Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Hebu tuchukulie kwamba, umefuatwa, au unafuatwa fuatwa na mtu uliyewahi kuambiwa kwamba ni baba yako ambaye alikukataa tangu ulipokuwa mdogo. Baba huyu alikukataa katakata kwamba wewe sio mtoto wake wa kumzaa na tangu wakati huo hukuwahi kumtia machoni.
Hii ina maana bila shaka kwamba, hawakuwahi kuishi na mama yako au labda hawakuwa wameoana. Umelelewa na mama au ndugu upande wa mama yako au na wasamaria wema tu. Baada ya kusoma na kupata mafanikio kiuchumi, baba huyu anakuja akiwa anataka umpokee na kumtambua kama baba yako aliyekuzaa. Huenda baba huyu amepigika kimaisha na ndiyo sababu ya kuja kwako au ameshitakiwa na dhamira tu. Hebu niambie, kama ni wewe ungefanya nini?
Hii ina maana bila shaka kwamba, hawakuwahi kuishi na mama yako au labda hawakuwa wameoana. Umelelewa na mama au ndugu upande wa mama yako au na wasamaria wema tu. Baada ya kusoma na kupata mafanikio kiuchumi, baba huyu anakuja akiwa anataka umpokee na kumtambua kama baba yako aliyekuzaa. Huenda baba huyu amepigika kimaisha na ndiyo sababu ya kuja kwako au ameshitakiwa na dhamira tu. Hebu niambie, kama ni wewe ungefanya nini?