Bashe kilimo sio makaratasi, acha kuitumia BBT kuwapotezea muda vijana, ajenda yako hasa ni ipi?

Mganguzi

JF-Expert Member
Aug 3, 2022
1,032
2,769
Mradi huu ni maono ya waziri Hussein Bashe, unaongozwa kwa mahesabu makali sana, tulijua kundi la kwanza litakaa field miezi miwili au mitatu kisha wagawiwe mashamba yao kama walivyokuwa wameahidiwa ili waende wakayasimamie wenyewe lakini mpaka sasa wamewashikilia na kuwaweka pamoja huu ni mwaka sasa unakaribia kuisha hakuna vijana wengine waliochukuliwa zaidi ya walewale.

Mambo yamekuwa mengi sasa wamekuja na mpya kwamba hawa vijana lazima wapitie JKT, du Bashe bwana, huko shambani kuna vita? Nilijua watawezeshwa kwa kupewa mikopo ya matrekta ili kila aende akafanye uzalishaji kwenye maeneo yao na kwenda kufundisha wengine.

Nilijua watakopeshwa mitaji ya kuwawezesha kununua vitendea kazi vitavyowafanya kulima kwa ubora zaidi naona sasa wapo JKT, mara mashamba darasa, nk. Ni lini watapewa mikopo waende wanaendesha kilimo mlichowafunza kila mtu kwa kujisimamia mwenyewe? Mtawaatamia mpaka lini?

Mtawagawia lini mashamba yao na kuwaacha huru walime kwa manufaa yao? Kila darasa lina mwisho vipi hii basheagriculture haina uhitimu ili waanze wengine? Haya sawa
 
Mradi huu ni maono ya waziri Hussein Bashe, unaongozwa kwa mahesabu makali sana, tulijua kundi la kwanza litakaa field manufaa yao? Kila darasa lina mwisho vipi hii basheagriculture haina uhitimu ili waanze wengine? Haya sawa
Wakulima wenyewe tupo Ruvuma, Rukwa .wao wanachukuwa vijana wa Dar tena wa mason wanawapeleka Israel.mimi mkulima na napenda kilimo wameniacha.nashauri week kwenye mikoa inayolima waanzishe huo mradi.
 
Siasa Ni Kilimo
Kilimo Cha Kufa Na Kupona
Kilimo Ni Uti Wa Mgongo
Kilimo Kwanza
BBT







Na Bado...................

tz ni nchi ya wasaka fursa hasa viongozi wanakuja na viproject uchwara wanapiga pesa wanapita hivi,hakuna mwanasiasa aliye tayari kuikwamua hii nchi kutoka kwenye umasikini kwambali ni nyerere na jpm hao walio baki ni wahuni kama wahuni wengine.

Hakika ccm ni chama chakavu.
 
Bashe ni wetu katila imani acha wasogeze siku sababu awamuu ni yao......hata ikibuma huguswiii....angalia mwingine yupo humu anashinda kutukana watu kisa Hamas eti Waziri kweli? Aibu lakini hagusikiii.....mwenzetu katika imanii
 
hivi ile kaulimbiu ya kilimo kwanza iliishia wapi? Serikali inge deal na wakulima hasa walioko mashambani wana struggle watoke kimaisha kuliko hizi BBT zilizowalenga vijana ambao hata kulima bustani ya mboga hawajui
Mkuu Hawa wanaanzisha hizi kwa lengo la kupata fedha wakishapata fedha wapita nazo ndo mwisho wa hio kauli mbiyu hata hi BBT nadhani ndo inakwenda mwishoni mwisho labda Mungu aingilie kati
 
Sehemu yake ya Upigaji yeye na Bibi Tozo. Wamejimilikisha Mashamba Kule Ruahambuyuni Kilolo Iringa pamoja na Bibi Tozo. Wanapiga kwenye Mbolea pitia So Called Ruzuku huku hawalipi Mawakala na Makampuni hadi tumeachishwa kazi One Acre Tanzania Ltd na watoto wetu wanalala njaa tokana na Kampuni Kukosa pesa kwani wanadai pesa nyingi sana walizosambaza Mbolea kwa Ruzuku alafu jamaa hawajatulipa.

Juzi walileta kakijana kamoja toka huko Iringa huku kwetu Njombe eti kametoka BBT na wamekapa tender na kameingia Mkataba na Wizara kauze miche ya Parachichi 22,000,000 kwa mikoa ya Njombe na Huko Iringa huku uwezo wake wa kuzalisha ni miche 1.2M kwa Mwaka. Mradi wa Kijinga kabisa wa Bashe huu. Atatua ajira za vijana wa hapa Njombe wanaozalisha miche ya Parachichi. Yeye hajali kwa kuwa kwao ni Somalia.

Bashe ana upigaji mwingi sana. Yeye ndio Punda wa Mama kwenye Kilimo. Mtapiga kelele ila Mama hasikii. Na kana majungu sana. Usipompa ushirikiano lwenye upigaji kama wewe ni Katibu Mkuu au ED au DG wa Shirika.ndani ya Wizara ya Kilimo ujue umeliwa kichwa. Muulize Dr. Ngailo wa TFRA.

Kusanyeni pesa tu za uchaguzi huku sisi watanzania tukiendelea kuwa maskini.
 
Aliyefuta agriculture mashuleni ilibidi apigwe risasi Moja ya kichwa au anyongwe juu ya mbuyu ! eti baada ya bibitii watu warudi kutoa Elimu Kwa wananchi! Huku SoMo muhimu mmelifuta na mnajua 75% ya watz hutegemea kilimo!
 
Mradi huu ni maono ya waziri Hussein Bashe, unaongozwa kwa mahesabu makali sana, tulijua kundi la kwanza litakaa field miezi miwili au mitatu kisha wagawiwe mashamba yao kama walivyokuwa wameahidiwa ili waende wakayasimamie wenyewe lakini mpaka sasa wamewashikilia na kuwaweka pamoja huu ni mwaka sasa unakaribia kuisha hakuna vijana wengine waliochukuliwa zaidi ya walewale.

Mambo yamekuwa mengi sasa wamekuja na mpya kwamba hawa vijana lazima wapitie JKT, du Bashe bwana, huko shambani kuna vita? Nilijua watawezeshwa kwa kupewa mikopo ya matrekta ili kila aende akafanye uzalishaji kwenye maeneo yao na kwenda kufundisha wengine.

Nilijua watakopeshwa mitaji ya kuwawezesha kununua vitendea kazi vitavyowafanya kulima kwa ubora zaidi naona sasa wapo JKT, mara mashamba darasa, nk. Ni lini watapewa mikopo waende wanaendesha kilimo mlichowafunza kila mtu kwa kujisimamia mwenyewe? Mtawaatamia mpaka lini?

Mtawagawia lini mashamba yao na kuwaacha huru walime kwa manufaa yao? Kila darasa lina mwisho vipi hii basheagriculture haina uhitimu ili waanze wengine? Haya sawa
Ccm inafanya siasa kwenye kila kitu.
 
Back
Top Bottom