Azimio la Arusha: Kuzaliwa upya?

Heri yako Maganjwa maana umetuletea uzi wenye maana katika wakati tukitafakari namna ya kuikomboa Tanzania kutoka katika umagharibi, pengine niseme kuwa azimio la Arusha ndiyo mwongozo bora wa kutupeleka pahala sahihi kama tutalisimamia bila ya kuhujumu mazuri yote yaliyomo, lilitamuka wazi kuwa Tanzania ni nchi ya ujamaa na kujitegemea. nimeyapigia mstari haya maneno mawili kwasababu ndiyo nguzo ya kutuwezesha kupambana na sera mbaya za benki ya dunia na shirika la fedha la umoja wa mataifa ambazo msingi wake ni ubepari unaoelekea kukomaa hapa kwetu ili uwe ubeberu, hii ni hatari kabisa maana hakutakuwa na nafasi ya Tanzania kuendelea kama taifa bali mtu mmojammoja sasa wapi tuna kwenda? Azimio tena la Arusha litasaisia kuondoa unyonyaji, uonevu ,ukandamizaji, uporaji na mambo mengine yanayofanana na hayo kwahiyo , tukaze jamani tukaze, tujifunge mikanda tuweze kurejesha Azimio la Arusha ili uzalendo na maadili ya WATANZANIA KWA TANZANIA yarudi.
 
Azimio la Arusha ni mti. Kuliacha azimio maana yake ni kuacha mti na kubaki katika matawi tukiogelea hewani ammbapo mwishowe ni kudondoka katika maisha na kuanguka jumla. kwahiyo turudishe mti turudishe azimio tuweze kustawi kwa ubora.
 
tuungane shime watanzania AZIMIO la arusha ndio jibu letu
Tunaweza kulipitia azimio upya kwa kuzingatia misingi yake mikuu na kuanzisha sera mpya ya ujamaa na kujitegemea. Viongozi wetu walipiga teke azimio la arusha baada ya kurubuniwa na ubeberu.
 
Huu ni ushauri wangu kwa CCM,

Natambua kwamba nafasi ya Azimio la Arusha ilichukuliwa na Azimio la Zanzibar. Ila kimsingi Azimio la Arusha lilikuwa na msimamo bora zaidi kwenye maswala ya Uongozi bora (Miiko ya Uongozi), utunzwaji na mgao wa rasilimali za Taifa kwa usawa na usawa na haki za raia.

Natambua kwamba endapo CCM itarejesha misingi ya Azimio la Arusha wapo viongozi wengi watakaopoteza sifa za kuwa viongozi. Lakini hii ndio itakuwa dawa ya kutiba Taifa letu.

Asanteni.
 
Hii ni sawa na kuamua kufukua kaburi la marehemu aliyezikwa mwaka 1984 pale Zanzibar miaka 19 iliyopita.
 
Thubutu yake ! Kurudisha azimio la arusha maana yake ni kupeleka jela viongozi wote wa ccm , nani atakubaliana na hilo ?
 
Hebu fatilia hii link ujikumbushe Azimio la Arusha lilikuwa linasema nini ndugu ZeMarcopolo (The Tanzania National Website). Kwa mtazamo wangu mazuri Azimio hili ni zaidi ya 85%.

Azimio la Arusha ni zuri kwa nchi ambayo ina social security sytem inayogusa raia wake wote.

Mtu anapokuwa kiongozi na kukatazwa kumiliki biashara yoyote, siku akipoteza maisha watoto wake hawana mtu wa kuwahakikishia financial support.

Cha msingi ni kuwa na mifumo inayohakikisha kuwa ubadhilifu unashughulikiwa ipasavyo. Kukataza watu kuwa na mali ni kuwakataza kutumia ubongo wao. Allow people to think. Nchi haiwezi kuendelea kama watu wake hawafikirii njia mbalimbali za kujikomboa kiuchumi. Bill Gates angekatazwa kuwa na biashara leo hii kusingekuwana na Microsoft.

Katika azimio la Arusha kiongozi anatafsiriwa kama Kiongozi pamoja na mke au mme wake. Hii ni kumaanisha familia ya kiongozi yoyote hairuhusiwa kufikiria uzalishaji mali mwingine wowote, itegemee mshahara tu!!!

Azimio HALITEKELEZEKI...
 
Mkuu kwani lilienda wapi?

nasikitika lilienda kaburini na viwanda vyetu vyote!!!!!!!!!!!! UFI, KIBUKU,MWATEX,MUSOMA TEXTILE, Kiwanda cha Chuma Mang'ula kauziwa mama Mchungaji Rwakatare leo kafanya shule mitambi imeuzwa yote kama chuma chakavu, Tanganyika Packers, STAMICO ilikufa leo wanajifanya kufufua kwa kuipa mgodi uliyokwisha, naomba Azimio lirudi na viwanda virudi!
 
Azimio la Arusha ni zuri kwa nchi ambayo ina social security sytem inayogusa raia wake wote.

Mtu anapokuwa kiongozi na kukatazwa kumiliki biashara yoyote, siku akipoteza maisha watoto wake hawana mtu wa kuwahakikishia financial support.

Cha msingi ni kuwa na mifumo inayohakikisha kuwa ubadhilifu unashughulikiwa ipasavyo. Kukataza watu kuwa na mali ni kuwakataza kutumia ubongo wao. Allow people to think. Nchi haiwezi kuendelea kama watu wake hawafikirii njia mbalimbali za kujikomboa kiuchumi. Bill Gates angekatazwa kuwa na biashara leo hii kusingekuwana na Microsoft.

Katika azimio la Arusha kiongozi anatafsiriwa kama Kiongozi pamoja na mke au mme wake. Hii ni kumaanisha familia ya kiongozi yoyote hairuhusiwa kufikiria uzalishaji mali mwingine wowote, itegemee mshahara tu!!!

Azimio HALITEKELEZEKI...
Wewe ni mburula maana kila thread unatetea magamba hata kama ina maslahi kwa taifa wewe unatetea magamba.jamani ebu tuweni na uzalendo japo kidogo maana watoto wetu, wajukuu zetu wataenda wapi kama nchi yote itauzwa kiholela namna hii? Buku 7 haziwafikishi popote hebu jaribuni kuwa serious kidogo.
 
Mtu anapokuwa kiongozi na kukatazwa kumiliki biashara yoyote, siku akipoteza maisha watoto wake hawana mtu wa kuwahakikishia financial support.
..
hii inatakiwa iingizwe kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM - 2015 NIMEIPENDA!!!
 
Tukiwa kwenye kumbu kumbu ya miaka 16 ya kifo cha aliekua Rais wa kwanza wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania embu turudi nyuma kidogo tujadili haya Maazimio.

Nikianza na Azimio la arusha ambalo wengi msingi wake mkuu ni kuishi kwa usawa,kuua mfumo wa kibepari ulioanza kukua miaka hiyo ya 1967.

Baada ya kuliua Azimio la Arusha na kuibuka na Azimio la Zanzibar 1994 miiko ya uongozi ilififia na huo ukawa ndio mwanzo wa kuchanganya siasa na biashara.

Azimio la Zanzibar ndio chanzo cha kupoteza maadili na miiko ya uongozi kwenye serikali.

Nukuu ya Mwalimu Nyerere" Mwalimu Nyerere alitaadharisha kwamba wale waliokwenda Zanzibar na kulitupa baharini Azimio la Arusha na miiko ya uongozi wanahujumu misingi isiyo na doa ya taifa letu. "

Msingi wa Azimio la Arusha ni ulibeba dhana zima ya Sera ya ujamaa na kujitegemea,

Msingi wa Azimio la Arusha ulibeba dhana zima ya mfumo wa kibepari.

.....Je miiko ya Azimio la Arusha iliishia wapi?
Je azimio la Zanzibar halikua na Miiko?
 
CCM ilipanda mbegu ambayo sasa imegeuka kuwa sumu maana punde sumu hiyo iliyokivuruga na kukigawa chama cha Mapinduzi ndio inakimaliza rasmi ma agenti wake wakiporomosha matusi huku na kule.
 
Back
Top Bottom