Askofu Kakobe Asipuuzwe: Ni kama David Koresh na Camp Davidians!

Ndugu yangu inawezekana kakobe akawa na nguvu ...lakini kwa kuwa yeye naye ni mwanadamu anaweza kutumia nguvu au ushawishi wake vibaya....hainiingii akilini kuona kakobe anapingana na serikali..bila sababu za msingi..

umeme unapita ndani ya hifadhi ya barabara ambayo inamilikiwa na TANROAD ..ambao wameshawapa kibali TANESCO...ndani ya hifadhi ya barabara ndipo panapohusu upanuzi wa barabara,mitaro,simu,gesi,umeme,maji etc...zote hizo ni huduma za jamii...ambazo ndugu kakobe hazipiti kwenye eneo la miliki yake....isitoshe hata mabango yake ameweka kwenye eneo la TANROADS tena bila kibali chochote...kimsingi kakobe hana haki yeyote pale zaidi nafikiri anazo hasira ....labda kwa kushindwa kuzuia kisheria wakati eneo lake lote la parking la kanisa alilojengaga barabarani lilipobomolewaga wakati wa kupisha upanuzi wa barabara ya Sam nujoma.........

serikali ya kikwete ina staha sana na huruma nadhani ...nafikiri angekuwa ni mkapa angembomolea kama alivomvunjia parking mwaka 2005.....na kakobe anautumia vibaya upole wa kikwete....

jambo lingine ambalo ni hatari kwa usalama ..linalotokea mara ya pili sasa ni la baadhi ya viongozi wa dini kama hawa kutumia misingi ya imani kuwachochea waumini wao kufanya jambo...tuliona wakati viongozi wa dini walipotumia imani kali ya kikristo kuingiza DECI na kuwafanya waamini kuwa DECI ni mkombozi aliyeletwa na YESU.....sasa kakobe anawafanya watu waache kulala makwao na wake zao au waume zao ...wanakesha wanaumwa na mbu kulinda eneo ambalo si la kwao kisheria ....nafikiri iikiendelea hivi badi anao uwezo wa kuwashawishi wajichome moto kama kibwetere[samahani kwa kufikia hapo]...lakini ndiko tunakoelekea kama tutaruhusu watu watumumie imani za waumini wau ..kuwatumikisha watakavyo!!!......

ni bora watu wa usalama wakawa makini na kuibuka kwa fundamenalism ...iwe kwenye christian everngelism au muslim ...zote ni sawa ...pamoja na kuwa ndugu zetu yao inatokuwa movements tofauti na ya wakristo ambayo mtu mmoja anaweza kuwakusanya watu kama mazoba na wakasahau kila kitu na kumfuata yeye....badala ya Mungu!!!

Unncecessary OVER-ANALYSIS na inalenga kupotosha ukweli. Suala la Waumini wa Kakobe kusimamia kile wanachokiamini ni sahihi kipimwe kwa hoja na sio hizi ad hominem. Vyombo husika vitalifanyia kazi hili suala kwa taratibu zilizopo. Haya mengine ni yenu na ni vyema mkadili nayo wenyewe kwenye vichwa vyenu.
 
Saa hizi ni Saa 8:39 za usiku!, yaani usiku wa manane, nimepita nje ya kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, la Askofu Zakaria Kakobe, nikushuhudia mamia ya waumini wake wamekaa kwenye viti na meza nje ya kanisa hilo huku limepambwa na disco lights zinazobadilika badilika rangi, kwa mgeni aweza dhania ni night club fulani.

QUOTE]

Ndugu yangu inawezekana kakobe akawa na nguvu ...lakini kwa kuwa yeye naye ni mwanadamu anaweza kutumia nguvu au ushawishi wake vibaya....hainiingii akilini kuona kakobe anapingana na serikali..bila sababu za msingi..

umeme unapita ndani ya hifadhi ya barabara ambayo inamilikiwa na TANROAD ..ambao wameshawapa kibali TANESCO...ndani ya hifadhi ya barabara ndipo panapohusu upanuzi wa barabara,mitaro,simu,gesi,umeme,maji etc...zote hizo ni huduma za jamii...ambazo ndugu kakobe hazipiti kwenye eneo la miliki yake....isitoshe hata mabango yake ameweka kwenye eneo la TANROADS tena bila kibali chochote...kimsingi kakobe hana haki yeyote pale zaidi nafikiri anazo hasira ....labda kwa kushindwa kuzuia kisheria wakati eneo lake lote la parking la kanisa alilojengaga barabarani lilipobomolewaga wakati wa kupisha upanuzi wa barabara ya Sam nujoma.........

serikali ya kikwete ina staha sana na huruma nadhani ...nafikiri angekuwa ni mkapa angembomolea kama alivomvunjia parking mwaka 2005.....na kakobe anautumia vibaya upole wa kikwete....

jambo lingine ambalo ni hatari kwa usalama ..linalotokea mara ya pili sasa ni la baadhi ya viongozi wa dini kama hawa kutumia misingi ya imani kuwachochea waumini wao kufanya jambo...tuliona wakati viongozi wa dini walipotumia imani kali ya kikristo kuingiza DECI na kuwafanya waamini kuwa DECI ni mkombozi aliyeletwa na YESU.....sasa kakobe anawafanya watu waache kulala makwao na wake zao au waume zao ...wanakesha wanaumwa na mbu kulinda eneo ambalo si la kwao kisheria ....nafikiri iikiendelea hivi badi anao uwezo wa kuwashawishi wajichome moto kama kibwetere[samahani kwa kufikia hapo]...lakini ndiko tunakoelekea kama tutaruhusu watu watumumie imani za waumini wau ..kuwatumikisha watakavyo!!!......

ni bora watu wa usalama wakawa makini na kuibuka kwa fundamenalism ...iwe kwenye christian everngelism au muslim ...zote ni sawa ...pamoja na kuwa ndugu zetu yao inatokuwa movements tofauti na ya wakristo ambayo mtu mmoja anaweza kuwakusanya watu kama mazoba na wakasahau kila kitu na kumfuata yeye....badala ya Mungu!!!

kaka umeongea point nzuri, lakini pia kakobe si mjinga kiasi hicho kuna mambo ya msingi anayodai au anaona hajatendewa haki katika zoezi hili, kwa hiyo lazima pia tupate facts toka upande wa pili.
 
kaka umeongea point nzuri, lakini pia kakobe si mjinga kiasi hicho kuna mambo ya msingi anayodai au anaona hajatendewa haki katika zoezi hili, kwa hiyo lazima pia tupate facts toka upande wa pili.

Wakati mwingine humu kunakujaga sweeping statements and baseless sentiments based on nothing really. Watu humu hata hawajishughulishi kujua case ya upande wa Kanisa la Kakobe ikoje tayari wamesha-jump kwenye conclusion.
 
Msingi wa hoja ya Pasco ni mmoja tuu, KAKOBE ASIPUUZWE. Yakuwa ananguvu na ushawishi mkubwa au kile anacho kipigania ni sahihi au si sahihi, bado hoja inasimama palepale kuwa KAKOBE ASIPUUZWE.
 
Msingi wa hoja ya Pasco ni mmoja tuu, KAKOBE ASIPUUZWE. Yakuwa ananguvu na ushawishi mkubwa au kile anacho kipigania ni sahihi au si sahihi, bado hoja inasimama palepale kuwa KAKOBE ASIPUUZWE.

Asipuuzwe ktk context gani ??? Na nani anastahili kupuuzwa??
 
Kaka niamini mimi, lazima Tanesco wafanye mazungumzo na hawa waumini na wasithubutu kujaribu kupitisha nyaya hizo bila ridhaa yao, kama hujaona vita kali jaribu kucheza na imani ya watu.

Hata mi nilipita nikaona wanalala nje nafikiri wana zaidi ya wiki sasa, mtu anayelala nje yupo tayari kwa lolote mkuu

Tanesco ikijaribu kufanya kazi yao kwa nguvu ya serikali basi yatakuwa ya mwembechai mengine.

Ni kweli kakobe ana nguvu - we kama unabisha nenda kaongee na yeye leo utamkuta pale then uje utupatie update.

ugomvi wangu ndio hapo ...kwani nini kakobe anatumia HUMAN SHIELD....tuseme serikali ikija na nguzo pale yakatokea mapigano ...wakafa ..atajibu nini kwa Mungu...??? je si biblia inayotaka tuwe wanyenyekevu??? mbona misamaha ya kodi ilipofutwa hatukuandamana wala kulala barabarani ...viongozi waerevu wa dini waliifuata serikali kwa HOJA hoja hadi ikasalimu amri??? serikali zetu zimekuwa zikiheshimu dini ....nadhani kwa kujenga hoja tu ingetosha kuitisha serikali ...kuliko kutumia human shield ..thats my main concern ,,...inayopelekea kuamini kuwa wale watu anaweza kuwaambia wafanyelolote wakakubali..analewa influence..Naogopa hasaa!!!
 
Huu ni uzembe wa vyombo vya dola. Hakuna mtu au kikundi cha watu wenye nguvu ya kuvunja sheria na dola ikawaangalia tu bila kutoa jawabu.

Polisi wanatakiwa wawakamate mmoja mmoja hao wanaozuia kazi ya TANESCO na ikiwezekana kuwafungulia mashitaka.

Whether Kakobe ana mazingaombwe au la is immaterial. Sheria ni msumeno.
 
Yule aliyesema kwamaba Askofu Kakobe asifananishwe na kina David na Kibwetere hajasema kwa nini? What is their difference? Au ni kwa vile Kakobe hajaleta maafa kama wale?
 
Katika pitapita nimegundua kuwa Kakobe ni mwepesi saaaaaaaaaaaana: Hebu check li-index page la website yake! Hana cha kuogopwa hao waumini wanalala pale kwasababu wanapewa japo milo miwili kwa siku na sehemeu ya kulala bure!

underconstruction.gif


Yours in His service,

Bishop Zachary Kakobe
 
Many of the Kakobe followers,hawaijui hiyo nguvu unayoiongelea.Lakini amini nakwambia mimi nimekuwa naangalia vipindi vya kakobe kwenye TV na mara zote nikiyaangalia macho yake huwa napatwa na hali ya wasiwasi mkubwa sana moyoni mwangu.nimekuwa ni mtu wa kujua watu wabaya tangu utotoni mwangu kwa kuwaangalia tu machoni mwao.Ila kwa Kakobe sijajua,labda mimi ndio mbaya.
There is something extraordinary in him that i cant explain
.na ninadhani hiyo ndiyo nguvu unayoingelea.
Huenda akawa ndiye muwakilishi wa mpinga kristo
 
Many of the Kakobe followers,hawaijui hiyo nguvu unayoiongelea.Lakini amini nakwambia mimi nimekuwa naangalia vipindi vya kakobe kwenye TV na mara zote nikiyaangalia macho yake huwa napatwa na hali ya wasiwasi mkubwa sana moyoni mwangu.nimekuwa ni mtu wa kujua watu wabaya tangu utotoni mwangu kwa kuwaangalia tu machoni mwao.Ila kwa Kakobe sijajua,labda mimi ndio mbaya.
There is something extraordinary in him that i cant explain
.na ninadhani hiyo ndiyo nguvu unayoingelea.
Huenda akawa ndiye muwakilishi wa mpinga kristo
Asante sana Notradammus, wewe ni mmoja kati ya wachache sana wenye jicho lenye uono wa nilichokiona mimi mpaka kusitisha interview.
Ili kuona hicho unachoona kwenye macho ya Askofu Kakobe, ujue na wewe u miongoni mwa watu wenye extra ordinary powers ila bado hujajua kuwa unazo, hivyo huzitumii, kitendo pekee cha kuona nilichokiona kwenye macho hayo, ni uthibitisho.

Posession ya powers sio kitu kibaya, its always good to have powers, unalolitaka linakuwa, only the use of those powers ndio what maters, some are putting them to a good use, like faith healing, some are using them as a means to gain weathy, some for political powers, some for communications, etc, yet some are abusing them, ndio hao kina David Koresh.

Concern yangu ni kuwa Askofu Kakobe has the powers, is he putting them to a good use or abusing then in the name of God?
 
Pasco and Notradamus please make the thread as a place to educate people,

what power are you talking about? what are the sources of your power? how your power and Kakobe's power can be evaluated? whose power is greater? why and what criteria are you using to say Kakobe as something 'uncommon' ?

Use criteria and standard please to analyse this issue; hizi za kufikirika mnazozisema hapa haziiingii akilini.

However, in bible we believe in the power of Holy Spirit if and only if that man is the man of God. We believe Holy spirit can do supernatural things , yes we believe miracles and all that Jesus did because he was filled with holy spirit. Yet today we are celebrating the promise of Holy spirit, if you repent and believe.

So power which you are talking about, I can describe through bible in my knowledge. However the power that you are taking about we need your education! and should be describable! otherwise tusipoteze muda.
 
Concern yangu ni kuwa Askofu Kakobe has the powers, is he putting them to a good use or abusing then in the name of God?

Here you need to know which power! Holy spirit gift is not permanent, if you abuse will flee!
 
Many of the Kakobe followers,hawaijui hiyo nguvu unayoiongelea.Lakini amini nakwambia mimi nimekuwa naangalia vipindi vya kakobe kwenye TV na mara zote nikiyaangalia macho yake huwa napatwa na hali ya wasiwasi mkubwa sana moyoni mwangu.nimekuwa ni mtu wa kujua watu wabaya tangu utotoni mwangu kwa kuwaangalia tu machoni mwao.Ila kwa Kakobe sijajua,labda mimi ndio mbaya.
There is something extraordinary in him that i cant explain
.na ninadhani hiyo ndiyo nguvu unayoingelea.
Huenda akawa ndiye muwakilishi wa mpinga kristo

Mkuu hapa Tanzania tulikuwa na J.K. Nyerere, na yeye alikuwa na yale macho... thank God hakuyatumia maguvu vibaya sana, he used them for poor people

Kakobe ni hatari kidogo
 
Kwani nani anampuuzia Kakobe? Wewe au nani? Au utueleze unaposema asipuuzwe una maanisha nini? Kama watu wasipompuuza unamaanisha wachukue hatua gani, kanisa lifungwe au? Nijibu hayo maswali, otherwise mi ntaona hapa unaendeleza majungu tu ya miaka nenda rudi kuhusu kakobe na hakuna aliyetokea kuthibitisha. Na Kakobe mwenyewe alishafanya kipindi maalum katika TV kuelezea mambo yote watu wanayomtuhumu na akajibu tuhuma zote, akaonyesha mpaka kwake na mali zake, waumini wakahojiwa kuhusu hayo madai mnayosema , kungekuwa na ukweli katika yote yanayosemwa muda wote huu ukweli ungekuwa umeshasurface.

Pia kama ndugu yangu Kakobe alipokuangalia ukaanza kutetema tatizo sio Kakobe, tatizo ni wewe ndani ya roho yako,wakati unauliza maswali haukuwa na nia ya kufahamu ukweli, bali ilikuwa katika kuharibu ,yaani ulishamuhukumu kabla,roho ya shetani ilikuwa ndani yako, na kutetemeka kwako ni kuwa roho ya shetani alikuwa anapigwa na roho wa Mungu.
 
Many of the Kakobe followers,hawaijui hiyo nguvu unayoiongelea.Lakini amini nakwambia mimi nimekuwa naangalia vipindi vya kakobe kwenye TV na mara zote nikiyaangalia macho yake huwa napatwa na hali ya wasiwasi mkubwa sana moyoni mwangu.nimekuwa ni mtu wa kujua watu wabaya tangu utotoni mwangu kwa kuwaangalia tu machoni mwao.Ila kwa Kakobe sijajua,labda mimi ndio mbaya.
There is something extraordinary in him that i cant explain
.na ninadhani hiyo ndiyo nguvu unayoingelea.
Huenda akawa ndiye muwakilishi wa mpinga kristo

Kakobe hana lolote laiti kama waziri wa nishati na madini angekuwa Dr. John Pombe Magufuli ndo kakobe angejua kuwa yeye si mali kitu. Anamtunishia misuli ngeleja kwa sababu anajua dogo yule ni bogus.
 
Hoja ya Pasco kuwa Kakobe asipuuzwe ni angalizo kuwa jamani tuwe waangalifu kama jamii na viongozi wa dini wa mfano wa Kakobe kwani huko nyuma watu wamepoteza maisha kwa kufuata maelekezo ya viongozi kama hawa na ndio akatoa mfano wa Koresh na Davidians kule U.S.A. na Kibwetere kwa jirani zetu Uganda!! Sio hao tu nakumbuka miaka ya nyuma kuna waumini waliojiua kwa kunywa sumu kwa maagizo ya kiongozi wao kule Georgetown Gayana!! Pasco alichotoa ni tahadhali ya kuepusha shari!!
 
Back
Top Bottom