Arusha: Usafiri wa daladala kurejea, madereva wamaliza mgomo

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Mgomo huo ulioibuka asubuhi ya leo Julai 3, 2023 baada ya madereva Daladala kudai kuingiliwa ruti na wenzao wa Bajaj, hatimaye wameyamaliza na usafiri unaratijiwa kurejea kama kawaida kuanzia asubuhi ya Julai 4, 2023.

Baada ya mazungumzo hatimaye maridhiano yamefikiwa kati ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) na madereva wa daladala.

Akizungumza na madereva waliogoma kwenye Stendi ya Kilombero, Afisa Mwandamizi wa LATRA, Amani Mwakalebela ametangaza kurejea kwa usafiri huo kutokana na maridhiano hayo.

Amesema kuanzia Julai 10, 2023 itakuwa mwisho wa Bajaj kwenda Mjini au kujihusisha na majukumu yanayofanana na daladala, badala yake wanatakiwa kukodishwa na si kukusanya abiria kama daladala wanavyofanya.

3ceb53fb-03a1-44fb-b530-f71e7abf5fde.jpg

Hali ilivyo Kwa Morombo jijiji Arusha Kwenye mgomo wa Daladala usiokuwa na kikomo madereva wakilalamikia kuongezeka kwa Bajaji jijini Arusha na Kuwaingilia kwenye Ruti zao ambapo Wananchi wametumia usafiri wa Mguta, Julai 3, 2023 kuingia mjini.


Pia soma: Mgomo wa Daladala Jijini Arusha asubuhi hii ya Julai 3, 2023
 
Mgomo huo ulioibuka asubuhi ya leo Julai 3, 2023 baada ya madereva Daladala kudai kuingiliwa ruti na wenzao wa Bajaj, hatimaye wameyamaliza na usafiri unaratijiwa kurejea kama kawaida kuanzia asubuhi ya Julai 4, 2023.

Baada ya mazungumzo hatimaye maridhiano yamefikiwa kati ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) na madereva wa daladala.

Akizungumza na madereva waliogoma kwenye Stendi ya Kilombero, Afisa Mwandamizi wa LATRA, Amani Mwakalebela ametangaza kurejea kwa usafiri huo kutokana na maridhiano hayo.

Amesema kuanzia Julai 10, 2023 itakuwa mwisho wa Bajaj kwenda Mjini au kujihusisha na majukumu yanayofanana na daladala, badala yake wanatakiwa kukodishwa na si kukusanya abiria kama daladala wanavyofanya.

View attachment 2677581
Hali ilivyo Kwa Morombo jijiji Arusha Kwenye mgomo wa Daladala usiokuwa na kikomo madereva wakilalamikia kuongezeka kwa Bajaji jijini Arusha na Kuwaingilia kwenye Ruti zao ambapo Wananchi wametumia usafiri wa Mguta, Julai 3, 2023 kuingia mjini.


Pia soma: Mgomo wa Daladala Jijini Arusha asubuhi hii ya Julai 3, 2023
Japo watu wa bajaji imekula kwao, maana watu wachache Sana wanaweza kukodi bajaji

Kuunganisha abiria wanne inasaidia,
ila hao madereva wa hiace Wana roho mbaya, mwendo wa kuwaharibia wenzao
 
Japo watu wa bajaji imekula kwao, maana watu wachache Sana wanaweza kukodi bajaji

Kuunganisha abiria wanne inasaidia,
ila hao madereva wa hiace Wana roho mbaya, mwendo wa kuwaharibia wenzao
Wabadilsihe tu pale mbele waweke kibao cha Private, ila kuunganisha abiria itaendelea kama kawa
Pia waache kwenda stendi, hiyo ndio iliwaharibia
 
Arusha Kuna shida sana na sijawahi ona watu primitive kama wa Arusha.Sasa hizo Bajaj si waache wafanye kazi Kwa uhuru Kwani nao si wanalipa Kodi Latra hapo mmezingua kwanza usafiri wenyewe huo wa vifodi umepitwa na wakati ni magari ya kubeba watoto wachekechea.Arusha badilikeni kwahiyo nako kungekuwa na mradi wa mwendo Kasi kama dar mngegoma?Biashara huria Wacha watu wafanye kazi.
 
Wamedanganywa hiyo tar 10 hamna lolote bajaj zitaendelea kama kawaida hakuna mgomo wa kunyimana rizik unaokubalika, biashara ni ushindani ukiona umezidiwa hamisha gari lako ndio maana hawajapewa majibu yanayoeleweka hata leo tar 4 kuna wanaofanya kazi wengine wanaendelea na mgomo.Pia ujue serikali wanatumia hekima hawakurupuki wanaangalia bajaj zimeajiri vijana wangap? Je Wakizuiwa wataishije?
 
Back
Top Bottom