Barua ya Kumfukuza Juliana Shonza na aibu kwa BAVICHA

Ndugu yangu George J Minja,

Awali ya yote nikupe pole kwani ingawa umejaribu kumpaka matope kishkaji Shonza na kuanza kumtuhumu Heche (ambaye hahusiki kabisa na theme ya mada yako); na kutokana na tarehe uliyojiunga hapa JF, inathibitisha kuwa uko kazini kutumika. Bahati mbaya kwako ni kwamba, uwezo na upeo wako kukufanya uwe hapa katika JF, haukidhi matakwa na dhima - yaani kuwa Great Thinker.

1. Barua hiyo haina mapungufu yeyote kama ulivyotaka kupotosha. Shonza amefukuzwa uanachama wa BAVICHA. Tuhuma zilizokuwa zinamkabili zimewekwa wazi katika barua hiyo na hata mtiririko mzima wa mashtaka umewekwa. Maamuzi ya kikao kwa lugha ya kawaida kuitwa 'Maazimio' na katika uandishi tunasema Kikao Kiliazimia (kiliamua) yafuatayo. Kingereza chake ni resolution. Na kwa wale walioko kwenye Taasisi za kufanya kazi, watakumbuka kitu kinachoitwa BOARD RESOLUTION. Hivyo uache kupotosha watu kwa makusudi.

2. Mamlaka halali imekaa na ikafikia maamuzi; na imefanya kulingana na Katiba yake, je kwa nini itafute second opinion? Kama Kamati ingekaa na kuandika 'mapendekezo', then muktasari wa kikao ndiyo ungepelewa ukiwa na mapendekezo kwa authority ya juu ambayo wajibu wake ni aidha kukubaki au kukataa hayo mapendekezo. For this case, kikao hichi halali, kimefanya maamuzi. Wakubwa wamepewa tu taarifa (Rejea Barua, Katibu Mkuu wa CHADEMA anapewa tu taarifa)

3. Ulitaka John Heche aje ajadili kuhusu jina? Katika taarifa ya Shonza alikuwa anatumia majina yote mawili kumwita Heche; hakuna popote alipotoa tuhuma zozote kuhusu hilo jina la pili. Hivyo, kama ni tuhuma ziwekwe wazi, na ushahidi uwekwe then John Heche atakuja kujibu.

Uandishi wa namna hii kama ulivyoufanya wewe na Juliana Shonza, si tu unapoteza hadhi ya JF, bali pia unafanya hapa paonekane kijiwe na majungu, sehemu ya watu ambao hawajasoma, lakini pia tunajenga picha mbaya ya elimu mliyoisoma na vyuo vyenu(tunavionea kutokana na madhambi yenu)

MWISHO
Leo mchana Shonza alilalamika kutokupata barua; wewe umeipata wapi? Umeipataje? Maana kama anajificha haonekani na anafanya vurumai, then haitamsaidia kitu. Halafu hata makazini, kama mwajiri hakutaki na amekufukuza kazi, hauwezi ukang'ang'ania ofisi, badala yake unakimbilia CMA ili haki yako ipatikane. Lakini kama hakutaki, no matter what, atakulipa visenti vyako vya miezi 12, unampisha, anaendelea na maisha yake na wafanyakazi wake wengine ambao ni loyal

Cc Molemo Crashwise Ben Saanane Juliana Shonza Mtela Mwampamba, Mchange & Mwita Maranya

Dah, sasa mbona umemaliza point zote za maana...s wengine tuchangie nini hpgasa??!!
Anyway, asante sana 'kamanda'!
 
Last edited by a moderator:
Kwa kiswahili changu kibovu ninadhani barua iko sahihi,wanadhamiria au wameazimia kumfukuza,na kama Shonza anaona hakutendewa haki kabla ya barua ya kumfukuza haijamkuta anauwezo wa kuomba rufaa ili kesi yake isikilizwe na baraza la juu.

Anachotakiwa Shonza siyo kulalamika kwenye magazeti au majukwaani bali kurudi nyuma na kuomba rufaa ili kesi yake isikilizwe na baraza la juu kabla hawajamfukuza. Mnaweza kunisahihisaha kama nimekwenda kinyume na maana halisi ya ujumbe
Na Tuntemeke aitwe kwenye hicho kikao, maana anatusumbua sana humu JF.
 
Kumbe yahusu kufukuzwa! Sasa umeshindwa kuelewa nini wewe? Uko darasa la ngapi?bila shaka form two A

Umeambiwa mwanzo wa barua kabisa! Yahusu kufukuzwa!

Mimi sio masalia lakini lazima nisema ukweli:

Hii barua ina mapungufu mengi sana na inatia mashaka juu ya uongozi wa BAVICHA.

Kichwa cha habari cha barua hii kinasema KUFUKUZWA UANACHAMA WA BARAZA LA VIJANA WA CHADEMA lakini para ya pili kutoka mwisho inasema BARAZA LIMEAZIMIA KUKUFUKUZA.

Tafsiri yake ni kuwa Baraza halijamfukuza Shonza bali limedhamiria kumfukuza baadae basi muweke hapa barua ya kumfukuza, huu ni UPUUZI, kama hamuwezi kuandika hata barua kwa umakini ni dalili mbaya.

Pili Kikao kimekaa tarehe 5 barua ikatoka tarehe 6 yaani hata hamkuwa na muda wa kuwashirikisha viongozi wenu wa juu kwa maana ya viongozi wakuu wa Chama kuhusu hili ikizingatiwa Shoza ambaye mimi namuona kama kilaza sana na mjinga wa kwanza alikuwa kiongozi mwenzenu wa ngazi ya juu

Jirekebisheni, hii inanipa shaka kubwa na viongozi wa BAVICHA.

Kwanza uwezo wa Juliana Shonza kama Makamu Mwenyekiti ni mdogo sana hakustahili hiyo nafasi na pili Uandishi huu wa Katibu mkuu wa baraza unanipa mashaka na uwezo wake pia

Lakini Tatu na kubwa shutuma za jina halisi la John Heche hazijajibiwa mpaka sasa iku inakaribia kuisha je tumuingize kwenye kundi la kina Mulugo Amim na Mwigulu Nchemba??

attachment.php

attachment.php
 
Mimi sio massalia na wala sio bootleaker kama wewe ,ninasema ukweli ili kuisadida BAVICHA na CHADEMA ambayo wakati tukiianzisha hiyo BAVICHA wengi mnaojifanya wanaBAVICHA hodari hamkuwepo

John Heche ni kiongozi makini sana namuamini na sijasikia hata wakati mmoja akiingia kwenye kashfa,ni mwanasiasa wa kweli mwenye uwezo wa kujenga hoja na kuisimamia,ana dhamira ya kweli na hata ukimwangalia usoni unaona hilo halina ubishi,kuna tofauti kubwa sna kati ya watu kama Mwigulu Nchemba na John Heche

Lakini Juliana Shoza kwenye waraka wake hapa leo amemtaja John Heche kwa jina jingine Sugutu sijui nini na nini,sasa wewe na unaowalamba miguu huko BAVICHA hamjakanusha jambo hili mpaka sasa siku inaisha maana yake ninini

Hilo Sugutu ni jina la Heche la Utotoni??
Au ni jina la Heche la kusomea??
Au ni jina la Heche la kutafutia pesa??
Au John Heche ni jina la mtu lilinunuliwa??
Au sio Mtanzania??

Kuna maswali mengi juu ya hili mngefanya hima kuondoa utata huu mngemsaidia Heche,CHADEMA,BAVICHA na mimi ambaye nilipoteza muda wangu mwingi kuchambua Rasimu ya Kwanza ya BAVICHA na kuwa mmoja wa Vijana wa awali kuichambua na kupitisha mkakati wa kuunda BAVICHA.

Kijana, mimi sio size ya Bavicha hata kidogo, usikosee. Nashukuru kwa maelezo yako mazuri. Nina swali dogo tu kwako, ni tangu lini umelisikia hilo jina jipya la Heche? Na je umefanya juhudi yoyote hata kujaribu kummuliza huyo Juliana amelitoa wapi hilo jina? Hata mimi nimelisikia leo. Kama ujafanya uchunguzi wowote au kufuatilia chanzo cha hilo jina, ni kwa nini unataka kupoteza imani na Heche haraka hivyo?

Tiba
 
Mimi sio massalia na wala sio bootleaker kama wewe ,ninasema ukweli ili kuisadida BAVICHA na CHADEMA ambayo wakati tukiianzisha hiyo BAVICHA wengi mnaojifanya wanaBAVICHA hodari hamkuwepo

John Heche ni kiongozi makini sana namuamini na sijasikia hata wakati mmoja akiingia kwenye kashfa,ni mwanasiasa wa kweli mwenye uwezo wa kujenga hoja na kuisimamia,ana dhamira ya kweli na hata ukimwangalia usoni unaona hilo halina ubishi,kuna tofauti kubwa sna kati ya watu kama Mwigulu Nchemba na John Heche

Lakini Juliana Shoza kwenye waraka wake hapa leo amemtaja John Heche kwa jina jingine Sugutu sijui nini na nini,sasa wewe na unaowalamba miguu huko BAVICHA hamjakanusha jambo hili mpaka sasa siku inaisha maana yake ninini

Hilo Sugutu ni jina la Heche la Utotoni??
Au ni jina la Heche la kusomea??
Au ni jina la Heche la kutafutia pesa??
Au John Heche ni jina la mtu lilinunuliwa??
Au sio Mtanzania??

Kuna maswali mengi juu ya hili mngefanya hima kuondoa utata huu mngemsaidia Heche,CHADEMA,BAVICHA na mimi ambaye nilipoteza muda wangu mwingi kuchambua Rasimu ya Kwanza ya BAVICHA na kuwa mmoja wa Vijana wa awali kuichambua na kupitisha mkakati wa kuunda BAVICHA.

Mimi kama wewe nimesoma ule waraka wa Juliana shonza ila sijaona sehemu alipomtuhumu Heche kuhusu suala la jina lake zaidi ni kwamba alikuwa anayatumia yote kwa pamoja....sasa labda unionyeshe wewe sehemu ambapo Heche ametuhumiwa kuhusu jina mpaka aje hapa kujibu
 
Kijana, mimi sio size ya Bavicha hata kidogo, usikosee. Nashukuru kwa maelezo yako mazuri. Nina swali dogo tu kwako, ni tangu lini umelisikia hilo jina jipya la Heche? Na je umefanya juhudi yoyote hata kujaribu kummuliza huyo Juliana amelitoa wapi hilo jina? Hata mimi nimelisikia leo. Kama ujafanya uchunguzi wowote au kufuatilia chanzo cha hilo jina, ni kwa nini unataka kupoteza imani na Heche haraka hivyo?

Tiba


Umekosea unatakiwa kusema MIMI SIO SIZE YAKO,silingani na wewe kabisa kama kwa akili zako za UDOM unakuja kutafuta size yako hapa hata mimi sio size yako
 
Dada wewe ni mmoja ninaowapenda kwa ujuvi wa kiswahili hapa jamvini,

Japo neno ujuvi unaweza kulinyumbulisha na kutohoa maana tenge, lakini bado waweza kusimamia ukweli wa sarufi za kiswahili maridhawa!

Neno "Kuazimia" kwa haraka ya mswahili wa leo aliyeakisi umagharibi anaweza kulileta kwenye maana moja tu nayo ni KUKUSUDIA.

La hasha hivyo sivyo, bali ni Baraka/amri/kibali/ruhusa itolewayo na kundi la watu kwa mtu ama watu.

Tumia kamusi stahiki ya BAKITA

Narudia tena wewe hujui tofauti ya ujuvi na ujuzi, maana ungejua usingetumia kumwambia mtu unampendea ujuvi wake. Kwa wenye taadhima zao ni matusi.

Maana ya kuazimia, kudhamiria na kukusudia ni moja kwa kamusi mbali ya la BAKITA bali hata la TUKI na Madan pia

Msitee uzembe kwa sababu umefanywa na watu muwashabikiao.

Lingefanywa na CCM hili mngelitetea?

Acheni unazi uso na manufaa
 
kwa kweli haya maubishi ya mtandaoni yanawavua pichu hawa wanasiasa chipukizi mada nyingi wanazoleta zinakupa wasiwasi na iq zao they are very poor in thinking!! yaani most of them hawako critical ni afadhali wakakaa kimya!! inanifanya nione kuwa hata mimi nimewashinda na naogopa wakijagombea sitawapa kura yangu maana ni bora nijiongoze mwenyewe!!
 
Kaka mwanahapa,eti katoa tamko kupitia cheo kipya huko NCCR hujaliona na anaenda tofauti na msimamo wa mwenyekiti wake waliyetaka kumpopoa mawe mtwara cjui kama alimconsult kabla ya hiyo press release! Ana kazi kweli huyo mwanasiasa uchwara Kisandu.


Siasa za kisandu ni siasa za maji taka, Tamko la Kisandu Binafsi lakini hapa JF kuna mtu ameweka uzi kwamba ni tamko la vijana wa NCCR.
 
1.Kutumika
Hii ni dharau na ni tusi,kujiunga kwangu JF tarehe za karibuni hakunifanye niwe Mtumikaji hasa wa Masalia kama unavyosema,wako watu wengi wanaojiunga na JF hata leo kwa nia njema na wala sio wapinzani wa BAVICHA na CHADEMA.Nakuomba ufute kauli yako ya kusema mimi natumika hasa kwa kigezo cha kujiunga JF hivi karibuni kwani hii inawadhalilisha wote wanaojiunga JF baada ya mgogoro wenu ndani ya BAVICHA.

1. Nakulaumu wewe binafsi na si wote waliojiunga JF hivi karibuni. Wala siwezi kufuta kauli yangu.
2. Mgogoro wetu BAVICHA; unajua mimi ni nani?

2.Usomi na Kijiwe cha majungu

Ukisoma kanuni za JF vizuri hakuna mahali popote imeandikwa kuwa hili ni jukwaa la wasomi na kwa taarifa yako Great Thinkers wengi wa leo sio wasomi bali wasomi wengi ndio wapuuzi wanaoharibu mustakabali wa nchi yetu rejea maneno ya Mzee Butiku siku ya kuazimisha miaka 51 ya uhuru pale Nkhrumah Hall.

Mimi ni wapi nimesema JF ni ya 'wasomi' wa darasani? Nimemaanisha JF ni ya watu ambao ni Great Thinkers. Thats all. Sijazungumzia usomi wa darasani. Na hapo Nkurumah siwezi kufika. Sijawahi kufika. Unadhani watu wote huwa tunafika Nkurumah au kufuatilia yanayotokea huko.

3.Utaratibu wa kumfukuza Juliana Shoza

Nakubaliana na wewe bila shaka kuwa mamlaka iliyokaa na kumfukuza Shoza ina baraka za katiba lakini upo utaratibu wa ndani ambao mara zote Utawala Bora unahitaji ufuatwe na hili halikufanyika pamoja na kwamba Shoza alikuwa hana mamlaka juu ya Kamati Tendaji lakini alikuwa Kiongozi wa juu wa Chama ,akitumika katika BAVICHA.hauhitaji katiba kukuueleza jinsi ya kupata ushauri kabla ya maamuzi makubwa.

Nadhani umekaririshwa maana ya Utawala Bora. CHADEMA kama Taasisi, ina ngazi zake (hierarchy of authority). Sasa kama Kamati imekaa ambayo imekuwa mandated kufanya maamuzi iliyoyafanya, sasa irudi tena kwa viongozi iwaombe ushauri? Lets say waliombwa ushauri tarehe 6 asbh na wakaridhiwa, hauoni kuwa ni sawa, kwamba asbh wameomba ushauri, wakaruhusiwa na ndiyo maana wakaendelea na mpango wao huo? Yaani hiyo unayoiita authority ika-cement tu maazimio ya Kamati Tendaji BAVICHA?

4.Lugha iliyotumiwa kwenye barua

Hii ni aibu kubwa kuwa unatetea UJINGA na UPUUZI ule ule ulioufanya kwenye barua ,Kiingereza ni Lugha na ina misamiati yake na wakati mwingine ukiitafsiri kwa kiswahili utapata maana nyingine kabisa,kulikuwa hakuna haja ya kulichukua neno RESOLUTION in Mutatis Mutandis way na kulifanay KUAZIMIA??hivi kweli KUAZIMIA na KUKUFUKUZA n i sawa,kuna shida kubwa hapo lazima ukiri,ilikuwa rahisi na ya kueleweka tuu kama mngeandika TUMEKUFUKUZA na mbona kwenye kicha cha habari hukuandika TUNAAZIMIA??kama ni neno sahihi ungeanza nalo basi kwenye kicha cha habari ungesema TUMEAZIMIA ,hakika isingeleta maana kama isivyoleta maana kwenye para ya nne.

Naamini wewe ni mdogo kwa umri, uko unasoma, tena kwa kukariri ndiyo maana unajenga hoja za kitoto. Nikusaidie kidogo. Kwa sehemu za kufanya kazi ambapo maamuzi mengi yanafanywa kupitia vikao, basi utaratibu uko hivi. Kikao kinafanyika kikiwa na mwenyekiti, katibu na wajumbe. Kunakuwa na agenda, zinajadiliwa, na maelekezo/maamuzi ya kikao yanafikiwa (kulingana na kila linalojadiliwa), maamuzi yanayofikiwa yanaitwa Maazimio. Baada ya Kikao, Katibu anaandika Muhtasari na kulingana na unyeti wa kikao, muhtasari unatoka siku hiyo hiyo au mapema kesho yake. Kikao kinapoisha, yale MAAZIMIO huwa yanachukuliwa na KATIBU kwani ndiyo mfuatiliaji.

Hivyo kikao kile cha Mbezi Garden, kiliazimia mambo mengi lakini jambo kubwa ni KUMFUKUZA UANACHAMA WA BAVICHA SHONZA (na mengineo - rejea press release ya Msemaji wa BAVICHA ambaye ni Mwenyekiti). Hakuna kasoro wala makosa yeyote ya kiuandikishi. Kikao kimeazimia kukufukuza, maana yake ni kuwa kikao mimejadili na kuamua kukufukuza.

Kama haujui mambo, uulize na siyo kukurupuka ili uonekane unajua. Njoo inbox nitakupa elimu ya huku duniani uache kukariri.
 
Mimi nafikiri inabidi tupate wanaojua kiswahili wasitusaidie kutwambia kama neno kuazimia na neno kudhamiria yana maana sawa.

Nikipata ufafanuzi, then nitarudi kuchangia hoja.

Tiba
Nadhani neno la kiingereza ni "resolution" - kitendo ni "resolved to.." ni sawa na na kusema "..amua...". Stand to be corrected.
 
Mimi sio massalia na wala sio bootleaker kama wewe ,ninasema ukweli ili kuisadida BAVICHA na CHADEMA ambayo wakati tukiianzisha hiyo BAVICHA wengi mnaojifanya wanaBAVICHA hodari hamkuwepo

John Heche ni kiongozi makini sana namuamini na sijasikia hata wakati mmoja akiingia kwenye kashfa,ni mwanasiasa wa kweli mwenye uwezo wa kujenga hoja na kuisimamia,ana dhamira ya kweli na hata ukimwangalia usoni unaona hilo halina ubishi,kuna tofauti kubwa sna kati ya watu kama Mwigulu Nchemba na John Heche

Lakini Juliana Shoza kwenye waraka wake hapa leo amemtaja John Heche kwa jina jingine Sugutu sijui nini na nini,sasa wewe na unaowalamba miguu huko BAVICHA hamjakanusha jambo hili mpaka sasa siku inaisha maana yake ninini

Hilo Sugutu ni jina la Heche la Utotoni??
Au ni jina la Heche la kusomea??
Au ni jina la Heche la kutafutia pesa??
Au John Heche ni jina la mtu lilinunuliwa??
Au sio Mtanzania??

Kuna maswali mengi juu ya hili mngefanya hima kuondoa utata huu mngemsaidia Heche,CHADEMA,BAVICHA na mimi ambaye nilipoteza muda wangu mwingi kuchambua Rasimu ya Kwanza ya BAVICHA na kuwa mmoja wa Vijana wa awali kuichambua na kupitisha mkakati wa kuunda BAVICHA.

Haya maswali ungemuuliza Shonza nafikiri angekupatia majibu muafaka, lakini wewe unajaribu kushadadia masalia na kutujazia server bure. Kama huna hoja si ni afadhali ukae kimya tu!!?
 
nimeanza kuwa na mashaka na uwezo wa upinzani hapa Tanzania naona kama shonza na mwenyekiti wake wana uchu wa madaraka watu wa ajabu wanaouaibisha upinzani Tz na "watoto" inawezekanaje viongozi wenye nia moja kufarakana shame to u Shonza na Heche
 
Chakusikitisha katibu wa BAVICHA ndugu Munishi nina mashaka sana na Elimu yake naamini yupo kundi moja na hao wanao PLAGARIZEE vyeti vya watu bila Kutoa ACKNOWLEDGE kwa wahusika na hii inaashiria kuwa wana ubovu wa viongozi katika hichi chama cha UDINI,UKABILA,UKANDA UFEDHULI,UJANGILI WA SIASA NA ASILIMALI ZA TAIFA LETU ..........................CHAMA CHA CHADOMO kimeshindwa kujenga hata ofisi za makao makuu ya chama je watakapoINGIA IKULU Wataigeuza ikulu kuwa Lango la walanguzi.........
 
Kha,chadema mkiambiwa ukweli hasa unaowauma mnakuwa wakali sana,kulikoni? Jibun hoja ila kwakweli BAVICHA mechemka na mmetia aibu!
 
Chakusikitisha katibu wa BAVICHA ndugu Munishi nina mashaka sana na Elimu yake naamini yupo kundi moja na hao wanao PLAGARIZEE vyeti vya watu bila Kutoa ACKNOWLEDGE kwa wahusika na hii inaashiria kuwa wana ubovu wa viongozi katika hichi chama cha UDINI,UKABILA,UKANDA UFEDHULI,UJANGILI WA SIASA NA ASILIMALI ZA TAIFA LETU ..........................CHAMA CHA CHADOMO kimeshindwa kujenga hata ofisi za makao makuu ya chama je watakapoINGIA IKULU Wataigeuza ikulu kuwa Lango la walanguzi.........

Wewe unafurahi kwa sababu Mama yako kajengewa na Wakuu baada ya Kutoa vitu maalumu
 
Narudia tena wewe hujui tofauti ya ujuvi na ujuzi, maana ungejua usingetumia kumwambia mtu unampendea ujuvi wake. Kwa wenye taadhima zao ni matusi.

Maana ya kuazimia, kudhamiria na kukusudia ni moja kwa kamusi mbali ya la BAKITA bali hata la TUKI na Madan pia

Msitee uzembe kwa sababu umefanywa na watu muwashabikiao.

Lingefanywa na CCM hili mngelitetea?

Acheni unazi uso na manufaa

What else can you do apart from this?
Mjuvi mwenye ujuzi wa kutafsiri maneno na kutupilia mbali maana ya kimantiki.
 
Back
Top Bottom