Askofu Zakaria Kakobe: Tanzania siyo nchi ya chama kimoja! Amtaka Rais Magufuli atubu

Dick rider
It is schadenfreude when thieves cannot provide offering to their brain masters.
Naona sikukuu haikuwapa nafasi ya kula pesa za wizi maana hii siyo hasira ya kawaida. Sadaka pia zimepungua.
Nawe uko kwa Kakobe unasubili upatiwe uzazi, mimba?
Hii siyo dunia ya kusubili neema kanisani wakati mbele yenu kuna mtu aliyeshindwa ajira zingine.
 
Kwani askofu alimtaja raisi wetu? Au mmeshindwa kutafsiri mafumbo ya askofu wetu kakobe? Alichoongea askofu ni ukweli mtupu, hata hizo chaguzi unazozisema, alikaa na aliona kila chaguzi masisiemu hayakosi kuiba kura, na hakuna chaguzi isiyoibiwa kura tz, hata kitongoji kura zinaibiwa labda huishi bongo!
Acheni sindano za maaskofu zizame na sio kuleta visingizio vya kufanya siasa madhabahuni, soon tutaskia kaanza kufuatwa na nisani patrol8):)):D
viumbe wajinga kila anayejiita askofu mnamuamini
 
Miongoni mwa misingi ya demokrasia ni kukubali kutokubaliana hivyo tukubali kuwa na mawazo mbadala ikibidi mbn dada zetu wanavaa nguo fupi hawajaitwa wachochezi au mchochezi ni mtu anaye pingana kisiasa?
 
It is schadenfreude when thieves cannot provide offering to their brain masters.
Naona sikukuu haikuwapa nafasi ya kula pesa za wizi maana hii siyo hasira ya kawaida. Sadaka pia zimepungua.
Nawe uko kwa Kakobe unasubili upatiwe uzazi, mimba?
Hii siyo dunia ya kusubili neema kanisani wakati mbele yenu kuna mtu aliyeshindwa ajira zingine.
Okay hypothetically tuseme huyo bwana ametumwa au anatafuta kiki, vyovyote vile au sadaka but it is indeed what he claims is a somewhat naked truth only retards will repudiate that..
 
Nimesoma mitandaoni maneno anayosadikiwa kuyasema kiongozi mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) lililopo Mwenge, Askofu Zakaria Kakobe akimsakama Rais Magufuli kwa maneno mazito na kumtaka atubu. Lahaula!

Nimebaki nikijiuliza kati ya Rais Magufuli na Askofu Kakobe nani anatakiwa atubu?!. *Askofu Kakobe anatakiwa aanze kutubu yeye* kwa sababu:-

1. Mwaka 1995 aliwaaminisha Watu kuwa Augustine Mrema atashinda urais na kuingia Ikulu. Kakobe alidai amepewa maono hayo lakini mwisho wa siku Mrema aliangushwa vibaya na Benjamin Mkapa akashinda urais. Kakobe ulishatubu juu ya hili?

2. Kakobe huyu huyu akaibuka tena 2015 akasema Mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa atashinda urais lakini akaishia kupata aibu nyingine ya Mgombea wake huyo kushindwa urais. Kakobe hakuwahi kutubu dhambi hii ya kuwadanganya Watanzania.

3. Kakobe aliwahi kuwaambia waumini wake umeme uliopita juu ya kanisa lake hautakaa ufanye kazi. Mpaka kesho umeme huo unafanya kazi. Kakobe alitakiwa aendelee kutubu tu kwa dhambi hii ya kuwadanganya mpaka waumini wake.

4. Kakobe huyu anayemvaa na kumrarua Rais Magufuli kwa maneno makali anatakiwa kuanza kutubu yeye maana ameshindwa kuheshimu mamlaka ya hapa Duniani wakati kwenye kitabu kitakatifu cha Biblia Mwenyezi Mungu amewaagiza Wanadamu kuheshimu mamlaka za hapa Duniani na za Mbinguni lakini huyu anayejiita Askofu Kakobe ameshindwa kulitambua na kuheshimu hili. Kakobe nenda katubu kabisa kwa kushindwa hata kuheshimu mamlaka, kuitii Biblia na kuheshimu agizo la Mwenyezi Mungu.

5. Kakobe huyu huyu anatakiwa atubu kabisa kwa kuanza kuhubiri siasa kanisani tena Madhabahuni (sehemu takatifu) badala ya kuhubiri neno la Mungu, kuhubiri Biblia inasemaje na kumuhubiri Mwenyezi Mungu. Kitendo cha kutelekeza neno la Mungu na kuvaa uanasiasa si tu kuwagawa Waumini wake bali pia ni kutikisa misingi ya amani ambayo imejengwa kwa gharama kubwa za jasho, mateso na kujitoa kwingi kwa Waasisi wetu. Kakobe nenda katubu kwa uchochezi huu.

Askofu Kakobe alitakiwa ajipe muda wa kutosha wa kufikiri juu ya matendo yake na kauli zake kabla ya kuzitoa madhabauni. Alipaswa kujifunza faida na hasara zake.

Askofu Kakobe alitakiwa aendelee kujifunza juu ya mwelekeo wa Tanzania Mpya na mwelekeo wake Mpya kwa sasa. Tanzania mpya ya sasa inayoongozwa na Rais Magufuli haina muda wa siasa za chini ya Mwembe tena.

Kwa Wahubiri wanasiasa kama Kakobe watamuona Magufuli ni tatizo ila kwa Watanzania Wazalendo tunamuona Rais Magufuli ni Mkombozi kwa Taifa letu. Tunamuona Rais Magufuli ndiye Mussa wa Watanzania wetu kwa sasa anayetutoa Misri kwenye mateso, anatuvusha bahari ya Shamu na kutupeleka Kaanani, nchi ya Maziwa na Asali. Daima sisi Watanzania wanyonge tutaendelea kumuunga mkono Rais Magufuli siku zote, nyakati zote.

Naona wameamua kumjibu kakobe.

Source

Breaking news swahili.
Pengo na shekh wa bakwata dar wao kazi yao ni kuisifu tu serikali hao mbona hamsemi wanachanganya dini na siasa?
 
Mbunge wa wa Tarime John Heche amewaonya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kuwa kama wanataka kumjibu Askofu Zacharia Kakobe kwa niaba ya serikali iliyopo madarakani basi wajibu kwa hoja na siyo kuropoka.

Heche amesema hayo ikiwa ni siku moja baada ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mkoa huo, Frank Kamugisha kumtaka Askofu Kakobe aende kufanya toba na kisha kuwaomba radhi wana CCM wa Dar es salaam kwa kuacha miiko ya kidini na kushindwa kutumia busara na kisha kusema hovyo.

Akizungumza jana na Wanahabari Kamugisha alivitaka vyombo vinavyohusika na sheria vihakikishe hakuna mtu anayepata fursa ya kumtukana au kumbeza Rais wa nchi na kufafanua kwamba Rais amejipambanua katika kuwasaidia wananchi na anafanya mambo hayo kwa udhati wa moyo wake hivyo mtu anyebeza moja kwa moja atakuwa msaliti.

Heche amandika kwenye ukurasa wake wa Twitter na kusema kwamba "CCM kama mnataka kujibu hoja za Askofu Kakobe kwa niaba ya Rais Magufuli na Serikali jibuni kwa hoja, sio kuropoka! kazi za wachungaji ni kukemea maovu yote yaliyopo duniani, watu wanapotea, wanapigwa risasi, wanaokotwa baharini, sheria za nchi hazifuatwi, haya yatakemewa na kila mtanzania" Heche.

Source eatv news.
 
# Nimekusiliza kwa makini Sana toka Jana na nimekua nikiirudia mara kwa mara clip yako ili nipate kujua Ulikua ukimaanisha nini. Katika kipande kile cha sauti nimekusikia ukilalamika kua raisi Magufuli hataki kushauliwa. Naomba nikuulize,Hivi unajua maana ya Ushauri? Naje unajua katiba inasema nini kuhusu Ushauri anao pewa raisi?

# Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania Sura ya Tatu ya katiba inayoelezea haki na wajibu wa Raia, ibara ya 37 kifungu kidogo cha Kwanza kinasema na nitanukuu "37.-(1) Mbali na kuzingatia masharti yaliyomo katika Katiba
hii, na sheria za Jamhuri ya Muungano katika utendaji wa kazi na shughuli zake, Rais atakuwa huru na hatalazimika kufuataushauri atakaopewa na mtu yeyote, isipokuwa tu paleanapotakiwa na Katiba hii au na sheria nyingine yoyote kufanya jambo lolote kulingana na ushauri anaopewa na mtu au mamlaka
yoyote."

# Nafikiri utakua umenielewa nini nilikusudia kusema, Kila mmoja anashauri kwa namna anavyoona yeye inafaa lakini rais anafuata katiba hivyo haruhusiwi wala halazimishwi eti kutembea kazi Ushauri wa mtu. Atafanya hivyo tu pale anapoona inafaa.

# Baba askofu unapaswa ujue maana ya Ushauri, Ushauri maana yake ni Mawazo ama mapendekezo anayo pewa mtu juu ya jambo fulani. Na mapendekezo hayo yaweza kukubaliwa ama kutaliwa, sasa yanapo kataliwa kwanini iwe nongwa?

# Baba askofu ukiisoma biblia vizuri katika kitabu cha injili ya Luka, Yesu alipo kua mlima sayuni akiomba na kulia huku jasho Kama matone ya damu yakitililika mpaka chini akiomba kwa Mungu kua,kama ikimpendeza amuepushie kikombe hiki cha Mateso lakini mapenzi ya Mungu ya timie na sio Ya kwake Yesu.

# Huu Ulikua ni Ushauri wake Yesu kwenda kwa Mungu, na Mungu alipo iona Hofu ndani yake alimtuma Malaika kuja kumtia moyo na yaliyoandikwa yakatimia.

# Hivyo baba askofu Kakobe Ushauri unaotolewa na watu mbali mbali usiufanye kua ati kwamba ni Lazima Raisi autekeleze.

# Hata wewe nakumbuka Ushauri uliopewa wa kuondoa kanisa hapo lilipo ulikataa na mpaka ukawavika T-shirt waumini wako kuiomba Tanesco Umuogope Mungu. Sasa kama wewe ulishindwa kufuata ushauri inakuaje iwe halali kwako kwa wengine iwe dhambi?

# Note Injili ya Luka Yesu anasema,mbona unakitazama kibanzi kilichomo katika jicho la nduguyo ilihali huoni boriti iliyo Katika jicho lako mwenyewe.

# Mnafiki wewe toa boriti katika jicho lako kisha uje utoe Kibanzi kwa nduguyo.
 
Jamaa yako atubu kwanza hadharani hata akifanya mazuri kiasi gani hayazidi ...za watu
 
Kama kawaida yao maccm wanaagiza mapolisi wakakamate na kutupa lupango (intimidation)

Nime note kupitia maneno yao maccm kuwa magufail ana kashfa (ndio maana anakashfika) ni mdhambi (ndio maana anatakiwa atubu)
Hafuati sheria (wanamsingizia udhati wa moyo! Mbona hachunguzi rushwa ya madiwani arusha udhati uko wapi hapo)

Ni mhalifu.
(amejipambanua kufurahia mateso kwa watanzania wapinzani)

AMEVUNJA KATIBA.
 
Namuunga mkono Heche. Sio kwamba nitamuunga mkono mtu yeyote, kwa cheo chake au hata kwa mdomo wake amtukane rais. Siungi mkono kabisaaaaa. Ila mngeweza kunionyesha matusi ya Kakobe nadhani ningeelewa. Jamani, tusiwe na kawaida ya kuongeza chumvi ili tu kuchajisha rais akasirike. Rais ni mtu ambaye Mungu kamjalia hekima tele hivyo mnatenda dhambi kumpotosha. Ana uwezo wa kuyatafakari maneno ayasikiayo. Msimsaidie kufikiri.
 
*ASKOFU KAKOBE AJIPE MUDA KUTAFAKARI .

Nimesoma mitandaoni maneno anayosadikiwa kuyasema kiongozi mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) lililopo Mwenge, Askofu Zakaria Kakobe akimsakama Rais Magufuli kwa maneno mazito na kumtaka atubu. Lahaula!

Nimebaki nikijiuliza kati ya Rais Magufuli na Askofu Kakobe nani anatakiwa atubu?!. *Askofu Kakobe anatakiwa aanze kutubu yeye* kwa sababu:-

1. Mwaka 1995 aliwaaminisha Watu kuwa Augustine Mrema atashinda urais na kuingia Ikulu. Kakobe alidai amepewa maono hayo lakini mwisho wa siku Mrema aliangushwa vibaya na Benjamin Mkapa akashinda urais. Kakobe ulishatubu juu ya hili?

2. Kakobe huyu huyu akaibuka tena 2015 akasema Mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa atashinda urais lakini akaishia kupata aibu nyingine ya Mgombea wake huyo kushindwa urais. Kakobe hakuwahi kutubu dhambi hii ya kuwadanganya Watanzania.

3. Kakobe aliwahi kuwaambia waumini wake umeme uliopita juu ya kanisa lake hautakaa ufanye kazi. Mpaka kesho umeme huo unafanya kazi. Kakobe alitakiwa aendelee kutubu tu kwa dhambi hii ya kuwadanganya mpaka waumini wake.

4. Kakobe huyu anayemvaa na kumrarua Rais Magufuli kwa maneno makali anatakiwa kuanza kutubu yeye maana ameshindwa kuheshimu mamlaka ya hapa Duniani wakati kwenye kitabu kitakatifu cha Biblia Mwenyezi Mungu amewaagiza Wanadamu kuheshimu mamlaka za hapa Duniani na za Mbinguni lakini huyu anayejiita Askofu Kakobe ameshindwa kulitambua na kuheshimu hili. Kakobe nenda katubu kabisa kwa kushindwa hata kuheshimu mamlaka, kuitii Biblia na kuheshimu agizo la Mwenyezi Mungu.

5. Kakobe huyu huyu anatakiwa atubu kabisa kwa kuanza kuhubiri siasa kanisani tena Madhabahuni (sehemu takatifu) badala ya kuhubiri neno la Mungu, kuhubiri Biblia inasemaje na kumuhubiri Mwenyezi Mungu. Kitendo cha kutelekeza neno la Mungu na kuvaa uanasiasa si tu kuwagawa Waumini wake bali pia ni kutikisa misingi ya amani ambayo imejengwa kwa gharama kubwa za jasho, mateso na kujitoa kwingi kwa Waasisi wetu. Kakobe nenda katubu kwa uchochezi huu.

Askofu Kakobe alitakiwa ajipe muda wa kutosha wa kufikiri juu ya matendo yake na kauli zake kabla ya kuzitoa madhabauni. Alipaswa kujifunza faida na hasara zake.

Askofu Kakobe alitakiwa aendelee kujifunza juu ya mwelekeo wa Tanzania Mpya na mwelekeo wake Mpya kwa sasa. Tanzania mpya ya sasa inayoongozwa na Rais Magufuli haina muda wa siasa za chini ya Mwembe tena.

Kwa Wahubiri wanasiasa kama Kakobe watamuona Magufuli ni tatizo ila kwa Watanzania Wazalendo tunamuona Rais Magufuli ni Mkombozi kwa Taifa letu. Tunamuona Rais Magufuli ndiye Mussa wa Watanzania wetu kwa sasa anayetutoa Misri kwenye mateso, anatuvusha bahari ya Shamu na kutupeleka Kaanani, nchi ya Maziwa na Asali. Daima sisi Watanzania wanyonge tutaendelea kumuunga mkono Rais Magufuli siku zote, nyakati zote.
 
Back
Top Bottom