Black Butterfly
Member
- Aug 31, 2022
- 54
- 99
Habari Wana JF, naomba kuleta malalamiko yangu hapa maana najua kuna Viongozi pia wanapita kusoma taarifa zetu hapa.
Ni muda mrefu sana Barabara ya kutoka Mbezi Luis kwenda Mpiji Magohe ni mbovu sana na wenye Mamlaka wako kimya wananchi tunateseka mno.
Tumejaribu kufikisha kero Ofisi za Serikali ya Mtaa lakini hakuna msaada wowote tunaopata.
=============
Barua ya Wazi kwa Waziri Mkuu kuhusu changamoto Mbezi Luis kwenda Mpigi Magoe
Shikamoo Baba yetu na Waziri Mkuu wetu kipenzi unayesikia na kujali.
Mimi ni Mwananchi wako kutoka Mbezi Mpigi Magoe, naomba tuonee huruma, huku Watoto wa Shule na Wananchi wako tunateseka sana na Barabara.
Kuna wakati Watoto wanafika Shule Saa 3 hadi saa 4 asubuhi kwa sababu ya changamoto ya barabara.
Hii barabara ni muhimu sana na ina wakazi wengi na viongozi, pia inatoka Mbezi Stand Kuu ya Magufuli inaenda hadi Bunju.
Ni barabara mbaya sana imeharibika, gari ikikwama mnaweza kaa hata saa kadhaa za kutosha hampiti. Ndio njia ambayo kama ikitengenezwa kwa lami Mabasi ya mikoa ya Kilimanjaro na Tanga yanapaswa kupita.
Tunaomba sema neno moja kwa ajili ya hii barabara hii maana tumedanganywa na kuahidiwa uongo vya kutosha.
Tumechoka Baba. Tusikie. Ahsante. Nikutakie majukumu mema Baba.
Soma RC wa Dar, Albert Chalamila atoa maelekezo barabara zijengwe usiku na mchana
Ni muda mrefu sana Barabara ya kutoka Mbezi Luis kwenda Mpiji Magohe ni mbovu sana na wenye Mamlaka wako kimya wananchi tunateseka mno.
Tumejaribu kufikisha kero Ofisi za Serikali ya Mtaa lakini hakuna msaada wowote tunaopata.
=============
Barua ya Wazi kwa Waziri Mkuu kuhusu changamoto Mbezi Luis kwenda Mpigi Magoe
Shikamoo Baba yetu na Waziri Mkuu wetu kipenzi unayesikia na kujali.
Mimi ni Mwananchi wako kutoka Mbezi Mpigi Magoe, naomba tuonee huruma, huku Watoto wa Shule na Wananchi wako tunateseka sana na Barabara.
Kuna wakati Watoto wanafika Shule Saa 3 hadi saa 4 asubuhi kwa sababu ya changamoto ya barabara.
Hii barabara ni muhimu sana na ina wakazi wengi na viongozi, pia inatoka Mbezi Stand Kuu ya Magufuli inaenda hadi Bunju.
Ni barabara mbaya sana imeharibika, gari ikikwama mnaweza kaa hata saa kadhaa za kutosha hampiti. Ndio njia ambayo kama ikitengenezwa kwa lami Mabasi ya mikoa ya Kilimanjaro na Tanga yanapaswa kupita.
Tunaomba sema neno moja kwa ajili ya hii barabara hii maana tumedanganywa na kuahidiwa uongo vya kutosha.
Tumechoka Baba. Tusikie. Ahsante. Nikutakie majukumu mema Baba.
Soma RC wa Dar, Albert Chalamila atoa maelekezo barabara zijengwe usiku na mchana