Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!

Kwa kwa wale mashabiki wa upinzani mtanisamehe bure, kwenye urais upinzani ni bado sana.

Paskali.
Kama wewe si mshabiki wa upinzani basi ni shabiki wa CCM, na kama ni hivyo basi ingeshangaza sana kama na wewe ungeona kwamba upinzani unafaa kutoa Rais iwe 2020 ama hiyo 2025. Mbali na U-CCM wako lakini pia kwa Makonda na Magufuli umepata sababu za ziada za kuwashabikia na siku hizi huoni haya kwa hilo!

Kama mpaka mwaka 2025 unaona ni CCM tu ndiyo inafaa kutoa Rais basi kuna tatizo, na tatizo la ziada ni pale unapoona anayefaa kugombea huo urais wenyewe. Hili na upinzani kuwa bado sana kwenye nafasi ya Urais ni kwa vigezo vya sayansi ya siasa ama ni kwa mtindo wenu wa kutumia kila zana haramu kuhalalisha ushindi wenu?

Toa sababu ni kwa nini Upinzani haujawa tayari kutoa Rais?
 
Huyu mtu anayejiita Paskali ukomo wake kufikiri umeshagota. Alitegemea ataonekana awamu hii lakini wapi. Hakuna fact hata moja ameandika zaidi ya mashudu ya karne
Huwa ni kazi ngumu sana kumwelewa mtu. Mwenye ideas kinzani na wewe,ndicho kinacho watesa CCM bungeni,
 
Nahisi umeandika ukiwa unakimbia ndo maana hukuwa na muda wa kuwaza vizuri.
Nakuomba ujue kuwa nafasi ya uraisi si ya majaribio,kama ni majaribio basi tosha. Kwa nchi kuongozwa kwa utashi wa mtu na si kwa kufuata katiba na sheria za nchi. ..hapo ni big NO brother,..Huyo mtu wako mshauri aende kwa kina ngosha wenzie kujaribu tu kupewa jimbo...atakuja kukupa salaamu!
Nafikiri watanzania tunataka rais mweledi,awe chini ya katiba na sheria za nchi. Asiwe na visasi,awe na mapenzi ya kweli kwa nchi na watu wake.
Ngosha,hebu kaa ufikirie tena halafu urudi na kama wazo la raisi ajaye bado litakuwa hilo hilo basi nakushauri ufanye ibada ya kufunga na kuomba umuulize Mungu akupe jina.
 
Huyu mtu anayejiita Paskali ukomo wake kufikiri umeshagota. Alitegemea ataonekana awamu hii lakini wapi. Hakuna fact hata moja ameandika zaidi ya mashudu ya karne
Huwa ni kazi ngumu sana kumwelewa mtu. Mwenye ideas kinzani na wewe,ndicho kinacho watesa CCM bungeni,
 
2020 Makonda atakuwa mbunge kipitia jimbo lolote hapa Dar kisha kupanda mpaka kuwa waziri kamili kwa umaarufu huu humu mtakuwa mashahidi.
 
Back
Top Bottom