Amelowanisha kitanda chote, nikalale wapi?

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,453
40,446
Wiki iliyopita, nilipata mwaliko kutoka kwa mpenzi wangu (mchepuko), kuwa ananihitaji, niende nikamchangamshe.

Baada ya kunishawishi sana kwa maneno matamu, nikaona bora niende nikamtimizie haja zake; asije akafa bure kwa kukosa huduma muhimu.

Kumbuka; huyu mwanamke ana umbo zuri sana, amekwenda hewani, kiuno nyugwi, chura ndio usiseme, sura inashawishi sana, rangi ya chungwa; ameolewa na ana watoto; mtoto wa kwanza yuko kidato cha sita.

Basi nikamwambie atafute chimbo ambalo atakuwa huru, ili nyumbani kwake wasielewe kinachoendelea.

Basi akaulizia na akafanikiwa kupata chimbo nzuri na kunitumia jina la sehemu, pamoja na maelekezo.

Nilipofika hapo mkoani, nikachukua boda mpaka sehemu husika; kwa ujumla kulikuwa na umbali kwa sababu nilimpa elfu tano.

Mazingira na mandhari ya hiyo lodge yalikuwa yametulia sana, milio ya ndege, na hakuna msongamano wala watu wakusimama simama njiani; kwa haraka haraka nikajua hapa wanandoa wengi huwa wanakuja kusaliti ndoa zao.

Basi wakanipeleka kwenye vyumba; mi nikachagua chumba chenye sebule, ili shoo zianzie sebuleni na baadaye kuitimisha huko chumbani.

Baada ya kuoga na kupata kahawa ili kuondoa baridi na uchovu; naona muhudumu kwa mbali anamleta mwenyeji wangu.

Akagonga mlango, nami nikamfungulia; kwa kweli tunda lilikuwa limekomaa sana na linahitaji kuliwa; ukizingatia nguo ya mitego aliyonivalia, akili ya kawaida ikahama; nikajikuta namkumbatia, nakuanza kubonyeza bonyeza tunda kama limeiva au bado.

Tukajikuta mapigo ya moyo yako juu, mara mguu uko juu ya sofa, mara chuma mboga, mbuzi kagoma, popo kanyea mbingu dah ilikuwa hatari sana.

Baada ya muda akanivuta, na kunipeleka chumbani, huko ndio usiseme, ikawa ni full kulalamika na kumtukana mumewe, kuwa huwa hampelekei shoo za kibabe.

Nikawa naendelea kuchochea kuni ili moto usizime; moto ukawa unawaka kwa kasi sana, matokeo yake, maji ya idara ya maji yakatoka kwa fujo na kwa presha kubwa na kulowanisha kitanda chote.

Baada ya hapo ndipo tumeshtuka; tutalala wapi?, kitanda chote kimelowana.
 
Back
Top Bottom