Bajeti ya Mishahara kupanda kwa zaidi ya asilimia 40!

huwezi kuwa shabiki wa magamba ukabaki kuwa timamu, narudia huwezi kuwa gamba ukawa na utimamu
 
hao ndio waandishi wetu. Mimi nimemsikiliza Ghasia alisema fungu la pesa za kulipa wafanyakazi limeongezeka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na mwaka jana. Hakusema mshahara umeongezeka kwa asilimia 40. Fungu kuongezeka haina maana mshahara umeongezeka, inawezekana madeni ya watumishi ndo mengi, au wafanyakazi walioajiliwa wamwongezeka ikilinganishwa na mwaka jana, au kuna taasisi mpya za serikali zimeongezeka. Ukweli ni kwamba mshahara haujaongezeka alisema serikali itaendelea kurekebisha mishahara ya wafanyakazi kulingana na hali ya maisha. SERIKALI HAINA PESA kwa sasa.
 
Hii 'spining' ni kwa sababu Nape kafanya ziara huko au?!!!

Mzee Avatar yako imenikuna sana kwani imenikumbusha enzi zileee za warant na mabasi ya Tanzania Railways Cooperation (TRC) hapo ilikuwa wapi, Tukuyu au??
 
Mnyika kasema hawa ni wasanii wanawadanganya watumishi mana hakuna sehemu yoyote inaonyesha kuwa kuna asilimia 40 imeongezeka kwenye mishahara.MAGAMBA wanaipeleka nchi pabaya.
 
Mishahara haijaongezeka hata senti, 40% ni nyongeza ya fedha tu katika utumishi wa uma.
 
Kwa jinsi nilivyo mpata waziri mwenye dhamana husika akiwasilisha hoja, Ni kwamba fungu zima la bajeti ya mishahara limepanda kwa 40% , sio kwa maana ya mshahara wa mtu mmoja mmoja. Cha msingi ni kusubiri tuone kutoka katika hizo 40% wanazigawa vp kwa mshahara wa mtu mmoja mmoja. Na sio mishahara kupanda tu pia wanaweza kuamua vile vile kutoka katika hilo fungu la 40% waka create ajira mpya. So kwa mantiki hiyo utengezaji wa ajira mpya unaweza ukaathiri kiasi cha ongezeko la mishahara kwa namna moja ama nyingine. Ni hayo tu wakuu, Naomba kuwasisha hoja!
 
Mtoa mada nadhani hata hukuifuatilia hotuba ya Hawa Ghasia, alisema kuwa bajeti ya wizara ya utumishi wa umma kwa mishahara imepanda kwa 40% na siyo mishahara!!! naomba uisome vizuri hiyo sentesi...
 
Back
Top Bottom