Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,833
Mtoto wa ajabu amezaliwa akiwa na viungo
vinne vya uzazi vya kiume, sehemu za
kutolea haja kubwa mbili moja ikiwa
mgongoni pamoja na mguu mkubwa wenye
vidole sita ambao nao umeota kati kati ya
mgongo.
Mtoto huyo ambaye mzazi wake Naishooki
(23), anatoka kijiji cha Injok, Wilayani
Arumeru, mkoani Arusha, alizaliwa juzi usiku
kwa njia ya upasuaji katika hospitali ya
Olturumet.
Akizungumza huku akilia kwa uchungu,
mama mzazi wa binti aliyejifungua mtoto,
Naishiye Logolie, alisema hawajawahi kuona
kitu cha ajabu na kutisha kama yaliyotokea
kwa mtoto wao.
Mwanangu alipokuwa mjamzito hajawahi
kuonyesha dalili za tatizo lolote.
Tumechachanganyikiwa kuona kitu kama
hiki. Tunaomba madaktari watusaidie kujua
ni nini hiki. Ni huzuni kwa jamii yangu,
alisema Mama Logolie katika wodi namba
mbili alikolazwa mama wa kichanga hicho.
Alisema mtoto wake alianza kupata
uchungu juzi na walipompeleka katika kituo
cha afya karibu na nyumbani kwao,
walishangaa kupewa rufaa kwenda
Olturumet, ambapo walipofika mdaktari
walimwambia ni lazima afanyiwe upasuaji
haraka kumwokoa mtoto na mama pia.
Aidha, alisema baada ya mwanaye
kupelekwa chumba cha upasuaji, walianza
kusali kuombea upasuaji huo uwe salama,
lakini baada ya upasuaji waliitwa na daktari
na kuambiwa kuwa mzazi yuko salama
isipokuwa kuna tatizo kwa mtoto.
Kwa haraka hatukudhani ni kile ambacho
kimetokea tulifikiri labda mtoto amechoka
sana au ana tatizo la kiafya ambalo
lingekuwa la kawaida, baada ya kuona
maumbile yake nilizimia, sikuamini na hata
sasa siamini mwanangu kazaa mtoto wa
aina hii, alisema Naishiye.
Mganga wa Halmashauri ya Arusha, Dk.
Thobias Mkina, alithibitisha kutokea kwa
tukio hilo na kusema kuwa wanajaribu
kufanya linalowezekana kuokoa maisha ya
mtoto huyo ambaye hajaweza kunyonya
maziwa ya mama yake tangu azaliwe juzi
usiku.
Matukio ya kuzaliwa watoto wakiwa na
matatizo yanatokea, lakini hili kidogo
linaonekana kuwa la kipekee sana kutokana
na maumbile ya mtoto, alisema Dk. Mkina.
Alisema sababu za kitaalamu zinazoweza
kusababisha matukio ya aina hii ni matumizi
ya dawa zenye kemikali na wakati mwingine
kuna matukio ya kurithi kutoka kwa kizazi
cha muhusika.
Hata hivyo, alisema uchunguzi unaendelea
na wakimaliza watampatia rufaa kwenda
katika hospitali kubwa zaidi.
Baada ya taarifa za kuzaliwa kwa mtoto
huyo, watu wamekuwa wakifurika katika
familia ya mwanamke huyo kujua
kilichotokea huku wengine wakisafiri kwa
mwendo wa kilomita zaidi ya 20 kufika
katika hospitali hiyo kumwona mtoto huyo.
Kuzaliwa kwa mtoto huyo mwenye uzito wa
kilo nne, kunatokea siku chache baada ya
tukio la ajabu kutokea katika siku za
karibuni mkoani Arusha la kondoo aliyezaa
kondoo mwenye kichwa cha binadamu
katika eneo la Kiserian, Wilayani Arumeru.
CHANZO: NIPASHE
vinne vya uzazi vya kiume, sehemu za
kutolea haja kubwa mbili moja ikiwa
mgongoni pamoja na mguu mkubwa wenye
vidole sita ambao nao umeota kati kati ya
mgongo.
Mtoto huyo ambaye mzazi wake Naishooki
(23), anatoka kijiji cha Injok, Wilayani
Arumeru, mkoani Arusha, alizaliwa juzi usiku
kwa njia ya upasuaji katika hospitali ya
Olturumet.
Akizungumza huku akilia kwa uchungu,
mama mzazi wa binti aliyejifungua mtoto,
Naishiye Logolie, alisema hawajawahi kuona
kitu cha ajabu na kutisha kama yaliyotokea
kwa mtoto wao.
Mwanangu alipokuwa mjamzito hajawahi
kuonyesha dalili za tatizo lolote.
Tumechachanganyikiwa kuona kitu kama
hiki. Tunaomba madaktari watusaidie kujua
ni nini hiki. Ni huzuni kwa jamii yangu,
alisema Mama Logolie katika wodi namba
mbili alikolazwa mama wa kichanga hicho.
Alisema mtoto wake alianza kupata
uchungu juzi na walipompeleka katika kituo
cha afya karibu na nyumbani kwao,
walishangaa kupewa rufaa kwenda
Olturumet, ambapo walipofika mdaktari
walimwambia ni lazima afanyiwe upasuaji
haraka kumwokoa mtoto na mama pia.
Aidha, alisema baada ya mwanaye
kupelekwa chumba cha upasuaji, walianza
kusali kuombea upasuaji huo uwe salama,
lakini baada ya upasuaji waliitwa na daktari
na kuambiwa kuwa mzazi yuko salama
isipokuwa kuna tatizo kwa mtoto.
Kwa haraka hatukudhani ni kile ambacho
kimetokea tulifikiri labda mtoto amechoka
sana au ana tatizo la kiafya ambalo
lingekuwa la kawaida, baada ya kuona
maumbile yake nilizimia, sikuamini na hata
sasa siamini mwanangu kazaa mtoto wa
aina hii, alisema Naishiye.
Mganga wa Halmashauri ya Arusha, Dk.
Thobias Mkina, alithibitisha kutokea kwa
tukio hilo na kusema kuwa wanajaribu
kufanya linalowezekana kuokoa maisha ya
mtoto huyo ambaye hajaweza kunyonya
maziwa ya mama yake tangu azaliwe juzi
usiku.
Matukio ya kuzaliwa watoto wakiwa na
matatizo yanatokea, lakini hili kidogo
linaonekana kuwa la kipekee sana kutokana
na maumbile ya mtoto, alisema Dk. Mkina.
Alisema sababu za kitaalamu zinazoweza
kusababisha matukio ya aina hii ni matumizi
ya dawa zenye kemikali na wakati mwingine
kuna matukio ya kurithi kutoka kwa kizazi
cha muhusika.
Hata hivyo, alisema uchunguzi unaendelea
na wakimaliza watampatia rufaa kwenda
katika hospitali kubwa zaidi.
Baada ya taarifa za kuzaliwa kwa mtoto
huyo, watu wamekuwa wakifurika katika
familia ya mwanamke huyo kujua
kilichotokea huku wengine wakisafiri kwa
mwendo wa kilomita zaidi ya 20 kufika
katika hospitali hiyo kumwona mtoto huyo.
Kuzaliwa kwa mtoto huyo mwenye uzito wa
kilo nne, kunatokea siku chache baada ya
tukio la ajabu kutokea katika siku za
karibuni mkoani Arusha la kondoo aliyezaa
kondoo mwenye kichwa cha binadamu
katika eneo la Kiserian, Wilayani Arumeru.
CHANZO: NIPASHE