BADO MMOJA
JF-Expert Member
- Jul 19, 2012
- 2,196
- 1,339
Sasa kama mnajua hivyo mnapiga kelele za nini sasa tulieni dozi iingie.Hebu ngoja nikuulize swali dogo tu.
Nape aliunda Tume ya kuchunguza tukio la kuvamiwa kwa Clouds Media na matokeo ya Tume hiyo akaahidi kuwa ataikabidhi kwa Rais.
Unajua nini kilimtokea Nape?
Alifukuzwa kazi kabla hata hiyo ripoti haijafika mezani kwa Rais!
Mbunge Nape alitishiwa kwa bastola pale Protea Hotel ili asiongee na waandishi wa habari, tunakumbuka jinsi Waziri wa mambo ya ndani alivyomuagiza IGP Mangu kuwa mtu yule aliyemtishia kwa bastola Nape akamatwe na afikishwe kwenye vyombo vya sheria.
Wote tunajua kuwa hadi leo huyo IGP wetu hajathubitu kumtia mbaroni yule jamaa aliyemtolea bastola Nape!
Sasa wewe unapomshauri Bashe aripoti tukio la kutishiwa kwake Polisi ni kuwa hujajua kuwa 'Bashite Forces' ni UNTOUCHBLES na haliguswi na chombo chochote cha dola hapa nchini!