Bashe: Kuna kikundi ndani ya TISS kinahusika na utekaji. Wabunge 11 wapo kwenye orodha ya kutekwa

Kwa madai kama hayo kweli akiambiwa atoe ushahidi na vielelezo anaweza? Kweli, Kiki nyingine ni mbaya na za hatari sana.
 
Bahati nzuri nina kumbukumbu nzuri!! Nahisi Zitto na Lissu hawakuwepo!!. Rais na naibu spika waajifanya wanamjua Mungu kila siku kanisani lakini nao ni muhimili wa uovu.Naibu spika alizuia kuitwa Makonda Chenge akaruhusu!!!.Ndugai aliwahi kuwaambia serikali kuwa upuuzi wao huo ubaki hukohuko serikalini na escrow lazima ijadiliwe!! mawakili wa escrow walienda mahakamani kuzuia.Naomba Mungu pamoja kwamba joka la makengeza nalo ni hatari lakini siku ambayo atakuwa mwenyekiti najua hoja hii itajadiliwa na wabunge watafunguka.Bila woga wala kuficha matukio yote haya yanaratibiwa kwa mukulu.Sisi Tanganyika hatukumwaga damu! haya mabo ya kuiga rwanda yatakuponza mukulu!!!!:(:mad::(;)
 
Mwanaharisi lilifungiwa pale lilipotaja muhusika wa utekaji wa Ulimboka na kuwa hao jamaa walihusika hata sasa hivi hao ndio wanahusika ukianza kuangalia wale walioenda mawingu na yule jamaa aliemtishia Nape kumbukeni siraha zipo nyingi mtaani mambo mnayoyafanya watu wakichoka hakuna alie salama na jinsi tulivyo chini kwenye uchunguzi tutabaki kuhisi tuu...
 
Si ujielekeze kuchambua na kujadili kilichoandikwa badala ya vitisho? Sasa vitisho vya nini? Ninawasikitikia waliokutuma uje kuwatetea humu JF. Unaruhusiwa kunitaja na usikishindwa kufanya hivyo basi ninapendekeza moderator akufungie kwa mwaka mmoja, had Aprili 9 2018!
Go ahead and tell the moderator
 
Hii hutokea duniani kwa serikali ambayo haijiamini na yenye udhaifu mkubwa, lengo ni kujenga woga kwa watawaliwa. Ila ni mkheri kufa ukiwa umesimama kuliko kuishi ukiwa umepiga magoti.
 
Tatizo wengi TISS wapo kwa migongo ya wazazi na ndugu, hawawezi kufanya kazi kwa weledi, ndio maana taasisi imekuwa genge.
 
Unapoona mtekwaji ameongozana na mmoja wa watu walio karibu na watuhumiwa wa matukio ya utekaji... huhitaji sana kufikiria kuwa "upishi" umeshafanyika!!

Kuna "watu" wasahaulifu sana! Wale wanaosahau kuwa "mtu" alitoa bastola hadharani na vyombo vya usalama vikiwepo havikuchukua hatua na mwisho wa siku waziri mwenye dhamana akadai "mtu yule hajulikani na wala si askari!"

Mh. Bashe anapodai na kuelezea khofu yake pakatokea mtu kupinga na kutoa maelezo ya kisiasa badala ya kufikiria kauli kama "... hili ni jambo la kawaida!!!" nadhani yale maneno ya Mbunge wa Mtambwe yanajikamilisha watanzania tunahitaji daktari tupimwe akili aisee!!!
 
Mnakumbuka enzi ya Rais Moi na Nyayo House jumba la kutesea watu.
 
Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe, ameomba mwongozo kuahirishwa kwa Bunge ili kutoa nafasi ya Wabunge wote kujadili matukio ya utekaji watu yanayoendelea.

Akiomba Mwongozo kwa Naibu Spika, Hussein Bashe amedai kuwa amefahamishwa na baadhi ya Mawaziri kuwa ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa kuna kikundi ambacho kinahusika na utekaji wa watu. Amedai kuwa kuna Wabunge 11 wapo kwenye orodha ya kutekwa na kuondolewa uhai. Mimi ni kati ya watu 11 tuliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya popote pale nijiangalie

"Kuna watu wamenitumia ujumbe kwamba mimi ni kati ya watu 11 tuliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya popote pale nijiangalie. Hatuwezi kulifumbia macho jambo hili, Watanzania wanatekwa na watu wasiojulikana".



Kwa hapa tulipofika, ni wazi kuwa JPM ajitafakari na baadhi ya watu wanaomzunguka.Kuna hali ya tahayari katika Taifa.

Jana nimeongea na Askofu mmoja wa Kikatoliki, nimeona dalili ya uhusiano wa JPM na Kanisa kudorora kwa namna anavyoendesha mambo ya Nchi.

Hatuwezi kulifumbia macho jambo hili, Watanzania wanatekwa na watu wasiojulikana'

Wasalaam


Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe, ameomba mwongozo kuahirishwa kwa Bunge ili kutoa nafasi ya Wabunge wote kujadili matukio ya utekaji watu yanayoendelea.

Akiomba Mwongozo kwa Naibu Spika, Hussein Bashe amedai kuwa amefahamishwa na baadhi ya Mawaziri kuwa ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa kuna kikundi ambacho kinahusika na utekaji wa watu. Amedai kuwa kuna Wabunge 11 wapo kwenye orodha ya kutekwa na kuondolewa uhai. Mimi ni kati ya watu 11 tuliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya popote pale nijiangalie

"Kuna watu wamenitumia ujumbe kwamba mimi ni kati ya watu 11 tuliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya popote pale nijiangalie. Hatuwezi kulifumbia macho jambo hili, Watanzania wanatekwa na watu wasiojulikana".



Kwa hapa tulipofika, ni wazi kuwa JPM ajitafakari na baadhi ya watu wanaomzunguka.Kuna hali ya tahayari katika Taifa.

Jana nimeongea na Askofu mmoja wa Kikatoliki, nimeona dalili ya uhusiano wa JPM na Kanisa kudorora kwa namna anavyoendesha mambo ya Nchi.

Hatuwezi kulifumbia macho jambo hili, Watanzania wanatekwa na watu wasiojulikana'

Wasalaam
 
Huyu Bashe anajistukia tu, kwanini asijilipue kabsa kwa kutaja wahusika maana anajijua kabsa hayupo CCM tokea kipindi kile lowassa amekatwa hivyo nafsi yake haina amani kabsa kuendelea kuwepo CCM ila tu anajilazimisha, kujilazimisha huko kuna mkuta anazungumza mambo ya ajabu kabsa ya kumchafua Rais. Chunguzeni kwanini wale team Lowassa wote kama bashe,msukuma,malima ndio wapiga kelele kila siku? Kwanini Wao tu?

Hivi usalama gani wa taifa ukawa na kikundi cha utekaji na tena utekaji wa kipuuzi kabsa kama tunaouona sasa? System ikitaka kukuua inakuondoa tu haisubiri kukuteka.

Hizi ni chuki tu za baadhi wa wabaya wa Magufuli maana kama kuyabana majizi ni kweli kayabana kwa hiyo tusitegemee mteremko kwa Magufuli hata siku moja.Watu wenye pesa chafu watahonga sana hawa whistleblower kumchafua Magufuli.

Watamsingizia mengi mno huyu mzee na ndio kwanza picha inaanza.
kuna MAJITU MENGINE HUMU wao chuki zao ni mbele tu HATA KWENYE UWONGO YANAKUBALI TU.....utasikia mtu anasema ETI MAGUFULI nchi imemshinda....SASA hao ambao nchi haikuwashinda walitufikisha wapi???mbna still mlikuwa mna piga kelele???
Afadhali ya huyu amabaye mnasema nchi imemshinda lakini pesa za walipa kodi zipo salama si kwenye mikono ya wachache.......
ACHA TU atunyooshe HII MIAKA 10 AKILI ZIKAE vizuri kichwani......THEN 2025 tutaamua je tunataka RAIS aina ya KIKWETE au MAGUFULI.....tutajaji hili kupitia MAHALI alipotufikisha JPM na mahali alipotuacha JK......
Naona umetoa povu ulichokiandika ni nonsense
 
Wakati waungwana wanapigania haki mtu kujiweka migongoni mwao kutafuta umaarufu ni upungufu wa uzalendo wa kiwango cha 5G!...Basheee usiwe mfano wa Bashiite katika hili!!...Acha kupiga mayowe chumbani mlango ukiwa wazi kutoka hutaki!!!
 
Mara nyingi huwa tunaelekeza hisia zetu na kupinga jambo moja kwa moja bila kutafuta ukweli!
Kwani ni uongo bashe hakukamatwa wakati wa mkutano mkuu wakiwa na msukuma?
Je hayo matukio kwasasa hayapo?
Je, bashe kuzungumza ukweli ameanza jana au leo?
Anyway nisikupangie cha kupost!!
 
Anakuambia ana pambana humo humo ndani ili hali INAJULIKANA KABSA anae mpigania YUPO CHADEMA.....ngoja tumtumbue sisi wenyewe.......NI SUALA MUDA TU
Hatukatai mtu kusema ukweli pale panapostahili.....LAKINI USIME UKWELI KWA AJILI YA KUMNUFAISHA MTU ALIYE NJE YA SYSTEM ULIYO WEWE au KUJINUFAISHA WEWE MWENYEWE.....hiki ndicho anachofanya BASHE
 
May
Mara nyingi huwa tunaelekeza hisia zetu na kupinga jambo moja kwa moja bila kutafuta ukweli!
Kwani ni uongo bashe hakukamatwa wakati wa mkutano mkuu wakiwa na msukuma?
Je hayo matukio kwasasa hayapo?
Je, bashe kuzungumza ukweli ameanza jana au leo?
Anyway nisikupangie cha kupost!!
Mayowe chumbani kuwa unapigwa huku watu wanaona bado uko huru kuondokana na wanaokupiga mlango ukiwa wazi??...Kweli??
 
Back
Top Bottom