Tutafika
JF-Expert Member
- Nov 4, 2009
- 1,443
- 631
Basi leo ndani ya A - town, nimetoka katika hotel moja kupata lunch nikiwa nimeshika chupa ya maji mkononi. Baada ya kutembea kama hatua 100, nikakuta mama mmoja aneonekana kuwa kichaa wa siku nyingi amekaa pembeni ya barabara na furushi la vitu. Mara nikasikia yule mama ananiita ''..mwanangu, we mwanangu naomba hayo maji ninywe. kweli kabisa mi sijawahi kuiba kitu cha mtu...na maneno mengine kibao''
Nikamuangalia kidogo nikakumbuka jana pale mjini Moshi nilikutana na kichaa mwanaume ana bonge la fimbo na akaja kwangu akiwa anafoka eti ''nikupige, nikupige..?'' nikajisemea ngoja niangalie kama na huyu ni wa aina ile ya jana!, Basi nikaona ni mpole nikamfuata kule alikokaa nikampa yale maji. Mama yule aliyapokea na kuanza kunimwagia baraka nyingi sana huku akichomoa Rozali yake shingoni. Yaani nimejisikia vizuri sana kupewa baraka na kichaa kwani nimehisi zimeandikwa mbinguni moja kwa moja!!
Blessed is the hand that give.....Lucky Dube
Nikamuangalia kidogo nikakumbuka jana pale mjini Moshi nilikutana na kichaa mwanaume ana bonge la fimbo na akaja kwangu akiwa anafoka eti ''nikupige, nikupige..?'' nikajisemea ngoja niangalie kama na huyu ni wa aina ile ya jana!, Basi nikaona ni mpole nikamfuata kule alikokaa nikampa yale maji. Mama yule aliyapokea na kuanza kunimwagia baraka nyingi sana huku akichomoa Rozali yake shingoni. Yaani nimejisikia vizuri sana kupewa baraka na kichaa kwani nimehisi zimeandikwa mbinguni moja kwa moja!!
Blessed is the hand that give.....Lucky Dube