BBC: Dr. Ulimboka yuko ICU (yuko kwenye koma) anasaidiwa na mashine

Tunamwombea kwa mungu apone haraka.
Waliofanya kitendo hiki watambue kwamba nao siku zao zinahesabika.
 
Concern
Ninashaka hapa hivi uchunguzi wa jeahi la polisi kama mimi mtendwa sitaki kwanini unalaImisha wakati sina imani na ulichokiunda na cha ajabu nawe unanambia hata kama hutaki sie tunaendelea. Nini kipo nyuma ya pazia la polisiiiiiii???[/QUOTE]

Bro sisi sote tunatakiwa kuonyesha uelewa wetu. Unachosema ni kuwa mtu UNAWEZA KUMUUA MWANAO NA KUSEMA KUWA NI MWANANGU. Au unaweza kunywa sumu na ukasema NIMEJIDHURU MWENYEWE! Mambo hayaendi hivyo. Polisi kazi yake ni kufanya uchunguzi hata kama wasingetangaza. Hiyo ni kazi yao ya msingi. Jambo la muhimu ni kuwa mazingira ya jambo lenyewe ni vigumu sana kupata ukweli wa mambo. Nionavyo mimi hata kama uchunguzi ufanywe na madaktari wenye bado ni VIGUMU KUPATA MAJIBU. Waacheni polisi wafanye na majibu yao KWA VYOVYOTE VILE HAYATAMSAIDIA ULIMBOKA. Ni fomalities tu.
 
Determine amesema hali ya uli inaimarika na kwa bbc hali yake ni tete na huku hawakuruhusiwa kumwona. Je bbc walijuaje km ni mahututi icu. Tumwamini nani jamani. Tunataka mpiganaji wetu apone.Mungu amsaidie uli.
 
tell us whom u trust mdau....apelejwe wapi sasa????ambako kuna usalama wake....
gazeti la nipashe lasema AFYA YA DR ULIMBOKA YAZIDI KUIMARIKA
vyombo vya habari vyote vya Tanzania havina maana, njaa inavimaliza, vimekuwa vinaendesha tu propaganda kuhusu huu mgomo. Hii serikali naishangaa sana, pesa za kuhonga vyombo vyote vya habari wanazo lakini kutengeneza mazingira bora ya kufanyia kazi hawana. Huu ni ujuha wa dhaifu na serikali yake.

Mimi binafsi nimemsikia mtangazaji wa BBC aliyemtembelea Uli hospitali akisema ulimboka yuko kwenye 'coma, na anapumua kwa kusaidiwa na mashine, wao wanasema hali yake inaimarika. Kweli Propaganda mpaka kwenye uhai wa mtu?.

Angalia Jambo leo linavyoripoti kwe kejeli hali ya Afya ya ulimboka. Angalia jinsi Umma unavyopotoshwa kuhusu mgomo. Mgomo unaendelea ingawa kuna baadhi ya madaktari wa MOI walisaini mahudhurio na kuondoka, hakuna daktari anaefanya kazi, msiwadanganye watu wakatoka mikoani kwenda Muhi2.

La kushangaza hata wanataaluma kama Prof Museru na Mwafongo nao wameingia kwenye usaliti wa taaluma na kuendelea propaganda za serikali. Hivi kufikia kumnyima hata ambulance colleague kwa sababu ya cheo au pesa ni ujuha au ni nini. Mwafongo, Museru na wengine Muhimbili, kumbukeni serikali hii ya kifisadi na kigaidi haina rafiki wa kudumu, itakapowageuka mtakumbuka ubaya mnaowafanyia wanataaluma wenzenu.
 
Mungu uliyemwokoa Ulimboka na kifo pale msituni tunakuomba umponye sasa..Amina!!!!!!!
 
SASA HUO UCHUNGUZI AU TUME ILIYOUNDWA NA POLISI UHALALI WAKE HUKO WAPI MAANA WAO NI WATUHUMIWA. KATIKA NCHI YETU HAPAJAWAHI TOKEA POLISI WAKACHUNGUZI SWALA LOLOTE LINALOWAGUSA NA MATOKEO YAKAWA FAIR. BASI TUMWOMBE MUNGU NDG YETU APATE KUPONA MAANAKE IKITOKEA IKAWA VINGINEVYO KUNASITOFAHAMU KWA WAPENZI, NDUGU , MARAFIKI NA WAPENA HAKI. MATAMUSHI YA WATAWALA YANAONYESHA ''Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyohakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo,lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemeavizuri zaidi kuliko wao wenyewewalioajiriwa na Serikali.'
 
Natamani kumowna akishuka kwenye ndege alitembea mwenyewe na kuzungumza na waandishi wa habari pale jk nyerere airport, ee mungu tunkuomba utimize ndoto yetu waja wako iwe kweli!
 
Yan watu wengne wanaleta siasa ht kwenye uhai wa mtu.Tunawawahis kuwa nao ni wahusika lakin bdo wanajichunguza....Naomba Mungu dkt MBOKA apone la sivyo tutaandamana mpk ikulu watu wa Mbeya mnatunyanyasa kwa kutuulia rasilimal zetu!
 
SASA HUO UCHUNGUZI AU TUME ILIYOUNDWA NA POLISI UHALALI WAKE HUKO WAPI MAANA WAO NI WATUHUMIWA. KATIKA NCHI YETU HAPAJAWAHI TOKEA POLISI WAKACHUNGUZI SWALA LOLOTE LINALOWAGUSA NA MATOKEO YAKAWA FAIR. BASI TUMWOMBE MUNGU NDG YETU APATE KUPONA MAANAKE IKITOKEA IKAWA VINGINEVYO KUNASITOFAHAMU KWA WAPENZI, NDUGU , MARAFIKI NA WAPENA HAKI. MATAMUSHI YA WATAWALA YANAONYESHA ''Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyohakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo,lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemeavizuri zaidi kuliko wao wenyewewalioajiriwa na Serikali.'

Kutokuwa mtumishi wa serikali hakumuondolei U-Tanzania wake na ubinadamu wake
 
sasa huyo wa BBC karuhusiwaje kumuona huko? na si wanasema yuko Ujerumani? ina maana kuna mtu anatuchakachua hapa na habari sio! ngoja tuone
 
Doctor anaendelea vzr,sema hatuwataki hawa BBC waende kumuona@ km kuna mtu hataki Dr ulimboka kupona bora ajinyonge make Doctor kashaanza kuimarika
at least utanifanya ninywe chai! natamani kusikia jk ndiyo anapumulia mashine, nitashinda nikinywa calabash!
 
Mungu mtakatifu aliyemwepusha na kifo katika msitu wa mabwepande awe pamoja naye hata SA.
 
Kikwete, Pinda, mtoto wa Mwinyi, kova. Kweli wanajisikiaje kumuona mwenzao anateseka.
 
Mungu mponye kijana huyu. Imani yetu ni kwamba atapona na kurudi nyumbani salama.
 
bahari nzuri nimerekodi hiyo taarifa ya bbc na ninayo hapa...

Ali mtasa mtangazaji wa bbc alikwenda hosp.moja huko africa ya kusini alokolazwa dr ulimboka.alipofika alienda maulizo na kuonyeshwa chumba alicholazwa. wakati akielekea huko alikutana n ndugu wa ulimbo walioko hapo hosp na yeye alimuona ulimboka kupitia kwenye vioo na wala hakuingia chumbani kabisa.

alipojitmbulisha kwa ndugu wa ulimboka, mara moja walimuambia aondoke hosp hapo maana hawahitaji mtu na wala asifatilie lolote kuhusu maendeleo ya ulimboka.alipoulizia hali yake inakwendaje hakujibiwa kitu isipokuwa aliambiwa aondoke mara moja. na akaondoka....

hiyo ya kusema kuwa dr uli yuko kwenye koma ameipika mwenyewe maana dr uli alikuwa amepumzika na wala hakunandugu hata mmoja aliyemwambia kuwa yuko kwenye koma..
 
Back
Top Bottom