Pole sana ndugu,ila mbona hapa si sehemu sahihi?Hapa mambo ya mahusiano tu.Mama yangu alikutana na baba yangu wakiwa masomoni nje ya nchi, wakapendana, wakafunga ndoa - nikazaliwa. Baada ya muda mfupi wakashindwa kuelewana -wakatengana nikiwa na miezi kadhaa na hawakuwa na mawasiliano tena, mama akaolewa na baba aliyenilea na kupata wadogo zangu. Walipoona umri unafaa, wakaniambia juu ya hilo na nikapata hamu ya kumfahamu, nikafanikiwa kumpata kupitia ndugu zake.
Nilisafiri kutoka tulipokuwa tunaishi mpaka kwake, nikafikia kwa ndugu yake ambae ndio tulikuwa na mawasiliano nae. ilipita wiki toka niwasili ndio tukaonana maana alikuwa busy hakuwa na muda wa kuja kuniona pale nilipofikia. Hakuonyesha furaha niliyoitarajia, nikarudi kwetu na hatukuwa na mawasiliano tena.
Nikiwa chuo, nilipata barua kutoka kwake, akilalamika simjali na kwamba namthamini zaidi baba aliyenilea lakini nikae nikijua kuwa yeye ndio baba yangu na sitaweza kubadili hilo. Niliumia. Baadae akaanza kunipigia simu akinitaka nimsaidie kifedha, basically mawasiliano yetu yamejengwa katika utaratibu wa kumsaidia kiasi nikiona simu yake najua kinachofuata! Nimekuwa nikimsaidia kila ninapoweza na kwa uwezo nilio nao ingawa hathamini wala kujali hicho kidogo ninachoweza kumsaidia. Bado nasoma, so anataka tugawane pesa za ufadhili!
Kwa kweli nina wakati mgumu, nashindwa kumshirikisha mama yangu sababu nitakuwa nakumbusha kilio matangani - mpaka leo bado ana hasira nae. Nimekuwa nikimsaidia kwa huruma kutokana na hali aliyonayo, amestaafu na hakujiandaa - ana maisha magumu. Lakini ananikwaza kwa jinsi anavyonilazimisha kumsaidia, ni kama vile ananidai! hana lugha ya upendo, hana subira - ananikwaza!
Naomba mawazo yenu, nifanyeje maana naona tunakoelekea sio kuzuri.