Baadhi ya watu wanapomweka mtu wa kuishi kwenye kiwanja ajishikize ama awaangalizie nyumba iliyokamilika huwa wanasahau kuwatoa, kunani ?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Kuna huu utaratibu mtu anakuja kukuomba ajishikize site kwenye kiwanja chako na wengi wao huwa wanapewa ulinzi wa kumuangaliza mwenye nyumba pale inapojengwa ama kumlindia kabla hajahamia.

Kisa cha kwanza: Kuna sehemu walipewa nyumba watu wamekaa mpaka wamezaa watoto wakubwa kabisa wa kwanza kamaliza anaingia darasa la saba mwakani, mwenye nyumba hakuwahi kuja kama miaka mingi mpaka watu walizani nyumba ni ya kwao hao waliopewa waiangalie, juzi juzi yule mwenye nyumba kaja na mjomba wake ambae kasaidia kwa kiasi kikubwa kuwatoa hadi watu wakashangaa aliejenga alikuwa wapi miaka yote.

Kisa cha pili: Kuna jamaa alihamia kwenye nyumba yake haina choo ila Kuna jirani yake alikuwa kajenga nyumba ina choo ila bado hakuhamia, jamaa yule asie na choo alimuomba jirani ambae hakuhamia atumie choo chake na akaruhusiwa bila kinyongo, Ila sasa baada ya muda yule jirani alihamia kwake, yule jamaa bado hajajenga choo kwahio wanatumia choo wote, Sasa jirani akapata pesa akajenga fensi, yaani yule jamaa alimnunia sana mwenzake, yaani Kuna visa vingi vilipita, nilijifunza kitu.
 
Wewe unashangaa huyo kuzaa watoto mpaka wanakua wakubwa.

Kuna gorofa mbezi beach block E Kuna mzee mmoja wa kimakonde alikabidhiwa alinde alikaa hapo mpaka akapata vitukuu. ( watoto wa site wanazaliana mapema sana)


Hiyo nyumba miaka ya JK ndio ikaja kununuliwa na Waziri mmoja kutoka kanda ya ziwa. Ndio anaishi mpaka sasa.
 
Wewe unashangaa huyo kuzaa watoto mpaka wanakua wakubwa.
Kuna gorofa mbezi beach block E Kuna mzee mmoja wa kimakonde alikabidhiwa alinde alikaa hapo mpaka akapata vitukuu. ( watoto wa site wanazaliana mapema sana)


Hiyo nyumba miaka ya JK ndio ikaja kununuliwa na Waziri mmoja kutoka kanda ya ziwa. Ndio anaishi mpaka sasa.
Yaani wakiona speed ya ujenzi inakuwa kubwa na chuki inazidi, wakiona unakaribia kuhamia ndio kabisaa, huwa kuna namna sio bure
 
Na ndio hapo sasa nao wanaweza kujiongeza
Umenikumbusha kuna mmoja alikaa kwenye nyumba ya babu kule nyegezi akajiona amepewa akae pale msukuma yule alikaa na familia yakr na akao mke wa pili mwenye watoto nane nyumba ikawa nyumba
 
Kuna huu utaratibu mtu anakuja kukuomba ajishikize site kwenye kiwanja chako na wengi wao huwa wanapewa ulinzi wa kumuangaliza mwenye nyumba pale inapojengwa ama kumlindia kabla hajahamia.

Kisa cha kwanza: Kuna sehemu walipewa nyumba watu wamekaa mpaka wamezaa watoto wakubwa kabisa wa kwanza kamaliza anaingia darasa la saba mwakani, mwenye nyumba hakuwahi kuja kama miaka mingi mpaka watu walizani nyumba ni ya kwao hao waliopewa waiangalie, juzi juzi yule mwenye nyumba kaja na mjomba wake ambae kasaidia kwa kiasi kikubwa kuwatoa hadi watu wakashangaa aliejenga alikuwa wapi miaka yote.

Kisa cha pili: Kuna jamaa alihamia kwenye nyumba yake haina choo ila Kuna jirani yake alikuwa kajenga nyumba ina choo ila bado hakuhamia, jamaa yule asie na choo alimuomba jirani ambae hakuhamia atumie choo chake na akaruhusiwa bila kinyongo, Ila sasa baada ya muda yule jirani alihamia kwake, yule jamaa bado hajajenga choo kwahio wanatumia choo wote, Sasa jirani akapata pesa akajenga fensi, yaani yule jamaa alimnunia sana mwenzake, yaani Kuna visa vingi vilipita, nilijifunza kitu.
😂😂😂inachekesha kweli
 
Kuna kijini kinaitwa kijini sahau

Unapigwa Kitu na hukumbuki kama una kiwanja wala nyumba ,,
Na unapita hapo hapo site kwako na hupakumbuki tena,

Mimi mwenzenu nimekoma
 
Ndumba zipo lakini pia nature nayo ina nafasi yake kubwa tuu
Sisi tuko connected na nature Hicho unapopata umiliki wa ardhi unapaswa kuitunza na kuipenda, kwa sababu wewe ni sehemu yake
Usipokuwa makini ukampa mwingine akutunzie na nature ikajenga ukaribu na huyo mtu, umekwisha, hutakaa urudi ama utarudi kwa shida sana
 
Back
Top Bottom