Kaniki1974
JF-Expert Member
- Dec 2, 2008
- 352
- 22
Rais bora wa TZ next to Mwl. J. Nyerere
Aliingia madarakani kwa haki bila rushwa wala kununua vyombo vya habari. Alikuwa na hoja na alieleza WAZI nia yake ya kugombea urais.
Alianza kazi kwa kasi hakungoja wiki mbili au zaidi kupanga baraza la mawaziri.
Aliunda serikali ndogo kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Alikuwa na falsafa binafsi, dira na msomi aliyependa kusoma na kujifunza.
Akapambana kijemedari kwelikweli na misukosuko ya Reli, MV Bukoba, Elnino na majanga mengine. Akapunguza mfumuko wa bei toka 48% 1994 na kubakia single digit enzi zote za utawala wake.
Akaboresha utumishi wa umma; kapunguza wafanyakazi hewa na kuboresha maslahi.
Akapunguza deni la nje na kuipa Tanzania heshima.
Akajenga miundo mbinu hususan barabara kwa kasi kubwa
Akavutia wawekezaji wenye tija kama TBL, NBC n.k
Akajenga EPZ alipanga zijengwe 22 nchi nzima
Akaimarisha majeshi yetu kwa kuwapatia motisha vitendea kazi na makazi.
Akajenga Uwanja wa Taifa
Akajenga Benki kuu Twin towers na kule Zanzibar. Twin Towers kama Bank of Canada, Toronto (kwa wanaojua)
Alikuwa na hoja zenye mashiko.
Alikuwa kiongozi kweli jasiri, mwenye kujiamini na hakuogopa mihadhara: iwe ya vyama vya siasa, vyuo vikuu au kimataifa. Alikuwa full of substance.
Ujasiri wake hata vita ingetokea enzi zake angetuongoza vyema sana kumshinda adui.
Hakuwa mwongo katika kauli na ahadi zake.
Alikuwa na maadili na na hekima na aliheshimu mamlaka na taratibu zilizopo.
Akawapa nguvu na haki zaidi wanawake.
Alipigania utandawazi kuwanufaisha wengi.
Alikuwa mchapakazi hakuwa mvivu.
Alikuwa makini na alipinga na kukwepa sana matumizi yasiyo lazima ya serikali.
Alisafiri ngambo pale tu ilipobidi. Alikaa ofisini na kufanya kazi.
Alijiheshimu hakuwa Fataki.
Hakuwa ombaomba, bali alipenda kujenga uwezo, kujitegemea na kuwasaidia ombaomba.
Akanunua ndege bora ya Rais, mafisadi wakaipinga.
Akanunua rada ya nguvu, mafisadi wakaipinga.
Alikuwa na vyeti vya nguvu na alifuzu vyema masomo yake. Alionyesha uwezo. Alikuwa na speech za kisomi.
Alihakikisha nchi inakaribia kupaa ndio akaikabidhi kwa JK. Tukadhani itapaa.
Na mengine mengi.
Huyo ndiye Benjamin William Mkapa, Rais ninayemkubali na kumrank second. Angekuwepo mpaka leo Tanzania ingekuwa emerging economy I am sure.
Mnaomsema vibaya mshindwe ka kulegea. Hamna shukrani. Ni kiongozi ambaye wanaokumbuka, tunamshukuru sana.
Aliingia madarakani kwa haki bila rushwa wala kununua vyombo vya habari. Alikuwa na hoja na alieleza WAZI nia yake ya kugombea urais.
Alianza kazi kwa kasi hakungoja wiki mbili au zaidi kupanga baraza la mawaziri.
Aliunda serikali ndogo kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Alikuwa na falsafa binafsi, dira na msomi aliyependa kusoma na kujifunza.
Akapambana kijemedari kwelikweli na misukosuko ya Reli, MV Bukoba, Elnino na majanga mengine. Akapunguza mfumuko wa bei toka 48% 1994 na kubakia single digit enzi zote za utawala wake.
Akaboresha utumishi wa umma; kapunguza wafanyakazi hewa na kuboresha maslahi.
Akapunguza deni la nje na kuipa Tanzania heshima.
Akajenga miundo mbinu hususan barabara kwa kasi kubwa
Akavutia wawekezaji wenye tija kama TBL, NBC n.k
Akajenga EPZ alipanga zijengwe 22 nchi nzima
Akaimarisha majeshi yetu kwa kuwapatia motisha vitendea kazi na makazi.
Akajenga Uwanja wa Taifa
Akajenga Benki kuu Twin towers na kule Zanzibar. Twin Towers kama Bank of Canada, Toronto (kwa wanaojua)
Alikuwa na hoja zenye mashiko.
Alikuwa kiongozi kweli jasiri, mwenye kujiamini na hakuogopa mihadhara: iwe ya vyama vya siasa, vyuo vikuu au kimataifa. Alikuwa full of substance.
Ujasiri wake hata vita ingetokea enzi zake angetuongoza vyema sana kumshinda adui.
Hakuwa mwongo katika kauli na ahadi zake.
Alikuwa na maadili na na hekima na aliheshimu mamlaka na taratibu zilizopo.
Akawapa nguvu na haki zaidi wanawake.
Alipigania utandawazi kuwanufaisha wengi.
Alikuwa mchapakazi hakuwa mvivu.
Alikuwa makini na alipinga na kukwepa sana matumizi yasiyo lazima ya serikali.
Alisafiri ngambo pale tu ilipobidi. Alikaa ofisini na kufanya kazi.
Alijiheshimu hakuwa Fataki.
Hakuwa ombaomba, bali alipenda kujenga uwezo, kujitegemea na kuwasaidia ombaomba.
Akanunua ndege bora ya Rais, mafisadi wakaipinga.
Akanunua rada ya nguvu, mafisadi wakaipinga.
Alikuwa na vyeti vya nguvu na alifuzu vyema masomo yake. Alionyesha uwezo. Alikuwa na speech za kisomi.
Alihakikisha nchi inakaribia kupaa ndio akaikabidhi kwa JK. Tukadhani itapaa.
Na mengine mengi.
Huyo ndiye Benjamin William Mkapa, Rais ninayemkubali na kumrank second. Angekuwepo mpaka leo Tanzania ingekuwa emerging economy I am sure.
Mnaomsema vibaya mshindwe ka kulegea. Hamna shukrani. Ni kiongozi ambaye wanaokumbuka, tunamshukuru sana.