cold water
Senior Member
- Oct 6, 2021
- 175
- 618
Nipo kwenye mahusiano ya miez 10, mwezi wa sita mpenzi wangu alinipromice kwenda kujitambulisha, akaniambia anasubiri kikao cha familia kwasababu mwaka huu wengi kwenye familia yao watapeleka barua. kuna wanao oa na wengine kuolewa kwa hiyo mila zao kuhusu swala la kumpelekea mtu barua hadi familia ijadili, na alinipa taarifa ya kikao kuwa kitafanyika siku ya Arobaini ya mwaka.
Kwasababu mzazi wake mmoja alifariki, hivyo kuna Arobaini ya mwaka, ndipo kikao kitafanyika na Siku hiyo yataongelewa pia mambo ya barua. Sasa jamani hadi Leo hii arobaini haijafanyika, bebi ananirusha rusha tu akidai anasubiri ndugu, hawezi kukurupuka tu ajipeleke mwenyewe ukweni.
Suala hili linafanya tugombane sana, kila nikimkumbusha ananiambia hadi ndugu hawezi fanya peke yake na ndugu zake wako mbali hadi waje siku ya arobaini.
Natamani sana akajitambulishe kwetu lakini ndio hivyo Arobaini haijafanyika hadi leo.
Kwasababu mzazi wake mmoja alifariki, hivyo kuna Arobaini ya mwaka, ndipo kikao kitafanyika na Siku hiyo yataongelewa pia mambo ya barua. Sasa jamani hadi Leo hii arobaini haijafanyika, bebi ananirusha rusha tu akidai anasubiri ndugu, hawezi kukurupuka tu ajipeleke mwenyewe ukweni.
Suala hili linafanya tugombane sana, kila nikimkumbusha ananiambia hadi ndugu hawezi fanya peke yake na ndugu zake wako mbali hadi waje siku ya arobaini.
Natamani sana akajitambulishe kwetu lakini ndio hivyo Arobaini haijafanyika hadi leo.