Askofu Zakaria Kakobe: Tanzania siyo nchi ya chama kimoja! Amtaka Rais Magufuli atubu

*ASKOFU KAKOBE AJIPE MUDA KUTAFAKARI .

Nimesoma mitandaoni maneno anayosadikiwa kuyasema kiongozi mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) lililopo Mwenge, Askofu Zakaria Kakobe akimsakama Rais Magufuli kwa maneno mazito na kumtaka atubu. Lahaula!

Nimebaki nikijiuliza kati ya Rais Magufuli na Askofu Kakobe nani anatakiwa atubu?!. *Askofu Kakobe anatakiwa aanze kutubu yeye* kwa sababu:-

1. Mwaka 1995 aliwaaminisha Watu kuwa Augustine Mrema atashinda urais na kuingia Ikulu. Kakobe alidai amepewa maono hayo lakini mwisho wa siku Mrema aliangushwa vibaya na Benjamin Mkapa akashinda urais. Kakobe ulishatubu juu ya hili?

2. Kakobe huyu huyu akaibuka tena 2015 akasema Mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa atashinda urais lakini akaishia kupata aibu nyingine ya Mgombea wake huyo kushindwa urais. Kakobe hakuwahi kutubu dhambi hii ya kuwadanganya Watanzania.

3. Kakobe aliwahi kuwaambia waumini wake umeme uliopita juu ya kanisa lake hautakaa ufanye kazi. Mpaka kesho umeme huo unafanya kazi. Kakobe alitakiwa aendelee kutubu tu kwa dhambi hii ya kuwadanganya mpaka waumini wake.

4. Kakobe huyu anayemvaa na kumrarua Rais Magufuli kwa maneno makali anatakiwa kuanza kutubu yeye maana ameshindwa kuheshimu mamlaka ya hapa Duniani wakati kwenye kitabu kitakatifu cha Biblia Mwenyezi Mungu amewaagiza Wanadamu kuheshimu mamlaka za hapa Duniani na za Mbinguni lakini huyu anayejiita Askofu Kakobe ameshindwa kulitambua na kuheshimu hili. Kakobe nenda katubu kabisa kwa kushindwa hata kuheshimu mamlaka, kuitii Biblia na kuheshimu agizo la Mwenyezi Mungu.

5. Kakobe huyu huyu anatakiwa atubu kabisa kwa kuanza kuhubiri siasa kanisani tena Madhabahuni (sehemu takatifu) badala ya kuhubiri neno la Mungu, kuhubiri Biblia inasemaje na kumuhubiri Mwenyezi Mungu. Kitendo cha kutelekeza neno la Mungu na kuvaa uanasiasa si tu kuwagawa Waumini wake bali pia ni kutikisa misingi ya amani ambayo imejengwa kwa gharama kubwa za jasho, mateso na kujitoa kwingi kwa Waasisi wetu. Kakobe nenda katubu kwa uchochezi huu.

Askofu Kakobe alitakiwa ajipe muda wa kutosha wa kufikiri juu ya matendo yake na kauli zake kabla ya kuzitoa madhabauni. Alipaswa kujifunza faida na hasara zake.

Askofu Kakobe alitakiwa aendelee kujifunza juu ya mwelekeo wa Tanzania Mpya na mwelekeo wake Mpya kwa sasa. Tanzania mpya ya sasa inayoongozwa na Rais Magufuli haina muda wa siasa za chini ya Mwembe tena.

Kwa Wahubiri wanasiasa kama Kakobe watamuona Magufuli ni tatizo ila kwa Watanzania Wazalendo tunamuona Rais Magufuli ni Mkombozi kwa Taifa letu. Tunamuona Rais Magufuli ndiye Mussa wa Watanzania wetu kwa sasa anayetutoa Misri kwenye mateso, anatuvusha bahari ya Shamu na kutupeleka Kaanani, nchi ya Maziwa na Asali. Daima sisi Watanzania wanyonge tutaendelea kumuunga mkono Rais Magufuli siku zote, nyakati zote.

Utter bullshit! Tujifunze kutokuwa na double standards! Tutafuta mchawi mpaka kesho kutwa Ila tunajiloga wenyewe kwa kauli za kinafki kama hizi. Hata kama mtazamo wa Kakobe siukubali, Ila hii kauli haipangui hoja yake, ndio kwanza inadhihirisha mapungufu ya mwandishi.
 
Mimi ninadhani kuna umuhimu wa kumwelewa mtu mwenyewe ni nani. Mhaya na kiswahili wapi na wapi? Msameheni bure tu maana bora hata mkurya ambaye huishiakusema vita ni vita mura lkn huyu anayesema basi nikaona land-rover ikaja ikabeba magari maine ya baba ikaondoka nayo. Utamuelewa?
 
Kwa Tanzanian swala la kushinda na kutangwaza mshindi ni vitu viwili tofauti unless hauishi ndiyo utakuwa huelewi. Kama unaishi Tanzania basi unajua yanayotokea na mfano nyang'avu ni Zanzibar. So swala lako la kwanza siyo valid.
Umesema aanze yeye kutubu na ukatoa makosa yake (mtazamo wako ) then atafata mkulu, please nitajie ya mkulu, au hakuna?
Then leta comparison yapi ni hatari kwa ustawi wa Taifa
 
Kauli moja tu ya Kakobe imewaibua mende, kenge, mamba you name it kutoka pangoni. Alipofananishwa na Mugabe hawa watu walikuwa wapi? Mifano ya Kakobe imewauma sana aisee. Rais mzima kujibishana na mwanafunzi wa chuo kikuu ni uzwazwa.
 
# Nimekusiliza kwa makini Sana toka Jana na nimekua nikiirudia mara kwa mara clip yako ili nipate kujua Ulikua ukimaanisha nini. Katika kipande kile cha sauti nimekusikia ukilalamika kua raisi Magufuli hataki kushauliwa. Naomba nikuulize,Hivi unajua maana ya Ushauri? Naje unajua katiba inasema nini kuhusu Ushauri anao pewa raisi?

# Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania Sura ya Tatu ya katiba inayoelezea haki na wajibu wa Raia, ibara ya 37 kifungu kidogo cha Kwanza kinasema na nitanukuu "37.-(1) Mbali na kuzingatia masharti yaliyomo katika Katiba
hii, na sheria za Jamhuri ya Muungano katika utendaji wa kazi na shughuli zake, Rais atakuwa huru na hatalazimika kufuataushauri atakaopewa na mtu yeyote, isipokuwa tu paleanapotakiwa na Katiba hii au na sheria nyingine yoyote kufanya jambo lolote kulingana na ushauri anaopewa na mtu au mamlaka
yoyote."

# Nafikiri utakua umenielewa nini nilikusudia kusema, Kila mmoja anashauri kwa namna anavyoona yeye inafaa lakini rais anafuata katiba hivyo haruhusiwi wala halazimishwi eti kutembea kazi Ushauri wa mtu. Atafanya hivyo tu pale anapoona inafaa.

# Baba askofu unapaswa ujue maana ya Ushauri, Ushauri maana yake ni Mawazo ama mapendekezo anayo pewa mtu juu ya jambo fulani. Na mapendekezo hayo yaweza kukubaliwa ama kutaliwa, sasa yanapo kataliwa kwanini iwe nongwa?

# Baba askofu ukiisoma biblia vizuri katika kitabu cha injili ya Luka, Yesu alipo kua mlima sayuni akiomba na kulia huku jasho Kama matone ya damu yakitililika mpaka chini akiomba kwa Mungu kua,kama ikimpendeza amuepushie kikombe hiki cha Mateso lakini mapenzi ya Mungu ya timie na sio Ya kwake Yesu.

# Huu Ulikua ni Ushauri wake Yesu kwenda kwa Mungu, na Mungu alipo iona Hofu ndani yake alimtuma Malaika kuja kumtia moyo na yaliyoandikwa yakatimia.

# Hivyo baba askofu Kakobe Ushauri unaotolewa na watu mbali mbali usiufanye kua ati kwamba ni Lazima Raisi autekeleze.

# Hata wewe nakumbuka Ushauri uliopewa wa kuondoa kanisa hapo lilipo ulikataa na mpaka ukawavika T-shirt waumini wako kuiomba Tanesco Umuogope Mungu. Sasa kama wewe ulishindwa kufuata ushauri inakuaje iwe halali kwako kwa wengine iwe dhambi?

# Note Injili ya Luka Yesu anasema,mbona unakitazama kibanzi kilichomo katika jicho la nduguyo ilihali huoni boriti iliyo Katika jicho lako mwenyewe.

# Mnafiki wewe toa boriti katika jicho lako kisha uje utoe Kibanzi kwa nduguyo.
6247e09944af94faebb1447db5f28195.jpg
 
Okay hypothetically lets say my english is poor mr. English professor, Do you think by any chance i might have a notion on that particular preposition?
 
JE KAKOBE ATAWEZA KUREJESHA ENZI ZAKE ?.

Waraka wa BASHIR YAKUB.
+255784482959.

Amepotezwa sana na wachungaji , manabii na mitume. Utitiri na ujio wa hawa katu haukumuacha salama kakobe.

Alitingisha sana miaka kama 10 iliyopita hivi. Kila mwenye ugonjwa, madeni, roho ya kukataliwa, mapepo, majini, tatizo la ajira, hitaji la ndoa, mikosi, kuandamwa, na kila jambo baya alimuwaza Kakobe. Basi anataka kurejesha enzi hizi.

Nakumbuka siku za ibada barabara ya Sam Nujoma ilijaa foleni na kila ulipouliza kunani barabara hii weekend, uliambiwa ni msururu wa kuingia kanisani kwa Kakobe.

Waumini walijaa pomoni ndani ya kanisa mpaka nje, na nje mpaka kwenye kingo za barabara ielekeayo mwenge. Mikoani watu waliuza vipande vya ardhi na mifugo ili wapate nauli ya kuja Mwenge kumuona Kakobe. Anajaribu kurejesha enzi hizi.

Nakumbuka vipindi vyake kwenye televisheni. Nakumbuka kile kilichoitwa SAA YA MAAJABU na baadae SAA YA FARAJA pale chanel ten. Wako watu walifikia hatua ya kuzikumbatia luninga zao wakibubujikwa na machozi wakati Kakobe akiomba. Wako walioamini kuangalia kipindi kile ni nusu ya kumuona Kakobe na kumuona kakobe ni nusu ya kumuona Mungu.
Kakobe anataka enzi hizi zirejee haraka.

Nakumbuka ziara yake nchi za Afrika ya kati hasa Kongo DRC. Nilibahatika kuona video yake tangu mapokezi hadi mahubiri kwenye mkutano ulioitwa "GREAT MIRACLE HEALING CRUSADE". Kwa kipindi kile nilikuwa sijawahi kuona umati kama ule. Mpaka rais Kabila Kabange na mkewe Olive Lembe walilazimika kuomba ziara kwenye mkutano wake ili wajue Kakobe ninani.

Maajab ya dunia, Kakobe si mtumishi anayetajwa leo. Si kimbilio tena. Si chaguo namba moja kwa wenye shida leo. Leo ukitaja watumishi wanaotingisha ati Kakobe humuweki tena !!!?, looh kweli mambo ya dunia ni ya mapito tu. Leo unakutana na mtu anakuuliza "hivi Kakobe huwa yupo". Leo akifufuka aliyekufa kipindi kile ukamwambia Kakobe si kimbilio namba moja kwa wenye kuhitaji kuombewa atajua amefufukia nchi nyingine.

Kakobe anayofanya sasa ni mbinu ya kutaka kurejesha enzi zake. Kakobe ni mwanafalsafa na hivyo anajua namna pekee ya kurejesha enzi zake ni kuzusha mabishano na mtu maarufu zaidi. Alifuatilia vizur mabishano ya Gwajima na viongozi na anajua ni kwa namna gani Gwajima alijijenga kupitia mtaji huo.

Anajua atakuwa gumzo, anajua ataiteka media hasa social media na kubwa anajua watu watajaa kanisani kwake siku za ibada wakisubiri kusikia leo atasema lipi kama ilivyokuwa kwa Gwajima.

Ni mtaji mzuri ikiwa atafanikiwa ila nachelea kusema ikiwa atafanikiwa. Trend ilivyo anaweza kupoteza zaidi badala ya kufanikiwa.

Sitazungumzia uaskofu wake ambao ndugu Pengo aliwahi kuhoji aliupataje, alipewa na nani na kwa utaratibu upi. Pengo alisema huwezi kuamka asubuh ukasema mi ni askofu.

Niseme tu Kakobe analazimisha kurejea. Swali ni je ametumia mbinu sahihi, na je ataweza ?.
 
Mjini Kila Mtu anatafuta namna ya kutoka!
Na Yeye anataka kuwa Talk of the town Kama Gwajima
 
Bro kama huna kazi ni bora muda uliupoteza kuandika huu upupu ungekaa na familia yako. Kwanza huu ni msimu wa sikukuu walau watoto na shemela wangesikia irregular tones yako.
In short huu ni upupu umeandika hapa.
Jitafakari
 
Back
Top Bottom