Are you intellingent? jibu swali hili!

Nadhani jibu ni Taifa la watu walikata tamaa ila nakuonea wivu elza zote hizo bucho na hizo ela zako, wewe mtoto wa Chenge nini maana hujajibu swali la jamaa
 
Last edited by a moderator:
nyie endeleeni kupiga majungu msifanye kazi , wengine tunazidi kuzikusanya.

224398_128941473864694_761823_n.jpg

Jirani yako kama ana njaa wewe huna UTULIVU WALA AMANI!
 
=Migomo isiyoisha
Mjerumani alikuwa mkoloni Mchoyo, ubahiri wake na uchoyo vilimfanya anyang'anywe makoloni yake yote na tawala zote kuchukuliwa na Waingereza. Wakoloni hao waingereza baada ya kuchukua dola waliamua kufanya kazi na babu zetu ambao walikuwa na serikali zao za kijadi kupitia watawala walioitwa Watemi (chiefs). Babu zetu hao walikuwa chini ya Local Government na wao kubaki kama serikali Kuu. Kama haitoshi, waingereza waliamua kusomesha watoto wa watemi hao ili walau kuwepo na balance of power and ideas kwani wao kwa kipindi hicho wasomi wao walifika shahada za uzamivu wakati babu zetu walikuwa na shahada za ndoa nyingi. Miongoni mwa watoto wa ma chief waliosoma ni pamoja na hayati mwalimu nyerere baba wa Taifa letu na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru mtoto wa Chief Kinjekitile Ngwale wa Ngalambe, majimaji resistance Leader of almost 20 tribes along east southern part of Tanganyika. Watawala wa sasa akiwemo mhe Jakaya M Kikwete ni miongoni mwa Viongozi walioandaliwa na Baba wa Taifa kuongoza Taifa. Ushahidi wa jambo hilo ni uchaguzi wa 1995 akiwa na umri wa miaka 45 tu alivyokuwa na mvuto katika jamii ikimtaka kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano. Ushaidi wa pili ni kura za mwaka 2005 ambazo zilimuingiza madarakani kwa asilimia 81. Kama haitoshi aliendelea na awamu ya pili kwa kuzoa asilimia 61 ya kura zote akiwaachia Lipumba, Slaa na wenzao kugawana zilizosalia. Ni watanzania ninyi ndo mlipiga kura hizo na sasa mmekuwa kama ringtones za simu za kichina kila siku tantarila tantarilaaaaa. Hivi sasa hamsemi ni yupi mnamtaka zaidi ya kukosoa tu. Ninachokiamini mimi ni kwamba Taifa la Tanzania lina histroia yake kama yalivyo mataifa mengine duniani. Kwamba, nchi haiwezi kukabidhiwa kwa Mbwa. Mbwa wanajijua siwezi kuwataja hapa, ila utawatambua watapoanza kubweka, wewe fuatilia tu thread hii utagundua na kubaini mbwa hao. Tofauti yao ni kwamba wengine ni dobberman, germany shepherd, lotoiller na Tanzania koko. Mabadiliko yanaweza kuja kwa nguvu za hoja na siyo haja za nguvu. Jambo usilolijua bwana ni sawa na usiku wa giza.

Hebu sasa na tuone huyu Ulimboka ni nani tena.
Ulimboka bwana ni Daktari Muungwana sana. Mtu anayekubali kukaa meza ya mazungumzo na anayeamini anakandamiza maslahi yake anapaswa kupewa sifa kwani anadiriki na kuthubutu. Lakini tukio lililomkuta lina utata sana. Kwetu gamboshi ukikuta mtu kakorofishana na jirani yake, wachawi hupata mwanya wa kumfanyia kitu mbaya waliyemnuia ili aone kuwa mbaya wake ndo katekeleza tendo hilo. Na ikitokea aliyefikwa na balaa hilo la mchawi amekwenda kwa mganga kucheck mambo, mara nyingi huambiwa mbaya wako ndo ametekela ubaya huo. Mganga husoma mazingira kuwa kila mwanadamu huwa na adui ama mbaya wake hivyo lazima utachukua maamuzi magumu dhidi yake. Hebu tuwafikirie ndugu waliofiwa jamaa zao wa karibu kama vile watoto, wazazi, wake ama waume zao kwa ajili ya mgomo wangekutana na ulimboka ingekuwa vipi. Hebu tuwafikirie wakubwa waliomwaga unga kwa ajili ya shinikizo la ulimboka na kikundi chake cha madaktari hamad kibindoni wakutane naye kona ingekuwa vipi. Hebu tuwafikirie wale ambao waliona mazungumzo baina yake yanaelekea kupata ufumbuzi unadhani wangemkuta kona usiku ingekuwa vipi, nadhani ingekuwa kwa Yartzyak Rabib the late ex-Israel's Prime Ministj
 
Back
Top Bottom