Anguko la January Makamba

Jazzie

Member
Jan 30, 2008
73
35
Acts 13:36 – “For when David had served God's purpose in his own generation, he fell asleep; he was buried with his fathers and his body decayed

Ni ukweli usiopingika kwamba kila kizazi kinahitaji kiongozi wake. Hiyo ni kwa sababu kila kizazi kina matatizo yake, maono yake, na matakwa yake. Ni ukweli usiopingika kwamba kizazi cha Tanzania leo hii kina kiu ya kiongozi wake.

Kwa muda ilionekana kama vile kuna vijana wawili – January Makamba and Zitto Kabwe, ambao walikuwa tayari kubeba jukumu la kusimama kama nyota ya uongozi wa kizazi kipya. Kili mmoja wetu anajua kilichojiri Bungeni hivi karibuni, hasa uamuzi wa January Makamba kupingana na hatua aliyoingoza Zitto Kabwe ya kudai uwajibikaji serikalini.

Ni dhahiri, ingawa wengine wanaweza kuwa na maoni tofauti, kwamba January amejiweka katika wakati mgumu kisiasa, hasa mbele ya vijana waliomtegemea.

Kwa muda January Makamba aliweza kung’ara katika anga za siasa Tanzania kwa sababu ya uwezo wa kupambanua mambo. Lakini kilichotokea Bungeni kimedhihirisha kitu kimoja – uwezo wa January kupambanua mambo na kutoa kauli “zilizoenda shule” peke yake hakumfanyi mtu kuwa kiongozi na shujaa wa kizazi chake. Kuna wakati na mazingira yanamtaka kiongozi kudhihirisha mawazo na moyo wake ulipo.

Pale Bungeni, wakati huo ulitokea na bahati mbaya sana January akaugopa wakati huo.

Pale mjengoni, January Makamba alidhihirisha kwamba mawazo yake na moyo wake yako mbali kama Mashariki iliyo mbali na Magharibi. Na ndio maana dhana ya “unafiki” inamzonga January. Katika utetezi wake, January Makamba aliandika hiki hapa chini:

"I can disagree with Zittokabwe on methods to reach the same objectives, and we are still brothers"

Mpaka leo sijasikia chochote toka kwa January kuhusu njia mbadala (tofauti na njia aliyopendekeza Zitto Kabwe) ya kuleta uwajibikaji serikalini. Kwa mantiki hiyo, hiyo kauli yake hapo juu ilikuwa ni jitihada tu ya kuzima zengwe na jinamizi la kisiasa linalomkabili.

What a waste.
 
Last edited by a moderator:
Mimi sijawahi kumweka kwenye list ya viongozi watarajiwa wa nchi hii

january was my first choice tena mbele ya ZITTO
ILA KWA SASA NAONA NAFUU UWE NA WATU KAMA SOFIA SIMBA kuliko kuwa na JANUARI

JANUARI kajiaribia sana na kwa kifupi kajimaliza sitokaa nimwamini tena

big up zitto
 
Huyu kijana sijawahi kuona umuhimu wake wala uhazina wake kwa taifa; kwangu mimi yeye ni sawa tu na Nape na William Malecela- wapo kulinda mzimu CCM kwa vile wazazi wao walipita huko- they cant forget honey and milk they have enjoyed since were born.
 
Mimi sijawahi kumweka kwenye list ya viongozi watarajiwa wa nchi hii

Mie labda mnisaidie wana JF, maana hawa wote wenye majina makubwa (kutoka kwa baba zao) huwa nawachukia siamini kwamba wanapata mafanikio kwa kuwa ni wachapakazi. Mwenye ushaidi kunibadilisha mawazo haya niliyonayo please come forward, zawadi nono itatolewa
 
hivi kuna ulazima gani wa watoto nao kuwa viongozi kama baba zao..hapo ndipo ninapopata kichefuchefu..kwani hakuna wengine wa kuongoza..tumejaa tele lakini kubaniana na kupeana nafasi kwa vilaza ndio kunaendelea..
 
the thing is ukiyakumbatia matapishi na yenyewe yakawa mengi nawe unabadilika kuwa sehemu ya hayo matapishi.
hawa jamaa lazima waelewe wananchi wanawaangalia kila step wanayoifanya iwe bungeni au nje ya bunge na siku moja watahitajika kuwajibika juu ya kauli zao zote.

Mungu ibariki Africa Mungu ibariki Tanzania.
 
Acts 13:36 – “For when David had served God's purpose in his own generation, he fell asleep; he was buried with his fathers and his body decayed

Ni ukweli usiopingika kwamba kila kizazi kinahitaji kiongozi wake. Hiyo ni kwa sababu kila kizazi kina matatizo yake, maono yake, na matakwa yake. Ni ukweli usiopingika kwamba kizazi cha Tanzania leo hii kina kiu ya kiongozi wake.

Kwa muda ilionekana kama vile kuna vijana wawili – January Makamba and Zitto Kabwe, ambao walikuwa tayari kubeba jukumu la kusimama kama nyota ya uongozi wa kizazi kipya. Kili mmoja wetu anajua kilichojiri Bungeni hivi karibuni, hasa uamuzi wa January Makamba kupingana na hatua aliyoingoza Zitto Kabwe ya kudai uwajibikaji serikalini.

Ni dhahiri, ingawa wengine wanaweza kuwa na maoni tofauti, kwamba January amejiweka katika wakati mgumu kisiasa, hasa mbele ya vijana waliomtegemea.

Kwa muda January Makamba aliweza kung’ara katika anga za siasa Tanzania kwa sababu ya uwezo wa kupambanua mambo. Lakini kilichotokea Bungeni kimedhihirisha kitu kimoja – uwezo wa January kupambanua mambo na kutoa kauli “zilizoenda shule” peke yake hakumfanyi mtu kuwa kiongozi na shujaa wa kizazi chake. Kuna wakati na mazingira yanamtaka kiongozi kudhihirisha mawazo na moyo wake ulipo.

Pale Bungeni, wakati huo ulitokea na bahati mbaya sana January akaugopa wakati huo.

Pale mjengoni, January Makamba alidhihirisha kwamba mawazo yake na moyo wake yako mbali kama Mashariki iliyo mbali na Magharibi. Na ndio maana dhana ya “unafiki” inamzonga January. Katika utetezi wake, January Makamba aliandika hiki hapa chini:

"I can disagree with Zittokabwe on methods to reach the same objectives, and we are still brothers"


Jamuary Makamba is left by Zito by an interval of 100 spaces interms of intelligence,integrity,accountability and realism.KIJANA AMEPOTEA,HANA MVUTO,AMEPWAYA,ANABOA,ANA UNAFIKI,ANA DHARAU,ANATAKA MADARAKA,ANAJIKWEZA,ANAJIONA,ANATAMAA,ANAUCHOYO.
 
Last edited by a moderator:
Naye anaogopa maana anajua akinyanganywa kadi tukirudi jimboni hana chake mbele ya M4C yenye kasi ya kimbunga.
 
Na mara baaday ya kuona kuwa ameingia cho cha kike siku ile, hakuwa tene na nguvu ya kwenda kusoma majumuisho ya kamati yake badala yake akamrushia yule mama wa singida.

Waliambiwa na V. Nyerere kuwa tegeme utapata nini ukiruka sarakasi huku umevaa taulo!!!! hao ndo majibu yake, na bado!!!
 
Mwenzenu hana hata muda nanyi, ndiyo kwanza anasema wabongo wanachonga sana bila kujua wanaloongea, na wao viongozi wenye kujua hawaongei kuwajuza wabongo katika style ya "aliyelala usimuamshe..."

The nerve...
 
huyo kijana anatamani uwaziri nishati na madini mnafiki tu.
 
Back
Top Bottom