Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Mkazi mmoja wilayani Muleba katika mkoa wa kagera anatafutwa na polisi kwa tuhuma za kumpa ujauzito mtoto wake wa kike wa kumzaa. Bwana Alex Felix, anatuhumiwa kumpa mimba binti huyo mwanafunzi wa kidato cha kwanza. Habari zinasema Bw. Felix alikuwa akimbaka msichana huyo hali iliyopelekea kupata ujauzito.
Kufuatia tukio hilo, mkuu wa wilaya ya Muleba Bi Angela Mabula amemuagiza mkuu wa polisi wa wilaya hiyo kumtafuta na kumkamata mtuhumiwa huyo na hatimaye kumfikisha katika vyombo vya sheria. Kwa sasa msichana huyo anahifadhiwa nyumbani kwa mkuu huyo wilaya baada ya baba yake huyo kutoweka na hivyo kukosa mtu wa kumpa matunzo. Binti mpaka sasa ana mimba ya miezi mitatu.
Kufuatia tukio hilo, mkuu wa wilaya ya Muleba Bi Angela Mabula amemuagiza mkuu wa polisi wa wilaya hiyo kumtafuta na kumkamata mtuhumiwa huyo na hatimaye kumfikisha katika vyombo vya sheria. Kwa sasa msichana huyo anahifadhiwa nyumbani kwa mkuu huyo wilaya baada ya baba yake huyo kutoweka na hivyo kukosa mtu wa kumpa matunzo. Binti mpaka sasa ana mimba ya miezi mitatu.