCM Busanda, CCM Biharamulo na 2010 ni CCM kwa kwenda Mbele.
Last edited by a moderator: