Barua ya livingstone yapatikana

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,159
10,869
Hatimaye barua halisi ya mmishionari David Livingstone imepatikana tena huku London kwenye mnada mmoja miaka 140 tangu aiandike barua hiyo katika hali ya kukata tamaa.
Alimuandikia rafiki yake Horace Waller akisema ."I am terribly knocked up but this is for your own eye only," "Doubtful if I live to see you again." .Alisoma biblia na kusoma mpaka akaanza kuchanganyikiwa bila dalili yoyote ya kuondokana na kukata kwake tamaa.`Katika hali hiyo aliyokuwa nayo ilibidi aombe msaada kutoka kwa waislamu wanaoitwa wafanyabiashara ya utumwa.Alisaidiwa sana na Tippu Tipu kwa kila hali.
Maandishi yake hayo, kulingana na bibi Debbie Harrison, mtafiti katika chuo kikuu cha Birkbeck University cha London yanamfanya atiliwe shaka katika ushujaa aliotajwa nao.Mwaka 1871 mmishionari huyu alikwama kwenye kijiji cha Bambarre huko Kongo na hatimaye kufariki huko Chitambo katika Zambia ya leo mwaka 1873.
David Livingstone letter deciphered at last - Yahoo! News
 
Wewe Anyisile hizo chuki zako zitakupa pressure. Sasa hiyo elimu ya madrassa vina uhusiano gani na kumsaidia Livingstone au hiyo barua yake aliyoandika?
 
Alimuandikia rafiki yake Horace Waller akisema ."I am terribly knocked up but this is for your own eye only," "Doubtful if I live to see you again." .Alisoma biblia na kusoma mpaka akaanza kuchanganyikiwa bila dalili yoyote ya kuondokana na kukata kwake tamaa.[/url]

Sijaona bado unataka kusema nini unamuonea huruma au?????????? Nenda muesum za Bagamoyo na Ujiji. Kilichofuata baada ya biashara ya utumwa ni kama biashara hiyo hiyo hiyo lakini kwa utaratibu mwingine.
 
Jaribuni kusoma autobiography ya Tippu Tip muone kama alikuwa anafanya biashara ya utumwa au ya pembe za ndovu?

Yeye alikuwa akifanya biashara ya pembe za ndovu, shanga, vitambaa na vitu vyengine ambavyo vilikuwa na thamani kwa wakati ule. Alikuwa akichukuwa biashara hizo kutoka kwa wahindi Zanzibar na kupeleka huko mabara mpaka Congo na (enzi zile) Ruanda - Urundi.

Sikuona kwenye kitabu chake akiandika habari ya kuuza watumwa ijapokuwa aliwataja akina Livingstone na Stanley na Wabelgiji wa kipindi kile.
 
Bimkongwe, heshima yako ndugu yangu. Japo kuwa Tipp Tipu hakuuza watumwa ( Labda; sina uhakika kuhusu hili) Wachukuzi wa mizigo yake walikuwa kaka zetu weusi, sasa sijui kama waliajiriwa na Tipp Tipu au walikuwa watumwa au manamba au vip[i. Kwa hali yoyote ile wale wachukuzi walinyanyasika na kuumia vibaya sana hebu fikiria kubeba pembe ya ndovu toka kigoma kwenda pwani ya Tanzania, na hatimaye kwenda kuyapakua unguja au uarabuni. Sijafika uarabuni, bali naambiwa kuwa kuna watu wengi tu weusi kama sisi na nywele zao kipilipili, nadhani hawa ni masalia ya wapagazi hao masikini.

Nakubaliana na wewe kuwa sio kila kitu kichambuliwe kwa mtazamo wa kidini, na kwa kweli sikuona sababu ya mwanzisha mada kuandika kuwa alisaidiwa na waisilamu
 
Hatimaye barua halisi ya mmishionari David Livingstone imepatikana tena huku London kwenye mnada mmoja miaka 140 tangu aiandike barua hiyo katika hali ya kukata tamaa.
Alimuandikia rafiki yake Horace Waller akisema ."I am terribly knocked up but this is for your own eye only," "Doubtful if I live to see you again." .Alisoma biblia na kusoma mpaka akaanza kuchanganyikiwa bila dalili yoyote ya kuondokana na kukata kwake tamaa.`Katika hali hiyo aliyokuwa nayo ilibidi aombe msaada kutoka kwa waislamu wanaoitwa wafanyabiashara ya utumwa.Alisaidiwa sana na Tippu Tipu kwa kila hali.
Maandishi yake hayo, kulingana na bibi Debbie Harrison, mtafiti katika chuo kikuu cha Birkbeck University cha London yanamfanya atiliwe shaka katika ushujaa aliotajwa nao.Mwaka 1871 mmishionari huyu alikwama kwenye kijiji cha Bambarre huko Kongo na hatimaye kufariki huko Chitambo katika Zambia ya leo mwaka 1873.
David Livingstone letter deciphered at last - Yahoo! News

This is what we read from this article..

Adding insult to injury, Livingstone, a crusading abolitionist, had been forced to seek help from Arab slave traders while he waited for outside support

Labda mueke source za hizo habari za Tip Tip kutokufanya biashara ya utumwa, ilhali hiyo nickname inasemekana alipewa kufuatia ukatili wake na mlio wa bunduki yake.

Just enlight us please..
 
Sijaona bado unataka kusema nini unamuonea huruma au?????????? Nenda muesum za Bagamoyo na Ujiji. Kilichofuata baada ya biashara ya utumwa ni kama biashara hiyo hiyo hiyo lakini kwa utaratibu mwingine.

Hapa ninachotaka uelewe kwanza ni kuwa uislamu ulitangulia kwa mbali kufika Afrika mpaka ndani Kongo.Wakati mara nyingi kuna dharau kwa waislamu na hujuma za kila aina kumbe wakristo wa mwanzo Afrika walifikia mikononi mwa waislamu.Nyinyi hamna shukrani kabisa!.
Kuhusu mada ya biashara ya utumwa humu imejadiliwa mara nyingi lakini nakuhakikishia walion'gang'ania uzushi unaouamini wewe walishindwa na kukimbia.Zamani mwaka 2008 na karibuni kabisa.Kabla hujaamua kuendeleza ubishi wako angalia kule https://www.jamiiforums.com/habari-...abu-wenye-asili-ya-kiafrika-6.html#post934898
 
Hapa ninachotaka uelewe kwanza ni kuwa uislamu ulitangulia kwa mbali kufika Afrika mpaka ndani Kongo.Wakati mara nyingi kuna dharau kwa waislamu na hujuma za kila aina kumbe wakristo wa mwanzo Afrika walifikia mikononi mwa waislamu.Nyinyi hamna shukrani kabisa!.
Kuhusu mada ya biashara ya utumwa humu imejadiliwa mara nyingi lakini nakuhakikishia walion'gang'ania uzushi unaouamini wewe walishindwa na kukimbia.Zamani mwaka 2008 na karibuni kabisa.Kabla hujaamua kuendeleza ubishi wako angalia kule https://www.jamiiforums.com/habari-...abu-wenye-asili-ya-kiafrika-6.html#post934898

Wewe bana acha kutetea ujinga.

Unaonekana hata hukusoma hiyo article ulioileta.

Article inasema Livingstone alienda kutafuta msaada kwa Waarabu walokuwa wakifanya biashara za utumwa (yaani kuuza watu kama kuku) ingawa yeye (Livingstone) alikuwa abolitionist. Hii haijustify chochote kwa waarabu wale na biashara zao za kishenzi.
 
Lunanilo na Abdulhalim, source ya kitabu ni "Maisha ya Hamed bin Muhammed El Murjebi - Tippu Tip, kwa maneno yake mwenyewe (1959), kimefasiriwa kwa kiingereza na W. H. Whitley

Ni kweli wabeba mizigo walikuwa ni weusi, lakini hiyo ilikuwa kwa kupatana kwa majora ya vitambaa na shanga. Na wengine walikuwa wanakimbia wakiona kazi nzito ijapokuwa walikuwa wameshapewa malipo. Kwa hivyo yalikuwa mapatano ya kibiashara ingawa sisemi kwamba yalikuwa mapatano ya kihalali au la.

Na ni kweli walikuwa wanapigana na bunduki mpaka akapata jina la Tippu Tip, na kwa enzi zile ilikuwa "ua nikuue", yaani mule wanamopita na misafara yao walikuwa wanapigana na wenyeji na wao kupigwa na hata kunyang'anywa hizo biashara.

Vile vile hata hao wazungu waliokuwa wanakwenda huko ndani Tanganyika walikuwa wanachukuwa wapagazi hao hao weusi, unadhani wengine wangetoka wapi? Angalia kitabu cha "Safari za Mwinyi Mtoro" ambacho nilikipata humu humu na kukidownload na kukisoma. Mjerumani Von Weissman alichukuwa wapagazi kutoka Zanzibar, Bagamoyo na sehemu nyengine, na wengine aliwachukuwa kutoka Comoro. Na hao akina Livingstone pia walichukuwa wapagazi kutoka Bagamoyo na maeneo ambayo alikuwa anapita. Na maiti yake ilibebwa na "Susi na Chuma" kutoka Kigoma mpaka Zanzibar na sio mtu mweupe.
 
Bitimkongwe,

Hicho kitabu cha Tip tip kiliandikwa na nani mpaka huyu mzungu (I presume) kuja kukitafsiri?
 
Hiyo ni "autobiography", yaani aliandika mwenyewe Tippu Tip. Kiswahili chake kwa kweli ni kile chenye asili ya kiarabu na kwa sasa wengi wanaweza wasielewe baadhi ya maneno. Ila ile version ya Kiingereza (ya Whitley) ndio rahisi kusomeka.

Kitabu chenyewe page moja ni kwa maneno yake na opposite page ndio iko kwa kiingereza.
 
Wewe Anyisile hizo chuki zako zitakupa pressure. Sasa hiyo elimu ya madrassa vina uhusiano gani na kumsaidia Livingstone au hiyo barua yake aliyoandika?
usiwe mwepesi wa kuhamaki, harafu mgumua kufikiri, kama usingelikuwa na pupa ungelijua kwanini nimesema tatizo la ilimu madrassa, usikurupuke tu kupost ishu juu ya ulikisoma hata kama hujakielewa. pole lakini kama umekwazwa na hiyo, tafuta elimu na ilimu
 
Bimkongwe, heshima yako ndugu yangu. Japo kuwa Tipp Tipu hakuuza watumwa ( Labda; sina uhakika kuhusu hili) Wachukuzi wa mizigo yake walikuwa kaka zetu weusi, sasa sijui kama waliajiriwa na Tipp Tipu au walikuwa watumwa au manamba au vip[i. Kwa hali yoyote ile wale wachukuzi walinyanyasika na kuumia vibaya sana hebu fikiria kubeba pembe ya ndovu toka kigoma kwenda pwani ya Tanzania, na hatimaye kwenda kuyapakua unguja au uarabuni. Sijafika uarabuni, bali naambiwa kuwa kuna watu wengi tu weusi kama sisi na nywele zao kipilipili, nadhani hawa ni masalia ya wapagazi hao masikini.

Nakubaliana na wewe kuwa sio kila kitu kichambuliwe kwa mtazamo wa kidini, na kwa kweli sikuona sababu ya mwanzisha mada kuandika kuwa alisaidiwa na waisilamu
uko sahihi mkuu kuna eneo moja pale Oman linaitwa Zanzibar, na warabu wa pale ni warabu weusi kama waha kabisa, na uarabu wao ni kwa ajili wamezaliwa pale tangu zama, kwa hiyo ni kweli kabisa kuwa hawa ni masalia ya wale waafrika wa kipindi hicho cha utumwa wakajikuta wako settled maeneo yale na kupaita Zanzibar
 
Bitimkongwe,

Hicho kitabu cha Tip tip kiliandikwa na nani mpaka huyu mzungu (I presume) kuja kukitafsiri?
Soma kipande kimoja cha maelezo ya Tippu Tip.Ikiwa kuna sehemu hujaelewa nitakusaidia.Ukipenda nitakuletea vipande zaidi.


╞ Nalipopata miaka thenashara ,nalishika safari za karibu.Hafanya biashara ya sandarusi pamoja na ndugu yangu Muhammed bin Masud el Wardi na mjomba wangu Bushiri bin Habib wa Abdallah bin Habib el Wardijan.Nachukua bidhaa kidogo,maana kijana.Nao wao ndugu yangu na wajomba wangu wakichukuwa bidhaa nyingi kidogo.Hafanza biashara ya sandarusi mwaka mmoja╡ (12)
 
Soma kipande kimoja cha maelezo ya Tippu Tip.Ikiwa kuna sehemu hujaelewa nitakusaidia.Ukipenda nitakuletea vipande zaidi.
hiki nini sasa?

╞ Nalipopata miaka thenashara ,nalishika safari za karibu.Hafanya biashara ya sandarusi pamoja na ndugu yangu Muhammed bin Masud el Wardi na mjomba wangu Bushiri bin Habib wa Abdallah bin Habib el Wardijan.Nachukua bidhaa kidogo,maana kijana.Nao wao ndugu yangu na wajomba wangu wakichukuwa bidhaa nyingi kidogo.Hafanza biashara ya sandarusi mwaka mmoja╡ (12)

haya yatamfanya mtu aelewe nini, ama ni mafumbo tu?
 
Soma kipande kimoja cha maelezo ya Tippu Tip.Ikiwa kuna sehemu hujaelewa nitakusaidia.Ukipenda nitakuletea vipande zaidi.


╞ Nalipopata miaka thenashara ,nalishika safari za karibu.Hafanya biashara ya sandarusi pamoja na ndugu yangu Muhammed bin Masud el Wardi na mjomba wangu Bushiri bin Habib wa Abdallah bin Habib el Wardijan.Nachukua bidhaa kidogo,maana kijana.Nao wao ndugu yangu na wajomba wangu wakichukuwa bidhaa nyingi kidogo.Hafanza biashara ya sandarusi mwaka mmoja╡ (12)

....and HOW ON EARTH hii inajibu swali langu???

Kama huelewi posts zangu tafwadhaal zione kama kituo cha polisi.
 
....and HOW ON EARTH hii inajibu swali langu???

Kama huelewi posts zangu tafwadhaal zione kama kituo cha polisi.
Hili jibu la nani aliandika autobiography ya Tippu Tip lilikwishajibiwa na BintMkongwe hapo juu.Baina ya post yake na yako ni 4posts.Kama wewe ni mtu madhubuti usingepaswa kunijibu mimi tena wala kuniuliza wala kushangaa kwamba hujajibiwa.
Wasioelewa post zako humu JF sio mimi peke yangu.Nimeona mara nyingi ukibezwa bezwa.Na kwa kweli hueleweki ndio maana ikawa hivyo.Mimi post zako huwa naziona kama jalala sio kituo cha polisi tu, na huwa nazikwepa kuzijibu.Lakini pale niliona kidogo labda umeuliza cha maana na ukijibiwa utaelewa imekuwa yale yale.
Kwenye hii mada post no.7 umesema."Labda mueke source za hizo habari za Tip Tip kutokufanya biashara ya utumwa, ilhali hiyo nickname inasemekana alipewa kufuatia ukatili wake na mlio wa bunduki yake."
Kwani mlio wa bunduki ya Tip tip ndio ushahidi kuwa yeye alifanya biashara ya utumwa?.Wewe Abdulhalim tukisikia unalia kwani lazima iwe umefiwa.Yawezekana umezomewa tu kwa upuuzi wako.
 
Nakubaliana na wewe kuwa sio kila kitu kichambuliwe kwa mtazamo wa kidini, na kwa kweli sikuona sababu ya mwanzisha mada kuandika kuwa alisaidiwa na waisilamu
Ni rahisi. Nadhani mleta hoja alikusudiwa kwamba ingawa Livingstone ambaye alikuwa mkristo alitegemewa kusaidiwa na waumini wenzake, alijikuta msaada wa maana anaupata kutoka kwa wenye imani tofauti na yake. Labda hilo linatufundisha kwamba tangu kale haukuwapo ubaguzi kama huu tunaoujenga kwa bidii zama hizi kidini. Mwenye akili na alielewe jambo hili kwa kina na kumsaidia. Kwa misingi hiyo ndio maana waisla na wakristo wanakaa mtaa mmoja majirani na hata kupanga nyumba moja wakisaidianaa kwa kila hali. Sasa wanaoshabikia udini wa kutugawanya wasitupotoshe kumbe hata mamisionari hawakulenga kutugawanya. Tippu Tip aliliona hilo, naye aliangalia maslahi na sio imani zisizo na tija. Ama sivyo angemfanya Livingston adui nambari moja kwa kukataza utumwa. Japo unanifumbua macho leo kwamba Tippu Tip hakuuza watumwa, that is likely kwa sababu aliwatumia watumwa kama malori ya kusomba mizigo yake na sio kama bidhaa.
 
Ni rahisi. Nadhani mleta hoja alikusudiwa kwamba ingawa Livingstone ambaye alikuwa mkristo alitegemewa kusaidiwa na waumini wenzake, alijikuta msaada wa maana anaupata kutoka kwa wenye imani tofauti na yake. Labda hilo linatufundisha kwamba tangu kale haukuwapo ubaguzi kama huu tunaoujenga kwa bidii zama hizi kidini. Mwenye akili na alielewe jambo hili kwa kina na kumsaidia. Kwa misingi hiyo ndio maana waisla na wakristo wanakaa mtaa mmoja majirani na hata kupanga nyumba moja wakisaidianaa kwa kila hali. Sasa wanaoshabikia udini wa kutugawanya wasitupotoshe kumbe hata mamisionari hawakulenga kutugawanya. Tippu Tip aliliona hilo, naye aliangalia maslahi na sio imani zisizo na tija. Ama sivyo angemfanya Livingston adui nambari moja kwa kukataza utumwa. Japo unanifumbua macho leo kwamba Tippu Tip hakuuza watumwa, that is likely kwa sababu aliwatumia watumwa kama malori ya kusomba mizigo yake na sio kama bidhaa.
Kwa kweli hakuwatumia kama malori ya kusomba mizigo,bali aliwalipa kwa kupatana nao.Na wengi walikuwa wakibeba masafa maalum na kurudi makwao kutumia pesa zao.
 
Back
Top Bottom