Baba zangu na kaka zangu nakuja tena hodi nyumbani. Msinichoke!

Wrevta

JF-Expert Member
Jan 18, 2023
1,440
1,720
Habari zenu nyote, najua kila mmoja anapitia matatizo yake kivyake ila naomba nipate kibali cha kushauriwa juu ya tatizo langu hili.

Baba zangu, kaka zangu, dada zangu, na rafiki zangu wa MMU; Mimi nina miaka 25 na sijawahi kuwa na mpenzi ingawa ngono ninashiriki kama kawaida.

Nina anxiety, ninapata wapenzi safi tu na wapo wanaoonesha kunipenda ila shida ni pesa, sina pesa za kutosha kuwatosheleza slay queens wa sasa, je, nitadumu nao?

Kuna kaka alileta stori humu kuwa alimnyang'anya rafiki yake mpenzi siku ya sherehe ya kuzaliwa ya mpenzi huyo. Kisa kikiwa ni pesa. Yaani huyo brother na rafiki yake walikwenda ukumbini na kukuta mgogoro, pesa ya sherehe ya mpenzi wake haikutosha na mwenye ukumbi anataka kuwatoa nje.

Huyu brother hakuwa na hela ya kutosha kujazia deni la ukumbi, hivyo rafiki yake akatoa kiasi akajazia (ni kama laki moja hivi), na usiku huo akamlala shemeji yake huyo. Na urafiki wao ukafa siku hiyo. Mapenzi kati ya huyo brother na mpenzi wake yakafa siku hiyo.

Naogopa mno hiki kunikuta. Nafanyaje? Kuwa na mpenzi siyp shida ila je, nitadumu nao na wakati ninasoma, na hela yangu ni ya kuunga unga? Yaani 'pesa ya madafu'?

Nitaweza kumnunulia zawadi za kuanzia laki moja kila birthday yake? Nitaweza kumrushia vocha za 20000 kila akiishiwa salio? Nitaweza kumpeleka lodges na hotels nzuri? Achilia mbali gharama za beach nk!

Naomba mnisaidie maoni yenu... uoga huu umefanya nisiwe na mahusiano mpaka muda huu. Nafikiria mno, wasichana wazuri wanahitaji pesa, mimi nategemea wazazi bado kwa sababu nasoma na sifanyi kazi, wapi nitatoa laki mbili mbili za vacation?

Pia, mimi ni mpole mno na nahitaji nibadilike niwe katili angalau hata kidogo ila naona naharibu tu. Nikisema nijaribu kuwa muongeaji au mcheshi najikuta naharibu tu na kujisikia vibaya, na kuamua kuirejea asili yangu ya ukimya na upole.

Maoni yenu ni muhimu sana. Inafika wakati naona wivu(si wivu mbaya) humu watu wanavyofunguka kuwahonga mamilioni wapenzi wao na hawalalamiki, kumaanisha kuwa wanazo hela za kutosha. Najisikia vibaya kiasi, na kupata hasira ya kutaka kupambana nizishike hela.

Sijawahi hata kutoa 10000 na kumpa msichana. Kuna wakati nawaza hata niwe punda tu wa kusafirisha drugs ili nipate pesa ninazotaka, ili niwe kwenye mahusiano ya kudumu na nipate tendo bila kipimo. Anyways nasikiliza ushauri wenu.

Njia ipi ni sahihi kwa sasa? Uelekeo upi ni sahihi? Nina haja ya kuwa na mahusiano ya kudumu, yatakayonipa uhakika wa tendo la ndoa bila pesa?
 
Achana na wanawakephobia mkuu.

Pesa siyo kila kitu kwenye Mapenzi japo pesa ina nafasi ya kunogesha Mapenzi. Ni kachumbari kwenye pilau la upendo baina ya wawili.

Wanawake ambao hawana tamaa ya pesa bado wanaishi.

Mkuu, kila la heri katika safari yako ya Mapenzi,sisi wengine tumeshakuwa wazee,enzi zetu pesa haikuwa sababu ya kupata wanawake wazuri,Bali ule upendo wa dhati kutoka moyoni.

Mshirikishe Mungu pia akupe mke mwema.
 
Dogo piga shule timiza ndoto zako.

Wengine tulipitia huko huko. Tena tulikua na wapenzi wa ndoto zetu vyuoni tukaja kuporwa na ma-lecturers. Lakini sasa tumepita huko, tuna kazi, tuna vyetu na maisha yamebadilika tunakula pisi zozote tunazotaka.

Nasisitiza ukomae utimize ndoto, kumbuka soko la ajira ni gumu pambana utoboe kimaisha utakula pisi kali mpaka uchoke. Roma alishasema, "Usishindane na mwanamke, Pedeshee atamuonga Noah, wanangu wa Old Moshi someni tu mtatoboa!"
 
Dogo piga shule timiza ndoto zako.

Wengine tulipitia huko huko. Tena tulikua na wapenzi wa ndoto zetu vyuoni tukaja kuporwa na ma-lecturers. Lakini sasa tumepita huko, tuna kazi, tuna vyetu na maisha yamebadilika tunakula pisi zozote tunazotaka...
Huo mstari wa Roma huwa unazunguka kichwani mwangu Sana. Siku hizi sio Noah ni Rumion
 
Achana na wanawakephobia mkuu.

Pesa siyo kila kitu kwenye Mapenzi japo pesa in nafasi ya kunogesha Mapenzi. Ni kavlchumbari kwenye pilau la upendo baina ya wawili.

Wanawake ambao hawana tamaa ya pesa bado wanaishi.

Mkuu, kila la heri katika safari yako ya Mapenzi,sisi we gone tumeshakuwa wazee,enzi zetu pesa haikuwa sababu ya kupata wanawake wazuri,Bali ule upendo wa dhati kutoka moyoni.

Mshirikishe Mungu pia akupe mke mwema.
Napiga magoti kwa imani kukushukuru kwa ushauri huu adhimu. Ahsante!

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Dogo piga shule timiza ndoto zako.

Wengine tulipitia huko huko. Tena tulikua na wapenzi wa ndoto zetu vyuoni tukaja kuporwa na ma-lecturers. Lakini sasa tumepita huko, tuna kazi, tuna vyetu na maisha yamebadilika tunakula pisi zozote tunazotaka....
Sasa wewe unao uhuru huo wa kula pisi utakazotaka, mimi sina, na ndiyo nautaka. Muda ni sasa.

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Miaka 25 ni umri wa kujiandaa kwa ndoa. Jitahidi kupunguza uhuni maana kwenye bandiko lako umesema umetembea na wanawake wengi ila hukuwahi kuwa na mpenzi wa kudumu.

Mungu aibariki safari yako.
Ahsante mzee, shida ni nani msichana mzuri wa kukubali kuolewa na kijana asiye na hela za kutosha, hasa kwa umri huu na ambaye anajitafuta kimaisha?

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Tafuta anaekupenda mkuu me namiliki pisi kali na nina hela za kawaida sana kila nikienda nae mahali watu wote macho kwangu

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Sawa, ila hizo hela za kawaida kwa umri wangu bado sina uhuru nazo. Unaweza kuwa unashika laki 5 mpaka milioni na ukaona hela za kawaida, ukisahau kabisa kwa Watanzania wengi hizo si hela za kawaida.

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom