Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Haya wakuu.. kutoka mmoja wetu humu humu:
Toba yarabi.. naenda kulala kwanza!
Kaka Mwanakijiji, tatizo langu ni kuwa mimi ni msichana na ninapenda mahusiano na mtu wa jinsia tofauti. Siku za hivi karibuni kuna dada mmoja ambaye nadhani anapenda mahusiano ya kimapenzi na kina dada wenzake. Kila akiniona huwa anazungumza huku ananirembushia macho na kunikonyeza konyeza.. halafu anataka yaani tuwe marafiki wa karibu. Mwanzoni nilidhani ni urafiki tu hadi pale nilipodokezwa kuwa huyo dada ni mcheza timu ya nyumbani.
Sasa kwa mambo mengine yote ni mtu mzuri lakini naogopa kumzoea au kuwa comfortable sana kwake asije akadhania ndio namkubalia. Juzi kaniomba ati twende Gym pamoja to work out. Kwa kweli najisikia kukwazika. Nifanyeje. Tafadhali usitoe jina langu.
Toba yarabi.. naenda kulala kwanza!