nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
*Kijana UVCCM awarushia tuhuma nzito
*Awapa siku 21 watuhumiwa wangoke
Na Mwandishi Wetu - Mtanzania
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Agustino Matefu, ameibuka na kusema tayari ana majina manane ya wana CCM walio kwenye orodha ya kupewa barua za kujivua uongozi.
Matefu, ambaye aliwashambulia baadhi ya wanasiasa wakongwe ndani ya CCM, alitaja orodha hiyo alipozungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Hadees, jijini Dar es Salaam, jana.
Aliwataja wanachama walio kwenye orodha ya kuadhibiwa kuwa ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge.
Wengine ni Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Taifa Beno Malisa; Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Martin Shigela; Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Francis Isack; na Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa, Hussein Bashe.
Kijana huyo alisema amechukua uamuzi wa kuzungumza suala hilo kama mchango wake kwenye mtafaruku na mgongano wa mawazo ya kimageuzi unaoendelea ndani ya CCM.
Ingawa hakusema kama alichokizungumza ni cha UVCCM Mkoa au ni mawazo yake binafsi, alisema wao kama vijana wanaunga mkono mabadiliko yanayoendelea ndani ya CCM.
Alisema wanapinga siku 90 walizopewa watuhumiwa wa ufisadi kwa maelezo kwamba ni nyingi mno. Badala yake, alisema UVCCM wanawapa watuhumiwa hao siku 21 wawe wameachia nafasi walizonazo, vinginevyo umoja huo Mkoa wa Dar es Salaam utachukua hatua kali.
Haiwezekani wakapewa siku 90 kama wapangaji, tunawapa siku 21, kwani hawa ni wezi wa rasilimali zetu kwa kuwa tumechoka kudanganywa na vi-mia mbili vyao, na muda huo ukifika wakiwa hawajaachia nafasi hizo jiji hili litakuwa halitoshi, kwani hatuna ugomvi na mtu zaidi ya kutetea maslahi ya chama chetu, alitamba Matefu.
Alisema kuwa ndani ya UVCM kuna mafisadi 100 wanaofadhiliwa na watuhumiwa wakuu wa ufisadi.
Aidha, alisema kuwa kutokana na UVCCM kushindwa kumshauri vizuri aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, hata kufikia chama kupoteza mwelekeo, ni busara sasa wakajipima na kukaa pembeni ili wengine waongoze.
Aliongeza kuwa makada wa chama hicho wanatambuliwa kwa uongo, unafiki na kujipendekeza kulikojaa uchu wa madaraka, huku wakikumbatiwa na mmoja wa wanasiasa wakongwe ndani ya CCM.
*Awapa siku 21 watuhumiwa wangoke
Na Mwandishi Wetu - Mtanzania
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Agustino Matefu, ameibuka na kusema tayari ana majina manane ya wana CCM walio kwenye orodha ya kupewa barua za kujivua uongozi.
Matefu, ambaye aliwashambulia baadhi ya wanasiasa wakongwe ndani ya CCM, alitaja orodha hiyo alipozungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Hadees, jijini Dar es Salaam, jana.
Aliwataja wanachama walio kwenye orodha ya kuadhibiwa kuwa ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge.
Wengine ni Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Taifa Beno Malisa; Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Martin Shigela; Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Francis Isack; na Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa, Hussein Bashe.
Kijana huyo alisema amechukua uamuzi wa kuzungumza suala hilo kama mchango wake kwenye mtafaruku na mgongano wa mawazo ya kimageuzi unaoendelea ndani ya CCM.
Ingawa hakusema kama alichokizungumza ni cha UVCCM Mkoa au ni mawazo yake binafsi, alisema wao kama vijana wanaunga mkono mabadiliko yanayoendelea ndani ya CCM.
Alisema wanapinga siku 90 walizopewa watuhumiwa wa ufisadi kwa maelezo kwamba ni nyingi mno. Badala yake, alisema UVCCM wanawapa watuhumiwa hao siku 21 wawe wameachia nafasi walizonazo, vinginevyo umoja huo Mkoa wa Dar es Salaam utachukua hatua kali.
Haiwezekani wakapewa siku 90 kama wapangaji, tunawapa siku 21, kwani hawa ni wezi wa rasilimali zetu kwa kuwa tumechoka kudanganywa na vi-mia mbili vyao, na muda huo ukifika wakiwa hawajaachia nafasi hizo jiji hili litakuwa halitoshi, kwani hatuna ugomvi na mtu zaidi ya kutetea maslahi ya chama chetu, alitamba Matefu.
Alisema kuwa ndani ya UVCM kuna mafisadi 100 wanaofadhiliwa na watuhumiwa wakuu wa ufisadi.
Aidha, alisema kuwa kutokana na UVCCM kushindwa kumshauri vizuri aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, hata kufikia chama kupoteza mwelekeo, ni busara sasa wakajipima na kukaa pembeni ili wengine waongoze.
Aliongeza kuwa makada wa chama hicho wanatambuliwa kwa uongo, unafiki na kujipendekeza kulikojaa uchu wa madaraka, huku wakikumbatiwa na mmoja wa wanasiasa wakongwe ndani ya CCM.