Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kesho kwenye ukumbi huo huo, Rais Kikwete atazungumza na wazee wa jiji hilo hilo la Dar kuelezea yale yaliyojiri Dodoma. Natumaini ataweka mguu wake ardhini na kusema ni nini hakiwezekani. Ni matumaini yangu waandishi badala ya kukaa na kuangalia kama walivyofanya akiwaambia baraza la mawaziri watauliza maswali haya yasiyokaribishwa.
Waandishi wetu wajifunze kurusha maswali wasingoje hadi waambie basi kuna maswali. Waulize tu hata kwa kurusha hata kama hayatajibiwa.
Juzi Dodoma walikuwa na nafasi kubwa ya kumuuliza maswali lakini wakamuacha anaondoka huku wao (waandishi) wakikusanya vijinotebook vyao kuwahi kuripoti..
"Mhe. Rais, kulikuwa na tetesi kuwa ulikuwa unafanya jitihada za kuwashirikisha wapinzani kuna ukweli wowote"?
"Mhe. Rais kama itatokea Mhe. Chenge akaonekana kuhusika na kashfa ya EPA utakubali wakati huo ajiuzulu au hakuna chochote kumhusu Chenge kitakachokufanya umtoe ndani ya baraza lako"?
"Mhe. Rais ulishiriki namna gani kuhakikisha kuwa Richmond haipewi mkataba, hasa tukikumbuka kuwa uliwaambia waandishi kuwa hukutaka walipwe kwanza"
"Mhe. Rais Kabla ya Waziri Mkuu kutangaza kujiuzulu ulikuwa na taarifa ya kitendo chake hicho au na wewe kama Watanzania wengine ulikisikia/kukiona kwenye radio na luninga"?
n.k n.k
Waandishi wetu wajifunze kurusha maswali wasingoje hadi waambie basi kuna maswali. Waulize tu hata kwa kurusha hata kama hayatajibiwa.
Juzi Dodoma walikuwa na nafasi kubwa ya kumuuliza maswali lakini wakamuacha anaondoka huku wao (waandishi) wakikusanya vijinotebook vyao kuwahi kuripoti..
"Mhe. Rais, kulikuwa na tetesi kuwa ulikuwa unafanya jitihada za kuwashirikisha wapinzani kuna ukweli wowote"?
"Mhe. Rais kama itatokea Mhe. Chenge akaonekana kuhusika na kashfa ya EPA utakubali wakati huo ajiuzulu au hakuna chochote kumhusu Chenge kitakachokufanya umtoe ndani ya baraza lako"?
"Mhe. Rais ulishiriki namna gani kuhakikisha kuwa Richmond haipewi mkataba, hasa tukikumbuka kuwa uliwaambia waandishi kuwa hukutaka walipwe kwanza"
"Mhe. Rais Kabla ya Waziri Mkuu kutangaza kujiuzulu ulikuwa na taarifa ya kitendo chake hicho au na wewe kama Watanzania wengine ulikisikia/kukiona kwenye radio na luninga"?
n.k n.k