figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
ASKOFU wa Kanisa la Full Gospel Bible Felloship (BGBF), Zachary Kakobe yupo wapi?
Ni mwaka wa pili sasa haonekani Kanisani. Hata Mke wake anaweza kuja Kanisani mara Moja kwa mwezi.
Je, kuna aliyemuona Askofu huyu huko mliko au kukutana naye?
Na wanaosambaza habari eti kapoteza kumbukumbu, naomba hizo habari msinipe mimi kwani nyie sio wasemaji wa Familia au Kanisa.
Kama anaumwa augue pole ila Kakobe ni Baba yetu wa Kiroho na tunamtegemea kwa Huduma.
Kanisa au Familia ijitokeze iseme yupo wapi ili kuondoa minong'ono isiyo furahisha. Baba yetu yupo wapi?
Kakobe anachunga kanisa Kubwa sana Dar-Es-Salaam, ambalo ni kanisa mama na amewafundisha yeye mwenyewe na kuwatuma kwenye mashamba ya Bwana zaidi ya wachungaji 700.
Jumapili, tarehe 7 Machi, 1993; aliwatawadha kundi la kwanza la wachungaji 28 (Wachungaji 19 na Wachungaji Wasaidizi 9); na kuwapa mamlaka ya kufungua makanisa tanzu ya kwanza 19 (au makanisa mtoto), katika makao makuu ya mikoa yote 19 iliyokuwepo Tanzania bara enzi hizo;
Na Februari 2000, Kakobe tayari alikuwa ameshaanzisha zaidi ya Makanisa tanzu 400 (au Makanisa mtoo) yaliyo tapakaa mikoa na wilaya yote ya Tanzania bara.
Mara ya mwisho mimi kumuona alikuwa na Hayati Magufuli katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya TCRA Jijini Dar es salaam
Ni mwaka wa pili sasa haonekani Kanisani. Hata Mke wake anaweza kuja Kanisani mara Moja kwa mwezi.
Je, kuna aliyemuona Askofu huyu huko mliko au kukutana naye?
Na wanaosambaza habari eti kapoteza kumbukumbu, naomba hizo habari msinipe mimi kwani nyie sio wasemaji wa Familia au Kanisa.
Kama anaumwa augue pole ila Kakobe ni Baba yetu wa Kiroho na tunamtegemea kwa Huduma.
Kanisa au Familia ijitokeze iseme yupo wapi ili kuondoa minong'ono isiyo furahisha. Baba yetu yupo wapi?
Kakobe anachunga kanisa Kubwa sana Dar-Es-Salaam, ambalo ni kanisa mama na amewafundisha yeye mwenyewe na kuwatuma kwenye mashamba ya Bwana zaidi ya wachungaji 700.
Jumapili, tarehe 7 Machi, 1993; aliwatawadha kundi la kwanza la wachungaji 28 (Wachungaji 19 na Wachungaji Wasaidizi 9); na kuwapa mamlaka ya kufungua makanisa tanzu ya kwanza 19 (au makanisa mtoto), katika makao makuu ya mikoa yote 19 iliyokuwepo Tanzania bara enzi hizo;
Na Februari 2000, Kakobe tayari alikuwa ameshaanzisha zaidi ya Makanisa tanzu 400 (au Makanisa mtoo) yaliyo tapakaa mikoa na wilaya yote ya Tanzania bara.
Mara ya mwisho mimi kumuona alikuwa na Hayati Magufuli katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya TCRA Jijini Dar es salaam