Barafu na ice cream

Che Kalizozele

JF-Expert Member
Jul 20, 2008
777
49
Binafsi matumizi ya maneno haya unitatiza kidogo.Nilipokuwa Mwanza,barafu umaanisha zile rambaramba.Lakini nilipofika Dar,barafu umaanisha lile bonge la barafu la maji matupu ambalo wakazi wengi wa dar utumia kupozea maji ya kunywa huku ice cream ikichukua nafasi ya rambaramba.Ninachouliza,kuna maneno ya kiswahili yanayoweza kutofautisha vitu hivi viwili barafu bonge na ice cream,na ni lipi neno la kiswahili kwa ice cream
 
Barafu/ice ni maji (peke yake) yameganda wakati ice cream ni maji yamechanganywa na maziwa (au kitu kingine)
Kimatumizi; barafu/ice unapoozea maji wakati ice cream wailamba yakhe ndio maana ice cream huku kwetu inaitwa lamba lamba.
Lakini kule kwenu kwa kuwa mnalamba hata ice/barafu- basi zote (ice na ice cream) mwaziita lamba lamba.

Maoni yangu.
 
Barafu/ice ni maji (peke yake) yameganda wakati ice cream ni maji yamechanganywa na maziwa (au kitu kingine)
Kimatumizi; barafu/ice unapoozea maji wakati ice cream wailamba yakhe ndio maana ice cream huku kwetu inaitwa lamba lamba.
Lakini kule kwenu kwa kuwa mnalamba hata ice/barafu- basi zote (ice na ice cream) mwaziita lamba lamba.

Maoni yangu.

Nashukuru kwa ufafanuzi wako,naomba unipe neno la kiswahili la ice cream ili nipate kutofautisha vizuri maneno haya.
 
Kuna barafu ambayo inatoka na uchanganyaji wa maziwa na maji na radha kidogo ya kahawa ama iriki ama maji na ukwaju, na inaweza kuongezwa rangi ili kuvutia inaitwa Malai.
 
Kuna barafu ambayo inatoka na uchanganyaji wa maziwa na maji na radha kidogo ya kahawa ama iriki ama maji na ukwaju, na inaweza kuongezwa rangi ili kuvutia inaitwa Malai.

Asante sana mkuu Kibunango kwa kunikumbusha.Kiini cha kuuliza swali hili ilikuwa malai.Neno hili nilisikia Zenj,nilipouliza vizuri jamaa akaniambia wazenj wanatumia maneno yote matatu,yaani barafu,malai na ice cream.Na akasema ukimsikia mzenj anasema ice cream ujue anamaanisha zile za bakhressa.Na hapo ndipo nikapa hamu yakutaka kujua neno la kiwsahili la ice cream
 
Mara nyingi husikia watoto wakisema ashikrimu wakitaka hizo lambalamba (wengine husema rambaramba hichi si kiswahili sahihi neno kuu ni Lamba na sio ramba)
Lamba inamaana ya kula kutumia ulimi kwa mtindo wa kutembeza ulimi ama kinacholiwa kwa kupakaza ulimi.
Baba Wa3 kuna maneno umeyatumia huwa yananichefua kidogo nikikutana na mtanzania mtumiaji wa kiswahili akiyatamka mfano
unitatiza badala ya Hunitatiza (ukiacha ile herufi H basi maana inabadilika na kumtatiza msomaji/msikilizaji)
vilevile kwa maneno "umaanisha" usahihi wake ni humaanisha.
Mkuu kibunango hebu tizama/tazama maneno niliyoyatilia rangi uniambie yakoje masikioni mwa msikilizaji
'Kuna barafu ambayo inatokana na uchanganyaji wa maziwa na maji na radha kidogo ya kahawa ama iriki ama maji na ukwaju, na inaweza kuongezwa rangi ili kuvutia inaitwa Malai.'

lengo langu sio linginelo zaidi ya kutaka tujitahidi kutumia kiswahili vizuri zaidi kwa kadri tuwezavyo ili tuweze kuwafunza na wengine kiswahili kizuri.
 
Mara nyingi husikia watoto wakisema ashikrimu wakitaka hizo lambalamba (wengine husema rambaramba hichi si kiswahili sahihi neno kuu ni Lamba na sio ramba)
Lamba inamaana ya kula kutumia ulimi kwa mtindo wa kutembeza ulimi ama kinacholiwa kwa kupakaza ulimi.
Baba Wa3 kuna maneno umeyatumia huwa yananichefua kidogo nikikutana na mtanzania mtumiaji wa kiswahili akiyatamka mfano
unitatiza badala ya Hunitatiza (ukiacha ile herufi H basi maana inabadilika na kumtatiza msomaji/msikilizaji)
vilevile kwa maneno "umaanisha" usahihi wake ni humaanisha.
Mkuu kibunango hebu tizama/tazama maneno niliyoyatilia rangi uniambie yakoje masikioni mwa msikilizaji
'Kuna barafu ambayo inatokana na uchanganyaji wa maziwa na maji na radha kidogo ya kahawa ama iriki ama maji na ukwaju, na inaweza kuongezwa rangi ili kuvutia inaitwa Malai.'

lengo langu sio linginelo zaidi ya kutaka tujitahidi kutumia kiswahili vizuri zaidi kwa kadri tuwezavyo ili tuweze kuwafunza na wengine kiswahili kizuri.

Nina hakika nitanyooka tu,usikate tamaa endelea kunielemisha.Lakini mkuu tatizo la msingi bado halijatatuliwa.Neno la kiswahili la ice cream,nilipokuona nikajua tayari swali limeshapata jibu kumbe bado.
 
Mara nyingi husikia watoto wakisema ashikrimu wakitaka ..............QUOTE]

Nakubaliana na wewe mkuu: 'Aiskrimu' au 'Ashikirimu' yote yamepata mashiko baina ya wazungumzaji wa kiswahili (wa bara). Kwa Unguja, neno 'malai' linatumika zaidi.
 
Last edited:
Mara nyingi husikia watoto wakisema ashikrimu wakitaka hizo lambalamba (wengine husema rambaramba hichi si kiswahili sahihi neno kuu ni Lamba na sio ramba)
Lamba inamaana ya kula kutumia ulimi kwa mtindo wa kutembeza ulimi ama kinacholiwa kwa kupakaza ulimi.
Baba Wa3 kuna maneno umeyatumia huwa yananichefua kidogo nikikutana na mtanzania mtumiaji wa kiswahili akiyatamka mfano
unitatiza badala ya Hunitatiza (ukiacha ile herufi H basi maana inabadilika na kumtatiza msomaji/msikilizaji)
vilevile kwa maneno "umaanisha" usahihi wake ni humaanisha.
Mkuu kibunango hebu tizama/tazama maneno niliyoyatilia rangi uniambie yakoje masikioni mwa msikilizaji
'Kuna barafu ambayo inatokana na uchanganyaji wa maziwa na maji na radha kidogo ya kahawa ama iriki ama maji na ukwaju, na inaweza kuongezwa rangi ili kuvutia inaitwa Malai.' lengo langu sio linginelo zaidi ya kutaka tujitahidi kutumia kiswahili vizuri zaidi kwa kadri tuwezavyo ili tuweze kuwafunza na wengine kiswahili kizuri.

Nakubali kiswahili yaweza itwa Lamba, lakini wauzaji walipokuwa wanapita wanasema Lamba Lamba, sasa ndio ikapatikana jina lamba lamba. Tukija kwa Maneno uliyomuuliza kibunango na kuyawekea rangi tofauti nadhani amekosea kuyaandika, mfano si "radha" bali ladha, pia si "iriki" bali iliki.

Nilipokuwa shule ya msingi, dio nilianza kulisikia neno Malai (ice cream), toka kwa watoto wa kipemba.
 
Nilipokuwa shule ya msingi, dio nilianza kulisikia neno Malai (ice cream), toka kwa watoto wa kipemba.

Neno Malai nijuavyo mimi lina maana ya ule utando mazito unaopatikana kwenye maziwa baada ya kuchemshwa na kuwekwa yapoe, yakipowa hufanya utando juu kama ngozi fulani, huo utando ndio huitwa MALAI (cream).
Pia kwa wale wenzetu wa pwani kwenye madafu kupatikana MALAI ya madafu ila haya sasa sio utando bali baada ya kunywa maji ya madafu basi kwenye fuu la dafu huwepo na uji mzito ambapo mara nyingine kama dafu limeanza kuelekea kuwa nasi basi MALAI yake huwa magumu zaidi na huweza kuwa kama nazi. basi huo ndio ufahamu wangu juu ya malai.
 
Back
Top Bottom