Atoboe au aendelee kuficha siri?!

Bibie kwa ushauri wako naamini kabisa jamaa hatothubutu tena kumsumbua mwanamama..
Mh ndugu yangu hii wala haitamsaidia sana kwani bado dhamira itaendelea kumsuta kwa aliyoyatenda. Ni uamuzi mbaya aliyoufanya sema tu nasi tunashirikiana naye kumshauri visivyo kwa kuwa alitakiwa amwambie ukweli mumewe then asubiri matokeo ila kwa kuwa ni wazi alichokifanya sicho basi ajaribu kote kote akishindwa ndo bazi zake zilitimia!

Ila sidhani kama hilo ni solution kwani kama shemeji ni mkorofi anaweza akaamua kulikisha news kwa njia yoyote ili amkomoe bibie lol na yeye ajitie kitanzi ah!
 
Duh hii kali mwambie Lucy ampe ili apate mtoto wa 2 tena maana jamaa huyo ana matatizo lakini alipo pata ujauzito alikosea kumwambia huyo pacha ilitakiwa aweke siri tu kulinda heshima ya ndoa.
 
Na huyo shemeji sasa ameamua kumnyanyasa mwenzake, kama aliamua kumsaidia anataka nini tena, tenda wema uende zako yeye anataka riba.
shemejishemeji huku wazima taaaa............ shemeji kaonja asali kwahiyo msimlaumu kwani muonja asali kuchonga mzinga asili yake.kosa ni la huyo mwanamke asiyekuwa na imani na Mungu wake akaaamua kuvunja amri ya sita shemeji wa watu walaaaa mchiguche kabthaaaaaaa
 
Back
Top Bottom